Ukweli mchungu na sababu za kusimamishwa kwa Chama jr

Ukweli mchungu na sababu za kusimamishwa kwa Chama jr

Kama uyasemayo ni kweli basi Simba ishinde mechi zake bila Chama amani itakuwepo, ikitokea Simba ikafungwa au kutoa sare bila Chama kuwepo Kuna mambo matatu lazima yatokee.
1.Kocha kufukuzwa
2. Mangungu kupewa shinikizo lakuachia
madaraka.
3.Chama kurudishwa kundini haraka, ili kutuliza upepo, kitu ambacho Benchika hatakubali na kuondoka.
4.Suluhisho pekee ni Simba kushinda mechi zake bila Chama kuwepo uwanjani.
Naunga mkono hoja
 
Ni akili mgando hizo. Hakuna anayekataa kuwa Chama alituvusha hadi kufika makundi lakini sasa hana cha kuipa Simba tena. Ni aidha kiwango kimeshuka au amechoka kuwepo Simba na ameonyesha hivyo kwa vitendo tena hadharani kuwa ameichoka Simba. Hata wewe mkuu hata kama mkeo amekuzalia watoto lakini imefika wakati amekuchoka na amepata buzi utang'ang'ania kuwa naye? Kwa mwanaume mwenye busara utamuacha kwa taratibu zote stahiki vinginevyo ukilazimisha kuwa naye utakuja kumkuta na hilo buzi lake kitandani kwako. Chama alikuwa na faida kwa Simba lakini sasa hana faida yoyote ni busara aondoke na tunamtakia maisha mema huko alikoahidiwa malisho mema.
Kwa heshima aliyojijengea Chama angeondoka kwa heshima ila huu ujinga anaofanya atakua na mwisho mbaya
 
Mlipeni pesa zake hao viongozi ndio wanawadanganya kila kukicha mtu anadai pesa mnasema maswala ya nidhamu...hata usajiri wake ulisumbua kisa mlitaka kumkopa wakati yeye anazijua hizi Team zetu.. acheni janja janja mpeni pesa yake yote anayoidai Simba sio mnampa kesi moja baada ya ingine...
Siku hizi ubabaishaji wote wanaumaliza FIFA, watakapozuiwa kusajili ndio watamlipa pesa zake, hapa tunapigwa kwamba Tu, Chama anavyopendwa na mashabiki wa Simba ukiona anazinguwa ujuwe anadai pesa zake na si vinginevyo.
 
Kwa heshima aliyojijengea Chama angeondoka kwa heshima ila huu ujinga anaofanya atakua na mwisho mbaya
Wewe uko tayari kudhurumiwa stahili zako kazini?

Msiwachukulie powa hao wacheza Mpira, retirement yao ni miaka 40 tu huna shughuri na hapo uwe na kipaji, miaka 30 tu unaitwa Mzee, au siyo nyinyi kila siku mnataka John Boko aachwe? halafu akafanye kazi gani?
 
Wewe uko tayari kudhurumiwa stahili zako kazini?

Msiwachukulie powa hao wacheza Mpira, retirement yao ni miaka 40 tu huna shughuri na hapo uwe na kipaji, miaka 30 tu unaitwa Mzee, au siyo nyinyi kila siku mnataka John Boko aachwe? halafu akafanye kazi gani?
Amedhulumiwa na nani Chama kasha kua mswahili yale yale ya kina Feisal , mchezaji gani kila msimu lazima azue kitu
 
Mambo sio mambo
 

Attachments

  • 469A843E-76AF-4AFE-A522-8CE24EF45A6D.jpeg
    469A843E-76AF-4AFE-A522-8CE24EF45A6D.jpeg
    216.4 KB · Views: 2
Back
Top Bottom