Ukweli mchungu kuhusu KINANA

Ukweli mchungu kuhusu KINANA

Alistaafu jeshi mwaka 1972 akiwa ametumikia jeshi miaka 20 ! Cheo cha mwisho 'Kanali'. Kwa mantiki hiyo alipata ofisa kadeti (Luteni)1952 ! Hili lilikuwa jeshi gani ? .......KAR ? ...TPDF !? JWTZ !?

You have a point mkuu! tatizo watu wengine mapenzi yao binafsi kwa Kinana yanawafunika mpaka wapo tayari kutudanganya kama watoto wadogo ili mradi aonekane ni msafi.
 
acha ujinga kumfagilia JANGILI.. huwezi kusema huyu mtu ni makini wakati ameshindwa kutupa majibu ya kinagaubaga kuhusu ujangili wake, na matokeo yake amaekuwa mtu wa kuchenga kutoa majibu...
Hawezi kuepuka katika kashfa hii ya meli yake kukamatwa na PEMBE ZA NDOVU NCHINI KOREA...
JIBU NI KWAMBA WEWE PAMOJA NA KINANA NI WAHALIFU NA WAFUJA NYARA ZA SERIKALI....
ETI MELI NI YANGU LAKINI ALIYETUMA MZIGO HUO SIMFAHAMU???????????
DOES ITS MAKE SENSE?
HUWEZI FANYA INTERNATIONAL BUSINESS KAMA HIZI HALAFU USIJUE NI MTU WAAINA GANI UNAFANYA NAYE BIASHARA HII,
KINANA HAFAI.. ILA CCM WAENDELEE KUMKUMBATIA NA WAJUE FIKA WAO NDO MWISHO UMEWADIA WA KUSHIKA DOLA YA TANZANIA....
POLE SANA KIJANAA KWA MAWAZO YAKO FINYU KAMA VILE UPO KATIKA NDOTO...
 
Kei mkiendelea kumchekea maccm kufikia 2020 tembo wote kwisha habari yake atahamia kwa albino.
 
sikudhani kama kuna watu wana mawazo ya kizamani kwaninini msifikirie kumkwamua yule mkulima,mfanyakazi mwananchi wa kwaida wa mtaani kupunguza ugumu wa maisha yao wewe unafikiria kumweka mtu kupambana na wapinzani upuuziiii mkubwa jifunzeni china aheni upuuuzi huuuu tumieni akili zenu kutatua matatizo
 
Ni mtu asiyejali au mpuuzi asiyezijua vyema siasa za Tanzania anayeweza akasimama na KUUPONGEZA AU KUUAHABIKIA uteuzi WA KIJINGA NA KIPUUZI uliofanywa na Rais Kikwete ambaye baada ya kushindwa mara kadhaa hatimaye amefanikiwa kumshawishi, mmoja wa wanasiasa makini na wakongwe, mtumishi wa umma wa muda mrefu, mwanadiplomasia na Kanali Mstaafu wa Jeshi, Abdulrahaman Kinana kuwa Katibu Mkuu wa CCM.
 
Na wasifu wote huo Tembo wanaisha na sasa hasafirishi tena anasaga hapa hapa anasafirisha refined product

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
naloliga hurita unapaswa kuzingatia kwamba utendaji wa Kinana umekuwa ukiporomoka tangu alipokabidhiwa mikoba ya Mukama, ni kweli ana historia au rekodi nzuri ya kiutendaji lakini kulingana na mabadiliko ya kasi ya kisiasa na vuguvugu la mageuzi linalokolea kila kikicha rekodi yake imeanza kuingia dosari ambazo kiukweli hazirekebishiki.

Kama kweli wewe ni mchambuzi wa mambo sidhani kama ingekuwa ni busara kuacha kuzungumzia jinsi alivyojikuta kwenye mitego ya kisiasa inayomfanya ajikute akitoa majibu ya hovyo badala ya kuendelea kutetea rekodi yake kwa kupangua hoja kwa hoja, kule Morogoro vijijini aliulizwa na mwanakijiji mmoja kuhusu tuhuma dhidi yake za pembe za ndovu.. alihamaki na kujibu mbele ya umati uliohudhuria kuwa "umetumwa wewe".. sasa mchambuzi unaweza kupata picha anaelekea wapi.. kwakifupi kuna nguvu inayotawala siasa za mageuzi tz inayofanya wana ccm wachanganyikiwe.

Pia akiwa mjini Morogoro akihutubia wananchi alijikuta kwenye mtego wa kuzungumzia cdm muda wote wa hotuba kana kwamba cdm ndio chama tawala na yeye na ccm ni wapinzani.. huko ni kukosa mwelekeo na kuchanganywa na siasa za kisasa ambako naamini hakumpeleki kwema kama katibu mkuu, bali ni kuzidi kukiangamiza chama hiki kikongwe.
 
Ni mtu asiyejali au mpuuzi asiyezijua vyema siasa za Tanzania anayeweza akasimama na kuudharau uteuzi uliofanywa na Rais Kikwete ambaye baada ya kushindwa mara kadhaa hatimaye amefanikiwa kumshawishi, mmoja wa wanasiasa makini na wakongwe, mtumishi wa umma wa muda mrefu, mwanadiplomasia na Kanali Mstaafu wa Jeshi, Abdulrahaman Kinana kuwa Katibu Mkuu wa CCM.

Kwa muktadha huo na kwa kuzingatia nafasi kuu ya utendaji aliyopewa, nitazungumzia kwa sehemu tu wasifu wa Kinana, mtu ambaye naamini anapaswa kuangaliwa kwa jicho la karibu na wakati mwingine kudhibitiwa ili kasi yake ya kukijenga chama alichopewa dhamana ya kukinusuru isije ikasababisha kuyumba kama si mauti ya kisiasa kwa baadhi ya vyama vya upinzani.

Ni wazi kwamba, kuteuliwa kwa Kinana kuwa Mtendaji Mkuu wa CCM Taifa, akirithi mikoba iliyomshinda, Wilson Mukama, kumetutia ganzi baadhi yetu ambao kwa muda mrefu tumekuwa ‘mashabiki’ au waumini wa kuchagiza kwa njia ya kalamu na wakati mwingine katika mijadala ya wazi kwamba, taifa lilikuwa na haja ya kutafuta mabadiliko ya uongozi kutoka nje ya chama tawala.

Sitaki kuwa miongoni mwa wapenda mabadiliko ambao kwa njia za kujifariji au za kujipa matumaini hewa wameingia katika mkumbo wa jumla jumla wa kumbeza Kinana kwa namna wanayotaka kuuaminisha umma wa Watanzania kwamba, mtu huyo anaweza akasukumwa kirahisi kwa namna ile ile ilivyopata kuwa kwa watangulizi wake kadhaa waliopata kushika wadhifa huo.

siku zote nilikuwa nikiamini kwamba, ukatibu mkuu kwa Kinana ilikuwa ni silaha moja ya maangamizi kwa vyama vya upinzani ambavyo naamini vinapaswa kuendelea kupewa fursa ya kuaminiwa na kukomaa.

Kinana anaendelea kubakia kuwa tishio kubwa kwa ustawi wa upinzani ambao ni rutuba muhimu kwa maendeleo ya demokrasia na misingi ya utawala bora.

Hili ndilo ambalo naamini wapinzani wanapaswa kulitazama na kulitafakari nyakati hizi wanapoendesha harakati zao za kukabiliana na maguvu ya dola na haya mapya ya hoja ambazo aghalab zitaongozwa na Kinana nyakati hizi taifa linapojiandaa kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa miaka mitatu ijayo.

Haitoshi kwa kina Freeman Mbowe, Profesa Ibrahim Lipumba, James Mbatia, Dk. Willibrod Slaa na Zitto Kabwe kumbeza Kinana na timu ya watendaji wake eti kwa hoja nyepesi na zisizo na mashiko za ufisadi au uchafu wa jumla jumla wa CCM.

Wapinzani na wachambuzi wa mambo wanapaswa kujua na kutambua kwamba, Kinana ni mwanasiasa wa vitendo, msomaji mzuri wa vitabu, ripoti, taarifa, magazeti, msikilizaji na msikivu mzuri wa mambo mepesi na mazito kuliko alivyokuwa ‘utopia’ Mukama anayeamini na kuzitetea nadharia zisizotekelezeka.

Si hilo tu, wapinzani wanapaswa kutambua kwamba, historia yake ya uaskari alioutumikia miaka 20 hadi mwaka 1972 akifikia cheo halisi cha jeshi cha Kanali ikimhusisha na mafunzo mahususi ya kimkakati ni sehemu ya mambo ambayo yanatawala nidhamu ya kazi ya aina ya kipekee iliyomfanya Kinana akawa jemedari wa mapambano ya CCM tangu mwaka 1995 hadi leo.

Wachambuzi wa mambo, nikiwamo mimi mwenyewe ambao siku zote tumekuwa tukiiona CCM kuwa chama kinachokufa kwa maana ya kuchungulia kaburi, tunapaswa kuanza kutafakari upya mawazo yetu hayo, nyakati hizi Kinana alipopewa dhamana ya kuwa mtendaji wake mkuu.

Tutakuwa wendawazimu iwapo tutamlinganisha Kinana na Mukama na kusahau kwamba huyu aliye kilingeni leo ndiye aliyemuongoza Benjamin Mkapa katika mapambano makali ya kisiasa mwaka 1995, zama Augustine Mrema alipokuwa tishio la kwanza la kweli dhidi ya CCM katika Uchaguzi Mkuu.

Alikuwa ni Kinana aliyefanya kazi kubwa katika kipindi chote cha kampeni akiratibu na kuongoza kampeni zote za Mkapa zilizomjumuisha pia Mwalimu Nyerere katika mazingira ambayo wengi walikuwa wakiamini CCM ilikuwa katika mwelekeo wa anguko la kihistoria.

Kinana ambaye kabla ya mwaka 1995 alikuwa tayari amepata kuwa Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Waziri wa Ulinzi alitumia vyema mbinu za medani na zile za kidemokrasia na kidiplomasia kumjengea uhalali Mkapa ambaye wakati huo alikuwa mwanasiasa ambaye hakuwa akijulikana sana.

Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, siku chache tu baada ya kuingia Ikulu kwa mara ya kwanza mwaka 1995, kwa sababu ama ya ulevi wa madaraka au kwa kutingwa na kazi za kimamlaka, Mkapa alisahau kazi kubwa aliyofanyiwa na Kinana.

Ni katika kipindi hicho cha kati ya mwaka 1995 na 2000 ndipo nilipokutana kwa mara ya kwanza na mara kadhaa na Kinana nyumbani kwake Masaki, jijini Dar es Salaam ambako nilipata fursa ya kumsikiliza na kuufahamu upeo mkubwa wa kuona mambo aliokuwa nao mwanasiasa huyo.

Tangu wakati huo hadi wakati wa kampeni za mwisho za mwaka 2010, niliendelea kukutana kwa nyakati fupi fupi na Kinana na mara kadhaa nikawa mtu wa kufuatilia na kuzisikiliza kwa makini, habari zake kutoka ama kwa marafiki au maadui zake wa kisiasa.

Sikushangazwa hata kidogo niliposikia tena kwamba, Mkapa alilazimika kumuangukia tena Kinana na kumuomba aongoze tena kampeni zake mwaka 2000 kabla ya Kikwete naye hajafanya kile alichofanya mtangulizi wake alipomuomba mwanasiasa huyo adhibiti joto la kiti cha urais mwaka 2010.

Uwezo wake mkubwa wa kisiasa, umakini wake na upeo mkubwa alionao katika kuona na kuchambua masuala ya siasa, uchumi na jamii ndivyo vitu ambavyo kwanza kwa nyakati tofauti vimepata kumfanya Kinana awe Mbunge wa Jimbo la Arusha kwa miaka 10, Mbunge wa Afrika Mashariki na Spika wa Bunge hilo.

Si ajabu hata kidogo kwamba, hata kabla ya kufikia huko, ni Kinana huyo huyo ambaye alipata kuwa Mwakilishi wa Kidiplomasia wa Rais wa Tanzania katika eneo la Maziwa Makuu na kabla ya hapo akiwa Mwenyekiti wa Mawaziri wa Ulinzi wa Nchi za Kusini Mwa Afrika (SADC) zama akiwa Waziri wa Ulinzi katika Serikali ya Awamu ya Pili iliyokuwa ikiongozwa Rais Ali Hassan Mwinyi.

Uzoefu wake katika siasa za kiraia unaanzia mwaka 1972 wakati alipostaafu jeshi akiwa Kanali baada ya kulitumikia kwa miaka 20 ndiyo ambao amekuwa akiutumia kama silaha kubwa ya kukijua chama chake na pengine kumfanya awe mmoja kati ya watu wachache ambao wamepata kuwafanyia kazi marais wote wane wa Tanzania.

Anarithi mikoba ya Mukama akiwa mmoja wa wanasiasa wachache wa CCM wa rika ile ile la kina Kikwete ambaye alilikimbia na kulikana kundi la mtandao mwaka 2005 ambalo baadhi yetu tunaamini kuwa, ndilo lilisababisha kuzaliwa kwa siasa mpya za kupakana matope, kuzushiana na kuhujumiana ndani na nje ya CCM.

Lakini pengine kubwa katika yote hayo anaingia madarakani huku akiwa na hazina ya uzoefu mkubwa wa kuongoza mapambano dhidi ya vyama vya upinzani na kushinda katika mazingira ambayo aghalab yamekuwa yakiacha vidonda visivyopona kwa wapinzani tangu mwaka 1995. Huyu si mtu wa kumpuuza au kumbeza hata kidogo.

kwahiyo kwa mawazo yako ushamsafisha
haya kachukue posho yako
ukitaka kumjua vizur waulize tembo
 
Umakini wa Kinana utawezaje kwa sasa hivi kubadilisha na kuboresha maisha ya Watanzania? Ni jinsi gani umakini huo utaweza kuondoa shutma dhahiri dhidi ya ccm na kuweza kugeuza mtazamo wa wananchi kwa ccm, tofauti na ilivyo sasa?
Meli imeshatoboka tunasubiri mshindo mkuu punde usemi utachafuka wacha watimie kwanza
 
Back
Top Bottom