Mambo mengi muda mrefu wa kuishi kwa mateso ukikosea step hapa Tanzania.
Mkuu motivational speaker ni watu wazuri sana usipo waelewa.
Mimi niliingiaa kwenye mtego baada ya kumotivetiwa na watu kama hao😀😀😀😀
Maliasili niliwajuaaa😀😀😀
Bwana wee nikaona mambo ya Masanja kulima Mpunga..nikaenda...
Mvuaaa ilaaniwe,,,,mpunga umekuwa unawaka waka..Bwana wee kumbe mwaka juzi mwaka jana lile vua lile lenyewe,Mto ukahamia kwangu na kwa majirani😀😀😀
Nimeona Bwawa shambani badala ya mpunga.
Sikuchoka mwaka huu nikarudi tena..wewe hii juu yenye inawaka achana nayo.😀😀😀
Naelewa kwanini watu wanalima Bangi kule Milimani Morogoro.
Tusikate tamaa tupige kazi ,ila si kwa kuwa motivated na wahuni wahuni.
Mambo ni magumu ukija kwenye battlefield..ukilegeza tu huna viungo.