Ukweli kuhusu nyota

Ukweli kuhusu nyota

Unapotumia nguvu za mashetani au uwezo ambao una ushaidi tosha kuwa si wa Mungu mwenyezi, hapo unafanya uchawi.
Uchawi unatia ndani Kuroga, Pepo, Kuwasiliana na Roho Waovu, na Ibada ya Shetani.

Mungu alikataza uchawi, soma (Mambo ya Walawi 19:26) “Asionekane kwako mtu . . . atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri, wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo.”

Na ukisoma zaidi katika Kumbukumbu la Torati 18:10-11. Utapata elewa zaidi uchawi ni nini.

Kwa kuongezea, Matendo ya Mitume 19:19 "Kwa kweli, idadi kubwa ya wale waliozoea kufanya uchawi wakakusanya vitabu vyao pamoja na kuviteketeza mbele ya kila mtu. Nao wakafanya hesabu na kupata vitabu hivyo vilikuwa na thamani ya vipande 50,000 vya fedha."
.sasa nyota mbona haihusiani Na uchawi au hauna elimu kuhusu nyotaa ?? Au hujui kuhusu mamajusi walifata nin kumwona yesu ??
 
Huwa napenda kufatilia makala zako mkuu kujiongezea maarifa.Katika masuala ya nyota ningependa kujua mtu aliyezaliwa mwezi wa 5 ni nyota gani? Pia katika kusoma makala nyingi nimegundua mtu anaweza tambua nyota yake kwa kuangalia mwezi aliozaliwa au jina lake LA mwanzo.Je ni kwa nn baadhi ya watu akitazama Mwezi wa kuzaliwa na Jina lake la mwanzo anakuta nyota tofauti?
Huwei kusematu mwei wa 5 ana nyota gani pasipo na kujuwa tarehe yake? Sema tarehe na mwei ndio nitajuwa nyota yake ni nyota ipi?
 
MziziMkavu naomba ufafanuzi wa nyota mapacha
coz nimezaliwa June 11

NYOTA YA MAPACHA (GEMINI)

Hii ni nyota ya tatu katika mlolongo wa nyota 12.
Wenye nyota hii ni wale waliozaliwa kati ya tarehe 21 Mei na 20 Juni ya mwaka wowote.
Sayari yao ni Mercury (Attarid).
Siku yao ya bahati ni Jumatano.
Namba yao ya bahati ni 5.
Rangi yao ya bahati ni njano na bluu isiyoiva.
Asili ya nyota yao ni upepo.

KIPAJI CHA MAPACHA: (TELEPATHIC):

Wenye nyota hii wana kipaji kikubwa cha kuwasiliana na watu ambao wako mbali kwa kutumia akili zao au hisia walizokuwa nazo.

TABIA ZA MAPACHA:


Watu wenye nyota hii ni watu wenye hisia kali sana ambao wanakasirika upesi, ni watu wasiotulia na wenye uwezo mkubwa wa kujieleza na kuzungumza na wanaweza sana kushawishi watu.
Ni watu ambao wanapenda sana mabadiliko na tofauti na wanapenda sana kujua mambo, wanapenda watu na wanapenda kujumuika na watu lakini wakati mwingine hawaeleweki. Wanapenda kusafiri sana.

TABIA YA MAPACHA KATIKA MAPENZI:
Watu wenye nyota ya Mapacha wanajulikana sana kwa hadhi yao ya kuwa na sura mbili. Kuna wakati wanakuwa na hisia tofauti na muda si muda wamebadilika.
Pamoja na kwamba hawapendi kubanwa sana , ni watu wachamgamfu na wenye mahaba mazuri.
Ni watu wenye asili ya mawasiliano na ni vigumu sana kuwafanya wajinga hivyo basi wakishampenda mtu wanahakikisha kwamba hawamchoshi huyo mpenzi. Watatumia muda mrefu kuzungumza maneno mazuri na wapenzi wao ili kuhakikisha kuwa uhusiano unazidi kuwepo.
Katika mapenzi, wao wanapenda vitu tofauti tofauti na wanahisi wamechoshwa basi huwa wa kwanza kuondoka aidha kwa muda au moja kwa moja.
Uaminifu ni kitu kigumu kwa watu wenye nyota hii na wanahisi kwamba kuna kitu wanakikosa nje hivyo basi wanatoka sana nje hata kama wakiwa wana ndoa yenye furaha.
Wengi wao wanafikia hatua ya kuishi maisha ya sehemu mbili; mke na bwana au bwana na mke.

MATATIZO YA KIAFYA:
Nyota hii inatawala mabega, mikono, viganja na sehemu ya juu ya mbavu.
Tatizo la kutopumzika kwa sababu ya kutafuta mambo mapya ndio yanayosababisha maradhi kwa wenye nyota hii. Wanafikia mpaka hali ya kuisahau miili yao na mara nyingi wanapata matatizo ya neva kutokana na uchovu kwa mishughuliko mingi.
Matatizo yanayotokana na nyota hii ni mgonjwa kukosa pumzi (bronchitis), pumu (asthma), matatizo ya kifua, mafua, flu, ajali za mara kwa mara kwenye mikono na mabega.

KAZI ZA WENYE NYOTA YA MAPACHA:
Kwa vile wenye nyota hii asili yao ni upepo na wao ni wenye kuzaliwa kwenye mawasiliano na uhusiano, wanapenda sana uhuru na uwazi katika kazi zao.
Wanapenda sana kazi ambazo zinawashughulisha na kufanya akili zao zisipumzike lakini siyo jambo hilo hilo kwa muda mrefu. Kuwa na mawasiliano na watu wengi kwa wakati mmoja ndio jambo linalopendwa na wenye nyota hii. Kazi zao hasa ni zile zinazohusiana na mambo ya utangazaji wa radio na televisheni.
Kazi ambazo zinahusika na mambo ya vitabu au uchapishaji vitabu. Kazi za kufundisha na kazi za ushauri nasaha.
Vilevile wenye nyota hii wanatakiwa wafanye kazi za ukalimani au kazi za biashara lakini zinazohusiana na safari za nje.

FAMILIA ZA MAPACHA:
Watu wa nyota ya Mapacha ni waliochangamka na wenye hiari na wazazi wa Mapacha huingia katika msisimko wa watoto wao kwa raha.
Ni wazazi wenye furaha muda wote katika kutekeleza shughuli zao za nyumbani pamoja na kupenda kucheza na watoto wao na wana mipango mizuri na wanajua wapi wakiwapeleka watoto watafurahi.
wenye nyota hii wanathamini sana elimu na hawawezi kuishi bila mawasiliano na habari, hivyo huwa wanapenda kuwanunulia watoto wao vitabu vingi.
Tatizo linalotokea iwapo mtoto ataonyesha kwamba hapendi kusoma na watajaribu kila njia kumuweka katika njia wanayoitaka wao. Wakishindwa wanaacha.
Wazazi wa Mapacha hawawezi kuelezea jambo na hawana uvumilivu wa kun'gan'gania kwa mtoto asiyeelewa mambo.

MADINI YA MAPACHA:
Wenye nyota ya Mapacha wanatakiwa wavae madini ya Agata au kito chochote chenye rangi ya njano. Kito hicho inasemekana kinamuwezesha mvaaji awe na uwezo wa mawasiliano na ufahamu.

UHUSIANO WA KIMAPENZI:

(MAPACHA NA MSHALE)

Tabia ya Mapacha ya kupenda kufahamu na kuelewa mambo hutulizwa na tabia ya Mshale ambao ni wasomi na wenye kuelewa mambo mengi.

VYAKULA VYA MAPACHA:
Wenye nyota hii wanashauriwa wapende kula vyakula vifuatavyo ambavyo ndio vinavyotawaliwa na nyota yao. Vyakula vyenyewe ni kuku, rasiberi, karoti na uduvi.

NCHI ZA MAPACHA:
Ili kupata mafanikio ya kinyota wenye nyota hii wanashauriwa watembelee au waishi katika nchi au miji ifuatayo inayotawaliwa na nyota yao. Nchi hizo ni Ubelgiji na Wales, na baadhi ya miji ni London (Uingereza) na San Fransisco (Marekani).

RANGI ZA MAPACHA:
Wenye nyota hii wanashauriwa kinyota wapake au watumie rangi za njano au bluu isiyoiva ambayo inapendeza ikipakwa ndani ya nyumba.

Ukiwa na Shida yoyote ile
Usipo pona kwa Dawa za Hospitali nitafute mimi nipate kukutibia upate kupona ukihitaji matibabu yangu
Unaweza kunitafuta kwa Mawasiliano Herbalist Dr. MziziMkavu Email barua ya pepe.fewgoodman@hotmail.com What's App na Viber +905344508169 Au Ni add Kwa Facebook tumia jina hili mzizimkavu. Au boonyeza hapa.Mzizi Mkavu
 
Tarehe 1 November na tarehe 1december
Pia tarehe 28 December

Mwenye Tarehe 1 November ni NYOTA YA NG'E (SCORPIO)

Hii ni nyota ya 8 katika mlolongo wa nyota 12.

Wenye nyota hii ni wale waliozaliwa kati ya tarehe 23 October na 21 Novemba ya mwaka wowote.

Sayari yao ni MARS (MARIIKH).

Siku yao ya Bahati ni Jumanne.

Namba yao ya bahati ni 9.

Rangi ya bahati ni Nyekundu isiyoiva au Maroon.

Asili yao ni MAJI.


KIPAJI CHA NG'E (MYSTICAL)


Wenye nyota hii wana kipaji na uwezo wa kiroho wa kuwasiliana na watu katika kutekeleza mambo wanayohitaji.

TABIA ZA NG'E

Wenye nyota ya Nge wana uwezo mkubwa wa uvuto au kuvutia watu katika mambo yao. Ni watu wenye uelewa mkubwa na ni majasiri katika kukabiliana na matatizo ambayo wengine yamewashinda.

Ni wenye tabia ya kutilia mkazo mambo yao, tena kwa ukali na ikibidi kutumia ukatili ili jambo litimie wao wako tayari.

Ni watu wenye tabia ya siri na wanapenda kufanya mambo yao kwa siri sana.Wenye nyota hii kama ilivyo alama yao hawaogopi kiza. Wana uwezo na kipaji cha asili cha kutekeleza mambo yao na wakafanikiwa.

Ni watu wenye akili nyingi, waerevu na wepesi sana kuelewa mambo.

Watu wa Nge vile vile wana tabia au wanaweza kujidhuru wao wenyewe.Mambo yanapowawia magumu.


TABIA YA NG'E KATIKA MAPENZI

Watu wenye nyota ya Nge wanapenda sana kutumia fursa ya kufanya mapenzi kama njia mojawapo ya kuonyesha ujasiri wao katika mapenzi na namna wanavyojua kufanya tendo la ndoa.

Kwao mapenzi au tendo la ndoa ni kiungo muhimu sana katika maisha yao hasa ikizingatiwa kwamba nyota ya Nge inatawala sehemu za siri.Inashauriwa wale wenye moyo mdogo wasifanye mapenzi na Nge sivyo watajuta. Kitu kingine ni kwamba ni watu ambao hawayumbi na hawakubali kushindwa upesi.

Ni watu wenye ashki na hasira wakiwa wamedhalilishwa au wameumizwa na wapenzi wao na wanapofanya tendo la ndoa hasira zao huisha mara moja.

Ni watu wasiri sana katika masuala ya mapenzi na wanakuwa hivyo ili waweze kuwapata wapenzi wengi kukidhi matakwa au kiu yao kubwa ya ngono.


TABIA YA NG'E KATIKA FEDHA

Hakuna kitu kinachoshindikana kwa wenye nyota hii, na chepesi zaidi ni namna ya kupata fedha. Wana uzoefu mkubwa wa kuhimili matatizo ya kifedha wanapoanguka, hata wakiwa matajiri na wakafilisika.

Watu wa Nge wana bahati ya kuvumbua fedha au utajiri katika njia ambazo watu wengine si rahisi kugundua.

Ni watu ambao sio rahisi kudanganyika wakiona mpango wowote wa kifedha. Mara nyingi ni kawaida yao kuchukua kitu au kufanya mradi ambao wengine wanauona wa kipuuzi na wakaugeuza kuwa wa thamani kubwa.

Ni wakarimu sana wanapokuwa na fedha, na hawapendi kujidai kwa utajiri wao. Wako tayari wakati wowote kuwatumia watu wengine kutekeleza malengo yao.
Kwa ujumla wao ni wataalamu wa kutafuta fedha katika njia ambazo watu wengi hawazifahamu.

MAVAZI YA NG'E

Wenye nyota ya Nge wanatakiwa wavae nguo zenye rangi inayong’ara, zenye kuonekana na maridadi,zilizo katika hali ya suti au mbili kwa pamoja.

Nguo ziwe za rangi nyekundu au shati jekundu au skafu nyekundu. Kitambaa kiwe cha sufi au cha fulana au chenye kumeremeta.

Mavazi yaendane na kofia na wanawake wapendelee sana kuvaa suruali.


MATATIZO YA KIAFYA

Nyota hii inatawala kifuko cha mkojo, uume, uke, kifandugu au kitonoko (coccy), mlango wa kizazi(cervix) na sehemu ya haja kubwa. Vile vile inatawala mfumo wa mkojo na tezi kibofu (prostate).

Matatizo yao makubwa ya kiafya yanatokana na sehemu zilizotajwa ambazo zinatawaliwa na nyota yao wenye nyota hii wanapenda kujizoesha sana mambo ya mapenzi na ngono. Wakati mwingine hisia zao zinakuwa kubwa sana kiasi kwamba wao wenyewe wanajishuku vibaya.

Inapotokea hivi wanahitajika kusafisha miili yao kwa fadhaa iliyowajaa kutokana na mfadhaiko wa hisia zao.

Kwa ujumla ni watu wenye afya nzuri na wanapona haraka maradhi yanayowasumbua. Wenye nyota hii wana tabia ya aidha kula, kunywa au kuvuta kupita kiasi au wengine hawafanyi mambo hayo kabisa.

Kwa vile nyota hii inatawala sehemu zinazoondoa uchafu wa mwili ni vizuri watu wa Nge wakawa waangalifu na mambo yanayochafua mwili wao.

Magonjwa makubwa ya wenye nyota ya Nge ni maradhi yanayohusiana na kibofu cha mkojo, maradhi ya kuziba mkojo, kansa ya tezi kibofu (prostate Cancer), matatizo ya damu ya kike na mabusha.


KAZI ZA WENYE NYOTA YA NG'E.

Nyota ya Nge ambayo alama yake ya asili ni Maji ni nyota mojawapo ya nyota zenye nguvu katika mambo ya kikazi.

Ni watu wenye milipuko ya hisia wanapokuwa katika miradi yao ya kazi. Wanafanya shughuli zao kwa hisia kali na hamaki na wanategemea wapate majibu ya kuridhisha.

Ni watu makini sana katika kazi na wanafanya kazi kwa kutilia mkazo na ushupavu wakihakikisha wanatekeleza malengo yao. Ni watu waerevu na wenye kung’amua mambo upesi. Ni wafanyakazi wazuri na wanaheshima kwa wafanyakazi wenzao.

Kazi zinazowafaa wenye nyota hii ni kazi za madawa au tiba, kazi za upelelezi, kazi za utafiti, kazi za fundi bomba, kazi za elimu ya kale, na kazi za ushauri wa mambo ya mapenzi na ngono.


FAMILIA ZA NG'E

Wazazi wenye nyota ya Nge ni watu ambao wanaonyesha utulivu wa hali ya juu. Kimaumbile huwa hawaonyeshi hisia walizokuwa nazo juu ya watoto wao, wanaweza wakawa na chuki kubwa lakini hawapendi kuiionyesha.

Kwa ujumla wazazi hao wanapenda watoto na wanatumia muda mwingi na hisia zao kuwangalia na kuwadhibiti watoto wao.

Pamoja na ukarimu wao ni wazazi wenye kupenda nidhamu na wanataka watoto wao wafuate maadili mema. Wazazi hao walivyokuwa wadogo wamepitia ujanja wote hivyo hawakubali watoto wao wawadanganye.

Watoto watagundua kwamba wazazi wao ni watu wa kutisha na kuogopwa lakini uhusiano wao unakuwa ni mzuri. Wazazi wa kike wanakuwa na hisia kali kwa watoto wao kitendo ambacho kinawafanya watoto wawe katika shinikizo.


MADINI YA NG'E

Wenye nyota hii wanatakiwa wavae vito vinavyoitwa BERYL NA RED CORNELIUS. Mawe haya yenye rangi ya damu ya mzee (Maroon) na rangi Nyekundu yanaakisi au kuashiria asili ya Nge ya uhusiano wake wa asili na kitu chochote cha miujiza na uchawi.


UHUSIANO WA KIMAPENZI

(NG'E, NG’OMBE)


Tabia ya Nge ya wasiwasi, wivu, hisia kali za kimapenzi na dhana mbaya kwa wapenzi wao hutulizwa na kuzimwa na nyota ya Ng’ombe ambao wana tabia ya utulivu, uaminifu, wasioyumba na wanaopenda kusikiliza wanayoambiwa.


VYAKULA VYA NG'E

Wenye nyota hii wanashauriwa wale vyakula au matunda yafuatayo ambayo yanatawaliwa na nyota yao, Mananasi, wapende sana vitunguu vibichi na vilivyopikwa, Nyama ya Kondoo mchanga na vyakula viambatane na viungo vikali.


NCHI ZA NG'E
Ili kupata mafanikio ya kinyota kwa wale wenye uwezo wanashauriwa aidha kuishi au kutembelea nchi au miji ifuatayo ambayo inatawaliwa na nyota hii.
Miji hiyo ni Liverpool(Uingereza) na New Orleans(Marekani) na nchi za Poland na Switzerland.

RANGI YA NGE
Wenye nyota hii wanashauriwa wapake nyumba zao au vyumba vyao au magari yao au sehemu zao za biashara rangi nzito yenye kutia shauku na kuvutia kama rangi ya damu ya mzee (Maroon).


Mwenye tarehe 1 december NYOTA YA MSHALE (SAGITTARIUS)


Hii ni nyota ya tisa katika mlolongo wa nyota 12.

Wenye nyota hii ni wale waliozaliwa kati ya tarehe 22 November na 21 December ya mwaka wowote.

Sayari yao ni Jupiter (Mushtary).

Siku yao ya Bahati ni Alhamisi.

Namba yao ya Bahati ni 3.

Rangi yao ya Bahati ni Hudhurungi.

Asili yao ni MOTO.

KIPAJI CHA MSHALE (Prophetic)


Wenye nyota hii wana kipaji cha kutabiri na kujua mambo ambayo yatatokea mbele au muda utakaokuja, na mara nyingi wanalolisema huwa linatokea hata likiwa la kipuuzi.


TABIA ZA MSHALE

Wenye nyota ya mshale ni wenye tabia ya kuwa na matumaini ya mafanikio kwa lolote wanalolitegemea. Wanapenda kuwa na uhuru wa kupenda na kuchagua na wanapenda watu wengine wawe kama wao.

Hawapendi mambo nusunusu na ni watu ambao wako wazi na wanaopenda kusoma. Ni wakweli na ukitaka kuelewana nao na wewe uwe mkweli.

Ni watulivu na ni waaminifu na wanapenda uadilifu. Ni watu ambao hawapendi kuamrishwa kufanya jambo kwa sababu wanaamini kwamba wao wenyewe wana uwezo mkubwa wa kutekeleza jambo lolote, lakini likiwaudhi wanakuwa wakaidi na wasioweza kutii amri.

Wenye nyota hii hawaoni taabu kusema lolote bila kujali athari zake mradi jambo hilo liwe la kweli.


TABIA YA MSHALE KATIKA MAPENZI

Pamoja na kwamba wenye nyota hii wanapenda wawe huru na wenye kujiamulia mambo yao wenyewe huwa wana starehe na kuona raha wanapokuwa ndani ya uhusiano wa kimapenzi.

Wenye nyota hii wanapenda sana kujihusisha na makundi makundi lakini huwa wanapata muda wa kuwa na wapenzi wao. Ni watu wachangamfu na wenye kupenda lakini tabia yao ya kutojali inawafanya wapenzi wao wajione kwamba wanakosa ulinzi wa kimapenzi.

Wanapoingia katika mapenzi wanakuwa waaminifu. Mwanzoni wanakuwa wagumu sana kujihusisha. Wanapenda sana wakati wote kuwa na wapenzi wapya au mapenzi ya kawaida kwa sababu wanaamini mapenzi ya kudumu yanawanyima uhuru.

Wapenzi wao wanaponyesha dalili ya kuwapenda basi wao huwa wanajiondoa kwa hofu ya kubanwa na kutokuwa na uhuru.

Ni watu wanaopenda kufanya ngono kwa muda mrefu na hisia zao ziko mbali na inashauriwa kwamba wapenzi wao wawe wamekula kabla ya tendo la ndoa vinginevyo itakuwa taabu.


TABIA YA MSHALE KATIKA FEDHA

Alama ya nyota hii ni Mshale na mategemeo yao ya kifedha yanalenga mbali na juu sana.

Wenye nyota hii fedha kwao ndio njia pekee ya kujikomboa na kupata uhuru hivyo wako tayari kufanya jambo lolote hata kama ni la hatari ili wapate fedha na wanapozipata huzitumia bila mpangilio.

Mara nyingi huwa hawapendi kutafuta fedha zao katika njia za kawaida wanapenda sana kutumia njia tofauti na kubuni mbinu mbali mbali kutekeleza malengo yao.

Ni watu ambao hawaoni haya kumtumia mtu mwenye pesa au uwezo ili watekeleze malengo yao. Kwa sababu hii wengi wao wanakuwa matapeli.

Matatizo yao makubwa ni kwamba wao ni watumiaji wabaya na hawana mipango thabiti ya matumizi ya fedha na ni watu ambao wakitoa ahadi ya fedha hawatekelezi.


MAVAZI YA MSHALE

Wenye nyota ya Mshale wanatakiwa wavae nguo zenye kuathiri na za mzaha mzaha kama koti au blauzi isiyo rasmi au nguo za kitamaduni zilizoongezwa ongezwa vitu vingi kama maua au nakshi nakshi.

Rangi ya nguo zao iwe ya Zambarau au rangi ya Hudhurungi iliyochangamka au rangi ya blue.

Vitambaa viwe vya sufu. Nguo ziambatane na mikanda, na viatu viwe vya buti.Wanawake wapendelee kuvaa sketi.


MATATIZO YA KIAFYA:

Nyota hii inatawala sehemu ya chini ya kiuno. Wenye nyota hii hawapendi kuugua. Lakini huwa wanapata maradhi kutokana na kujishughulisha kupita kiasi na kutumia nguvu zao na akili zao kwa muda mrefu bila mapumziko. Wanathamini sana mizunguko kuliko mapumziko.

Vile vile ni watu wasiopenda ushauri kuhusiana na afya zao.

Tatizo lao lingine ni kuwa wanapenda sana kula na kunywa na hiyo huwaletea unene usiotakiwa. Wakitaka kujikomboa na matatizo wanashauriwa wawe na tabia ya kujipumzisha.

Magonjwa yanayohusiana na nyota hii ni majereha na maradhi ya nyonga, mapaja, maradhi ya ini (Liver Disorder) kupooza kwa miguu (paralysis of limbs) na ugonjwa wa kuumwa mishipa au misuli ya nyuma ya paja.



KAZI YA MSHALE

Kupata au kukosa, kushinda au kupoteza, kuna uchangamfu wa asili kwa nyota hii na uzoefu katika hali yeyote.

Ni watu waaminifu wanaopenda sana mafankio na wako tayari wakati wowote katika kazi. Kutokana na hili wanakuwa na bahati ya kuwa katika sehemu muafaka na katika muda unaotakiwa.

Wenye nyota ya Mshale ni wafanyakazi waaminifu na hawapendi kuwasimamia watu katika kazi. Ni wenye kuwaamini wafanyakazi wao na wanapokuwa ofisini huleta mazingira ya urafiki na kuaminiana.

Kazi zinazowafaa ni za usafiri, kazi za sheria, Wakili au Hakimu, kazi za uandishi, ualimu, dini, sheikh au padri au makanisani au misikitini, michezo, kazi za kijeshi na uuzaji.



FAMILIA ZA MSHALE
Wazazi wenye nyota ya Mshale ni wenye kuwachangamsha sana watoto wao. Nyumba zao zinakuwa zinajaa vitabu na vifaa mbali mbali na wanawahimiza sana watoto wao wawe huru na majasiri.
Wenye nyota hii wanapenda kuwatembeza watoto wao katika sehemu za elimu, kama vile, Makumbusho au sehemu za kihistoria.
Elimu na masomo hupewa kipaumbele na mzazi mwenye nyota ya mshale ambaye mara nyingi huhakikisha mtoto wake anasoma. Wazazi hawa wanapata matatizo makubwa kuwadhibiti watoto wasiosikia kwa sababu wao wenyewe wanapenda uhuru kwa sababu hii huwa wanavumilia tabia mbaya za watoto wao hata watoto wakiwa wajeuri.

MADINI YA MSHALE
Wenye nyota hii wanatakiwa wavae vito vinavyoitwa SAPPHIRE. Mawe haya nyenye rangi ya bluu yana uwezo mkubwa wa kinyota wa kumletea mvaaji afya nzuri, nguvu na kinga vitu ambavyo wenye nyota hii wanavihitaji.


UHUSIANO WA KIMAPENZI
(Mshale na Mapacha)

Tabia ya kufanya mambo haraka haraka au kukata tamaa na kupenda kuelewa mambo ya wenye nyota ya Mapacha inaingiliana vizuri na wenye nyota ya Mshale ambao ni wenye busara na subira na wasiokata tamaa.

VYAKULA VYA MSHALE

Wenye nyota hii wanashauriwa wale vyakula au matunda yafuatayo ambayo yanatawaliwa na nyota yao. Nyama mwitu, kunazi za rangi ya bluu, maboga na juice ya mapera.

NCHI ZA MSHALE
Ili kupata mafanikio ya kinyota kwa wale wenye uwezo wanashauriwa aidha kuishi au kutembelea nchi au miji ifuatayo ambayo inatawaliwa na nyota zao.
Nchi hizo ni USA na SPAIN na miji ni Budapest (Romania) na Cologne (Ujerumani).

RANGI ZA NYOTA
Wenye nyota hii wanatakiwa wapake nyumba zao au vyumba vyao au sehemu zao za biashara rangi zenye kusisimua na uchangamfu na zinazoashiria hali ya kumkaribisha mgeni.
Rangi hizo ni Nyekundu iliyochangamka (Warm Red) rangi ya Zambarau (Purple) na rangi ya hudhurungi au kahawia (Brown).




MWENYE Tarehe 28 December ni NYOTA YA MBUZI (CAPRICON)

Hii ni nyota ya kumi katika mlolongo wa nyota 12.
Wenye nyota hii ni wale waliozaliwa kati ya tarehe 22 Dec na 19 Jan ya mwaka wowote.
Sayari yao ni SATURN (ZOHAL)
Siku yao ya bahati ni Jumamosi.
Namba yao ya bahati ni 8.
Rangi yao ya bahati ni rangi ya Kijivu au Nyeusi.
Asili yao ni Udongo.

KIPAJI CHA MBUZI(GRADUAL)
Wenye nyota hii wana kipaji cha kuchambua mambo kidogo kidogo au kufuatilia kitu bila watu kujua na kupata ufumbuzi wa uhakika mwishoni.

TABIA ZA MBUZI
Wale wote waliozaliwa katika nyota hii ni watu ambao wanapenda kuwajibika, ni wenye bidii ya kazi, katika kazi yeyote watakayofanya hata kama ikiwa ni ya kipuuzi.
Ni viumbe waaminifu sana na ni watu wastahamilivu na wenye kuweza kuvumilia matatizo yeyote.
Kwa upande mwingine ni watu wenye tamaa kubwa ya kimaisha na kimaendeleo, na kwa sababu ya kutekeleza malengo yao basi huwa wanakuwa wabinafsi na wenye uroho na uchu.

TABIA YA MBUZI KATIKA MAPENZI
Watu wenye nyota hii wanakuwa ni watu wenye aibu sana kwa wapenzi wao lakini aibu ikishawaondoka huwa ni wapenzi wa kutisha, kwa maana ya kwamba kwa vile wao ni waaminifu wanataka wapenzi wao wawaunge mkono katika hisia zao za kimapenzi.
Ni watu wanaoogopa sana kuachwa na wapenzi wao hivyo basi huwa wanakuwa waangalifu sana katika kuchagua wapenzi.
Jambo jingine ni kuwa huwa wao wenyewe hawajiamini kimapenzi, mara nyingi wanashindwa kuingia katika mapenzi kwa woga tu hivyo kukosa nafasi nzuri ya kupendwa.
Kwa ujumla ni wapenzi makini na huwa hawaoi mpaka wapate uhakika wa kutosha kutoka kwa wapenzi wao. Ni wapenzi makini, waaminifu na wanaoweza kuaminiwa. Lengo lao katika mapenzi ni usalama.

TABIA YA MBUZI KATIKA FEDHA
Kwa watu wenye nyota hii fedha ni kitu muhimu sana katika maisha.
Watu wa Mbuzi wanaamini kabisa kwamba fedha ndio zitawapa uwezo wa kuweza kupambana au kukabiliana na mazingira ya Dunia, hivyo basi suala lolote la fedha na mali wanalichukulia kwa uzito mkubwa sana.
Inawachukua muda mrefu kutekeleza malengo yao ya kifedha lakini wakishazipata basi huwa hawatetereki tena. Wana uwezo wa kuhifadhi walichonacho.
Ni watu wabahili sana na hata kama wakiwa na fedha nyingi utaona wanaishi maisha ya kawaida na wala huwezi kuwajua.
Fedha zao zinatoka kwa sababu maalum ya dharura na wala siyo katika starehe au vinginevyo na hiyo ni kwa sababu hupenda kukumbuka walikotoka katika hali ya umasikini au ufukara.


MAVAZI YA MBUZI
Wenye nyota ya Mbuzi wanatakiwa wavae nguo za mitindo, zilizoshonwa kwa ustadi.
Nguo hizo ziwe za rangi ya kijivu au Kijani iliyoiva au hudhurungi nzito.
Kitambaa kiwe cha kitani (Linen) au cha ngozi.
Nguo ziwe ni suti na ziambatane na saa za mikononi.

MATATIZO YA KIAFYA
Nyota hii inatawala Mifupa, Magoti na Ngozi.
Matatizo yao makubwa ya kiafya huwa yanasababishwa na muda mrefu ambao wanafanya kazi au kujishughulisha.
Hii ni kwa sababu hawamwamini mtu mwingine afanye shughuli zao ambazo zina mipangilio ya muda mrefu, nguvu nyingi, na akili hutumika.
Shughuli zao nyingi za mizunguko na kufikiria huwaletea maradhi kama Baridi Yabisi (rheumatism).
Maradhi yao mengine makubwa ni ugonjwa wa ngozi, matatizo ya Magoti na maradhi ya mifupa.

KAZI ZA MBUZI
Wenye nyota ya Mbuzi kitu muhimu katika maisha yao ni kazi na maisha mazuri na yanayoeleweka ambayo yako katika mpangilio wanaoutaka wao.
Ni watu ambao wanazingatia sana muda wa maisha na wana mpangilio maalum kwamba katika umri fulani awe amepata nini au awe na fedha kiasi gani.
Ni wenye kupenda utekelezaji wa kazi wa hali ya juu na wao wanapoagizwa hufanya hivyo.
Kazi zao zinazowafaa ni zile za kutumia akili, Uhandisi, Usanifu Majengo, Saveya, kazi za Serikali, Siasa na Daktari wa Meno.

FAMILIA ZA MBUZI
Wazazi wenye nyota ya Mbuzi ni watu ambao wamepangilia kabisa mipango ya watoto wao kabla hawajazaa.
Ni wazazi ambao wanayachukulia kwa uzito mkubwa majukumu yao ya kulea na hawakubali kabisa watoto wao kufanya michezo michezo ya kipuuzi. Wanapenda kuwahimiza watoto wao kuwa na malengo ya maana.
Wanapenda sana nidhamu katika familia zao.
Mara nyingi wazazi wa kiume huwa hawapati muda kuwa na watoto wao kutokana na kazi nyingi walizonazo lakini kwa wazazi wa kike wanakuwa wanatumia akili ya hali ya juu katika kutatua matatizo au hisia za watoto wao.

MADINI YA MBUZI
Wenye nyota hii wanatakiwa wavae vito vinayoitwa Black Jet.
Jiwe hili inaaminiwa lina uwezo wa kuongeza ujasiri na kumletea mvaaji mafanikio ya kibishara.


UHUSIANO WA KIMAPENZI (MBUZI NA KAA)
Tabia ya Mbuzi ya ubahili na kutopenda anasa hulainishwa na tabia ya Kaa ya upendo, mapenzi na huruma.

VYAKULA VYA MBUZI
Wenye nyota ya Mbuzi wanashauriwa wapende kula vyakula au matunda yafuatayo. Ambayo ndio yanatawaliwa na nyota yao.
Wapende sana vyakula vya Nazi na Nyama yeyote.
Vile vile wapendelee kula Viazi Vitamu na Samaki Gamba (Shellfish).

NCHI ZA MBUZI
Ili kupata mafanikio ya kinyota kwa watu wenye uwezo wanashauriwa aidha waishi au watembelee miji au nchi zifuatazo ambayo inatawaliwa na nyota ya Mbuzi.
Miji hiyo ni Brussels (Ubelgiji) na Oxford (Uingereza) au nchi za Mexico na India.

RANGI ZA MBUZI

Wenye nyota hii wanashauriwa wapake rangi zifuatazo kwenye nyumba zao, rangi ya Kahawia (Brown) Rangi ya Kijivu (Grey) au Nyeusi.


USHAURI WANGU:
Una nyota nzuri lakini kila ukifanya jambo huwa haliwi? Unajiuliza kwa
nini kila nikifanya mambo yangu yanaharibika?Jibu haulipati Jibu lake ni utakuwa umerogwa au nyota yako imechukuliwa na wachawi au mtu mwengine anaitumia ukitaka mambo yako yawe mazuri kupandishwa nyota yako iwe juu iwe ina ng'ara na kufanikiwa kwa mambo yako na kupata pete ya nyota yako pete ya bahati na kinga unaweza kunitafuta kwa njia hizi hapa chini.Unaweza kunitafuta kwa Mawasiliano Herbalist Dr. MziziMkavu Email barua ya pepe.fewgoodman@hotmail.com What's App +905344508169 Au Ni add Kwa Facebook tumia jina hili mzizimkavu. Au boonyeza hapa.Mzizi Mkavu
 
Unapotumia nguvu za mashetani au uwezo ambao una ushaidi tosha kuwa si wa Mungu mwenyezi, hapo unafanya uchawi.
Uchawi unatia ndani Kuroga, Pepo, Kuwasiliana na Roho Waovu, na Ibada ya Shetani.

Mungu alikataza uchawi, soma (Mambo ya Walawi 19:26) “Asionekane kwako mtu . . . atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri, wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo.”

Na ukisoma zaidi katika Kumbukumbu la Torati 18:10-11. Utapata elewa zaidi uchawi ni nini.

Kwa kuongezea, Matendo ya Mitume 19:19 "Kwa kweli, idadi kubwa ya wale waliozoea kufanya uchawi wakakusanya vitabu vyao pamoja na kuviteketeza mbele ya kila mtu. Nao wakafanya hesabu na kupata vitabu hivyo vilikuwa na thamani ya vipande 50,000 vya fedha."
Usikalili vifungu vichache bila kuelewa hiyo elimu ya nyota ipo tokea zamani na ndiyo maana hata alipozaliwa yesu Kristo watu wa kwanza walikuwa ni wamajusi na walitambua hivyo kupitia nyota iliyowaongoza had kwenye zizi la ng'ombe alipozaliwa yesu Kristo. Kasome mathayo mtakatifu 2:1-2 nanukuu vifungu hivyo " yesu alipozaliwa katika berthlehemu ya uyahudi zamani za mfalme herode , tazama mamajusi wa mashariki walifika Yerusalemu wakisema , yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa wayahudi , kwa maana tuliiona nyota Yake mashariki nasi tumekuja kumsujudia" mwisho wa kunukuu. Kwahiyo hapo tunajifunza kuwa kupitia nyota Yake yesu kristo iliwawezeshe hao wa mamajusi kujua amezaliwa mfalme kwa sababu nyota Yake ilikuwa tofauti na zingine.

Sasa kama ni uchawi kama baadhi yenu mnavyosema unazan kwanin mungu alitoa uwezo huo kwa watu kujifunza hiyo Elimu .
 
mm desember 14 nyota yangu plz

Mwenye tarehe 14 december NYOTA YA MSHALE (SAGITTARIUS)


Hii ni nyota ya tisa katika mlolongo wa nyota 12.

Wenye nyota hii ni wale waliozaliwa kati ya tarehe 22 November na 21 December ya mwaka wowote.

Sayari yao ni Jupiter (Mushtary).

Siku yao ya Bahati ni Alhamisi.

Namba yao ya Bahati ni 3.

Rangi yao ya Bahati ni Hudhurungi.

Asili yao ni MOTO.

KIPAJI CHA MSHALE (Prophetic)


Wenye nyota hii wana kipaji cha kutabiri na kujua mambo ambayo yatatokea mbele au muda utakaokuja, na mara nyingi wanalolisema huwa linatokea hata likiwa la kipuuzi.


TABIA ZA MSHALE

Wenye nyota ya mshale ni wenye tabia ya kuwa na matumaini ya mafanikio kwa lolote wanalolitegemea. Wanapenda kuwa na uhuru wa kupenda na kuchagua na wanapenda watu wengine wawe kama wao.

Hawapendi mambo nusunusu na ni watu ambao wako wazi na wanaopenda kusoma. Ni wakweli na ukitaka kuelewana nao na wewe uwe mkweli.

Ni watulivu na ni waaminifu na wanapenda uadilifu. Ni watu ambao hawapendi kuamrishwa kufanya jambo kwa sababu wanaamini kwamba wao wenyewe wana uwezo mkubwa wa kutekeleza jambo lolote, lakini likiwaudhi wanakuwa wakaidi na wasioweza kutii amri.

Wenye nyota hii hawaoni taabu kusema lolote bila kujali athari zake mradi jambo hilo liwe la kweli.


TABIA YA MSHALE KATIKA MAPENZI

Pamoja na kwamba wenye nyota hii wanapenda wawe huru na wenye kujiamulia mambo yao wenyewe huwa wana starehe na kuona raha wanapokuwa ndani ya uhusiano wa kimapenzi.

Wenye nyota hii wanapenda sana kujihusisha na makundi makundi lakini huwa wanapata muda wa kuwa na wapenzi wao. Ni watu wachangamfu na wenye kupenda lakini tabia yao ya kutojali inawafanya wapenzi wao wajione kwamba wanakosa ulinzi wa kimapenzi.

Wanapoingia katika mapenzi wanakuwa waaminifu. Mwanzoni wanakuwa wagumu sana kujihusisha. Wanapenda sana wakati wote kuwa na wapenzi wapya au mapenzi ya kawaida kwa sababu wanaamini mapenzi ya kudumu yanawanyima uhuru.

Wapenzi wao wanaponyesha dalili ya kuwapenda basi wao huwa wanajiondoa kwa hofu ya kubanwa na kutokuwa na uhuru.

Ni watu wanaopenda kufanya ngono kwa muda mrefu na hisia zao ziko mbali na inashauriwa kwamba wapenzi wao wawe wamekula kabla ya tendo la ndoa vinginevyo itakuwa taabu.


TABIA YA MSHALE KATIKA FEDHA

Alama ya nyota hii ni Mshale na mategemeo yao ya kifedha yanalenga mbali na juu sana.

Wenye nyota hii fedha kwao ndio njia pekee ya kujikomboa na kupata uhuru hivyo wako tayari kufanya jambo lolote hata kama ni la hatari ili wapate fedha na wanapozipata huzitumia bila mpangilio.

Mara nyingi huwa hawapendi kutafuta fedha zao katika njia za kawaida wanapenda sana kutumia njia tofauti na kubuni mbinu mbali mbali kutekeleza malengo yao.

Ni watu ambao hawaoni haya kumtumia mtu mwenye pesa au uwezo ili watekeleze malengo yao. Kwa sababu hii wengi wao wanakuwa matapeli.

Matatizo yao makubwa ni kwamba wao ni watumiaji wabaya na hawana mipango thabiti ya matumizi ya fedha na ni watu ambao wakitoa ahadi ya fedha hawatekelezi.


MAVAZI YA MSHALE

Wenye nyota ya Mshale wanatakiwa wavae nguo zenye kuathiri na za mzaha mzaha kama koti au blauzi isiyo rasmi au nguo za kitamaduni zilizoongezwa ongezwa vitu vingi kama maua au nakshi nakshi.

Rangi ya nguo zao iwe ya Zambarau au rangi ya Hudhurungi iliyochangamka au rangi ya blue.

Vitambaa viwe vya sufu. Nguo ziambatane na mikanda, na viatu viwe vya buti.Wanawake wapendelee kuvaa sketi.


MATATIZO YA KIAFYA:

Nyota hii inatawala sehemu ya chini ya kiuno. Wenye nyota hii hawapendi kuugua. Lakini huwa wanapata maradhi kutokana na kujishughulisha kupita kiasi na kutumia nguvu zao na akili zao kwa muda mrefu bila mapumziko. Wanathamini sana mizunguko kuliko mapumziko.

Vile vile ni watu wasiopenda ushauri kuhusiana na afya zao.

Tatizo lao lingine ni kuwa wanapenda sana kula na kunywa na hiyo huwaletea unene usiotakiwa. Wakitaka kujikomboa na matatizo wanashauriwa wawe na tabia ya kujipumzisha.

Magonjwa yanayohusiana na nyota hii ni majereha na maradhi ya nyonga, mapaja, maradhi ya ini (Liver Disorder) kupooza kwa miguu (paralysis of limbs) na ugonjwa wa kuumwa mishipa au misuli ya nyuma ya paja.



KAZI YA MSHALE

Kupata au kukosa, kushinda au kupoteza, kuna uchangamfu wa asili kwa nyota hii na uzoefu katika hali yeyote.

Ni watu waaminifu wanaopenda sana mafankio na wako tayari wakati wowote katika kazi. Kutokana na hili wanakuwa na bahati ya kuwa katika sehemu muafaka na katika muda unaotakiwa.

Wenye nyota ya Mshale ni wafanyakazi waaminifu na hawapendi kuwasimamia watu katika kazi. Ni wenye kuwaamini wafanyakazi wao na wanapokuwa ofisini huleta mazingira ya urafiki na kuaminiana.

Kazi zinazowafaa ni za usafiri, kazi za sheria, Wakili au Hakimu, kazi za uandishi, ualimu, dini, sheikh au padri au makanisani au misikitini, michezo, kazi za kijeshi na uuzaji.



FAMILIA ZA MSHALE
Wazazi wenye nyota ya Mshale ni wenye kuwachangamsha sana watoto wao. Nyumba zao zinakuwa zinajaa vitabu na vifaa mbali mbali na wanawahimiza sana watoto wao wawe huru na majasiri.
Wenye nyota hii wanapenda kuwatembeza watoto wao katika sehemu za elimu, kama vile, Makumbusho au sehemu za kihistoria.
Elimu na masomo hupewa kipaumbele na mzazi mwenye nyota ya mshale ambaye mara nyingi huhakikisha mtoto wake anasoma. Wazazi hawa wanapata matatizo makubwa kuwadhibiti watoto wasiosikia kwa sababu wao wenyewe wanapenda uhuru kwa sababu hii huwa wanavumilia tabia mbaya za watoto wao hata watoto wakiwa wajeuri.

MADINI YA MSHALE
Wenye nyota hii wanatakiwa wavae vito vinavyoitwa SAPPHIRE. Mawe haya nyenye rangi ya bluu yana uwezo mkubwa wa kinyota wa kumletea mvaaji afya nzuri, nguvu na kinga vitu ambavyo wenye nyota hii wanavihitaji.


UHUSIANO WA KIMAPENZI
(Mshale na Mapacha)

Tabia ya kufanya mambo haraka haraka au kukata tamaa na kupenda kuelewa mambo ya wenye nyota ya Mapacha inaingiliana vizuri na wenye nyota ya Mshale ambao ni wenye busara na subira na wasiokata tamaa.

VYAKULA VYA MSHALE

Wenye nyota hii wanashauriwa wale vyakula au matunda yafuatayo ambayo yanatawaliwa na nyota yao. Nyama mwitu, kunazi za rangi ya bluu, maboga na juice ya mapera.

NCHI ZA MSHALE
Ili kupata mafanikio ya kinyota kwa wale wenye uwezo wanashauriwa aidha kuishi au kutembelea nchi au miji ifuatayo ambayo inatawaliwa na nyota zao.
Nchi hizo ni USA na SPAIN na miji ni Budapest (Romania) na Cologne (Ujerumani).

RANGI ZA NYOTA
Wenye nyota hii wanatakiwa wapake nyumba zao au vyumba vyao au sehemu zao za biashara rangi zenye kusisimua na uchangamfu na zinazoashiria hali ya kumkaribisha mgeni.
Rangi hizo ni Nyekundu iliyochangamka (Warm Red) rangi ya Zambarau (Purple) na rangi ya hudhurungi au kahawia (Brown).


USHAURI WANGU:
Una nyota nzuri lakini kila ukifanya jambo huwa haliwi? Unajiuliza kwa
nini kila nikifanya mambo yangu yanaharibika?Jibu haulipati Jibu lake ni utakuwa umerogwa au nyota yako imechukuliwa na wachawi au mtu mwengine anaitumia ukitaka mambo yako yawe mazuri kupandishwa nyota yako iwe juu iwe ina ng'ara na kufanikiwa kwa mambo yako na kupata pete ya nyota yako pete ya bahati na kinga unaweza kunitafuta kwa njia hizi hapa chini.Unaweza kunitafuta kwa Mawasiliano Herbalist Dr. MziziMkavu Email barua ya pepe.fewgoodman@hotmail.com What's App +905344508169 Au Ni add Kwa Facebook tumia jina hili mzizimkavu. Au boonyeza hapa.Mzizi Mkavu
 
Usikalili vifungu vichache bila kuelewa hiyo elimu ya nyota ipo tokea zamani na ndiyo maana hata alipozaliwa yesu Kristo watu wa kwanza walikuwa ni wamajusi na walitambua hivyo kupitia nyota iliyowaongoza had kwenye zizi la ng'ombe alipozaliwa yesu Kristo. Kasome mathayo mtakatifu 2:1-2 nanukuu vifungu hivyo " yesu alipozaliwa katika berthlehemu ya uyahudi zamani za mfalme herode , tazama mamajusi wa mashariki walifika Yerusalemu wakisema , yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa wayahudi , kwa maana tuliiona nyota Yake mashariki nasi tumekuja kumsujudia" mwisho wa kunukuu. Kwahiyo hapo tunajifunza kuwa kupitia nyota Yake yesu kristo iliwawezeshe hao wa mamajusi kujua amezaliwa mfalme kwa sababu nyota Yake ilikuwa tofauti na zingine.

Sasa kama ni uchawi kama baadhi yenu mnavyosema unazan kwanin mungu alitoa uwezo huo kwa watu kujifunza hiyo Elimu .
Mkuu usiumize kichwa kushindana na watu ambao hawana elimu hivyo hapa wanajifunza wanajuwa Mtandao wa Jamii Forums ni chuo kikuu. Kwa hiyo watakuumiza kichwa chako wanayosema ni maneno ya pumba waache na ujinga wao wa kutokuwa na elimu ya kutosha Elimu ya Nyota ni Sayansi kubwa sana ukiijuwa unaweza kutabiri kila kitu katika hii dunia elimu ya nyota ni elimu kubwa sana sio ya kuifanyia mchezo.
 
.sasa nyota mbona haihusiani Na uchawi au hauna elimu kuhusu nyotaa ?? Au hujui kuhusu mamajusi walifata nin kumwona yesu ??
Siyo swala la kutokuwa na elimu! Biblia imeongelea majusi au manajimu, yaliongozwa na nyota (shetani) ili watakapo muona Yesu waweze toa taarifa kwa mfalme Herodi.

Soma Mathayo 2:1,2,11,16. Lengo la kuongozwa Mamajusi na nyota lilikuwa ni kuleta mauwaji ya watoto wa miaka 2 nchi nzima. Tambua kwamba Mamajusi yalimtembelea Herod kwanza kabla Mtoto Yesu, ili kumpa taarifa kuzaliwa kwake. Ndipo Herod akatangaza watoto chini ya miaka miwili wauwawe!

Nyota isiyo ya kawaida iliwavutia “mamajusi” kutoka Mashariki, na mwishowe iliwaongoza kwa mtoto mchanga Yesu, kama inavyoelezwa katika Biblia, Mathayo. (Mathayo 2:1-12)

Kwahiyo, hiyo nyota haikuwa ishara kutoka kwa Mungu, bali Shetani mwenye lengo la kutaka mtoto Yesu auwawe. Wakristo wa kweli hawajiusishi na unajimu (astrology) sababu umekatazwa ndani ya biblia katika Kumbukumbu 18:10-12 na Isaya 47:13-15.
 

Nyota ya 10 nı nyota ya Mbuzi: Desemba 22 – Januari 19


alama-za-nyota_mbuzi

Ni alama ya udongo na mwenye kuhitaji nyumba yenye amani ili kuhisi ukamilifu.

Mwenye malengo , mipango na matarajio makubwa

Ni mtatuaji wa matatizo kwa vitendo na mapangiliaji mzuri wa mambo-Mtendaji

Ni mwenye mipango na mfuatiliaji wa mipango yake

Si mshirikishaji mzuri mpaka aombwe au asukumwe.

Ni mpenzi mzuri na rafiki wa maisha

Mgumu kubadilika

Mbishi na asiyekubari kushindwa kirahisi

Mfanyabiashara

Mwajibikaji

UHUSIANO WA KIMAPENZI (NYOTA YA MBUZI NA NYOTA YA KAA)
Tabia ya Mbuzi ya ubahili na kutopenda anasa hulainishwa na tabia ya Kaa ya upendo, mapenzi na huruma.
nimezaliwa 29-Decemba naona umepatia kwa asilimia 70% hapo mkuu
 
nimezaliwa 29-Decemba naona umepatia kwa asilimia 70% hapo mkuu
Kazi kwako kuamini au kuto amini mimi hiyo sio kazi yangu. Mimi ninaamini kuwa nyota zinasema ukweli kwa Asilimia 1000%1000 sasa wewe ukiamini au usipo ziamini mimi hiyo sio kazi yangu.
 
Na tarehe 14 July inakuaje hapo mkuu

NYOTA YA KAA (CANCER)
Hii ni nyota ya nne katika mlolongo wa nyota 12.
Wenye nyota hii ni wale waliozaliwa kati ya tarehe 21 Juni na tarehe 20 July ya mwaka wowote.
Sayari yao ni mwezi (moon).
Siku yao ya bahati ni Jumatatu.
Namba yao ya bahati ni 2 na 7.
Rangi yao ya bahati ni Nyeupe.
Asili ya nyota yao ni Maji.

KIPAJI CHA KAA (SENSITIVE):
Wenye nyota hii wana kipaji cha hisia ya kugundua mambo yanayotendeka ikiwa ni pamoja na kubashiri mambo, kumwelewa mtu kwa undani na kujua jambo ambalo mtu anataka kulifanya au jambo litakalotendeka hasa kwenye watu wengi.

TABIA ZA KAA
Watu wenye Nyota hii ni wenye tabia ya hisia nzito ni wapole na wenye huruma. Wakiwa na dhamira ya ulezi na kuwaangalia watu wengine na hiyo inaonekana waziwazi katika nyumba zao na familia zao.
Hata hivyo upande mwingine ni watu ambao wana gubu na wakali ne wenye kupenda kujishughulisha na wanajiamini.
ni watu ambao wanaweza kubadilika lakini wenye msimamo na itikadi na wanaweza kuwa ni wenye wivu mkali na wenye kudhibiti.

TABIA YA KAA KATIKA MAPENZI :
Hisia ni kitu muhimu sana katika mapenzi kwa wenye nyota hii pamoja na kwamba kimaumbile ni watu wanapenda kujilinda na wanaogopa sana kuumizwa kimapenzi na wapenzi wao.
Wanapenda sana kuwa karibu na wanayempenda na kuwaonyesha huba na upendo mkubwa. Kwao hakuna mapenzi ya nusu nusu na wanapenda sana kuwa na mtu ambaye atadumu nae milele.
Wenye Nyota hii bila ya kuwa na mpenzi hujihisi hawajatimiza lengo lao katika maisha hivyo basi huwa hawana raha.
Ni wapenzi waaminifu na wanategemea wapenzi nao wawe waaminifu kama wao.
Ni wagumu sana kuachana na wapenzi na inapotokea huwa hawaagi wako radhi wao waumie kuliko kuachana na anayempenda.

MATATIZO YA KIAFYA:
Nyota hii inatawala njia kuu ya chakula kuelekea tumboni, mbavu, mfupa wa kidari, tumbo la uzazi, utumbo mdogo na utumbo au sehemu zote za kusagia chakula.
Vile vile inatawala bandana na matiti.
Tatizo lao kubwa la maradhi yao linatokana na ukimya wao wanapoudhiwa. Inapotokea hivyo wao hushindwa kusema na huumia kimya kimya.
Maradhi yao makubwa yanakuwa maradhi yanayosababishwa na gesi , au vidonda vya tumbo au kiungulia au maradhi yanayotokana na mwili kuwa mnene au umbo kubwa.

KAZI ZA WENYE NYOTA YA KAA:
Wenye nyota hii wanatakiwa wafanye kazi ambazo zitawafanya wao wawe walezi wa wale wanaowatumikia ili kukidhi mahitaji ya nyota yao.
Wanatakiwa wafanye kazi za utabibu kama vile Madaktari au Wauguzi, kazi za baharini kama vile mabaharia, kazi za huduma ya chakula kama hoteli, migahawa, kazi za kuhudumia watoto kama katika shule za chekechea, kazi za benki au kazi za maneja utumishi au kazi za kuandika.

FAMILIA ZA KAA:
Wenye nyota hii ni wazazi asilia, na wazazi wakiume mara nyingi huonekana wakiwasaidia wake zao kulea watoto.
Wanafanya kwa bidii kuhakikisha familia zao zinapata kila kitu kinachohitajika.
Mzazi wakike ana hisia kiuzazi kuliko mume na kwa mtoto kwa mtoto anyependa kuwa huru kuna muda hujihisi kwamba mama yake anambana.
Wazazi wa nyota hii wana tabia ya kuangalia mambo yaliopita nyuma hivyo hupenda mambo yasibadilike milele.
Hali ya Wazazi hao ya kubadilika badilika huwapa wakati mgumu watoto hasa wale wenye hisia ndogo ambao huhisi wanasukumwa sana na hutaka kujikomboa ili waondokane na baa hilo.
Wazazi wenye nyota hii hupenda sana watoto wao wafanye wanzozitaka wao kinyume na matakwa ya watoto wao .

MADINI YA KAA:
Wenye nyota hii wanatakiwa wavae madini ya moonstone au jiwe lolote lenye rangi ya maziwa.
madini haya yana uwezo wa kuongeza hisia na kufanya wawe na ari ya kuwatumikia na kuwakinga wenzao.

UHUSIANO WA KIMAPENZI:
Tabia ya Mbuzi ya ubahili na kutopenda anasa hulainishwa na tabia ya Kaa ya upendo, huba na huruma ambayo humfanya mbuzi atulie na atumie kile alichonacho .

VYAKULA VYA KAA:
Wenye nyota hii wanashauriwa wapende kula vyakula vifuatavyo ambavyo ndivyo vyakula vinavyotawaliwa na nyota yao.
Vyakula vyenyewe ni kama Mapeas, kaa au vyakula vya baharini, na mboga kama kabichi na saladi (lettuce).

NCHI ZA KAA:
Ili kupata mafanikio ya kinyota wenye nyota hii wanashauriwa watembelee au waishi katika miji au nchi zifuatazo ambazo zinatawaliwa na nyota yao.
Miji hiyo ni New York (Marekani) na Venice (Ugiriki) au nchi za New Zealand na Scotland.

RANGI ZA KAA:
Wenye nyota hii wanashauriwa kinyota wapake au watumie rangi zozote ambazo siyo nzito au zenye uwiano na rangi nyeupe.

USHAURI WANGU:
Una nyota nzuri lakini kila ukifanya jambo huwa haliwi? Unajiuliza kwa
nini kila nikifanya mambo yangu yanaharibika? Jibu lake ni utakuwa umerogwa au nyota yako imechukuliwa na wachawi au mtu mwengine anaitumia ukitaka mambo yako yawe mazuri kupandishwa nyota yako iwe juu iwe ina ng'ara na kufanikiwa kwa mambo yako na kupata pete ya nyota yako pete ya bahati na kinga unaweza kunitafuta kwa njia hizi hapa chini.Unaweza kunitafuta kwa Mawasiliano Herbalist Dr. MziziMkavu Email barua ya pepe.fewgoodman@hotmail.com What's App +905344508169 Au Ni add Kwa Facebook tumia jina hili mzizimkavu. Au boonyeza hapa.Mzizi Mkavu
 
Back
Top Bottom