Ukweli Mchungu: Utitiri wa TOZO, PAYE kubwa n.k, wa kulaumiwa ni sisi Watanzania wenyewe

Ukweli Mchungu: Utitiri wa TOZO, PAYE kubwa n.k, wa kulaumiwa ni sisi Watanzania wenyewe

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Sasa hivi mitandaoni ni kilio cha tozo na hii ni kwasababu tozo imetugusa wote na si kundi moja katika jamii, otherwise kilio kingekuwa si kikubwa kiasi hiki na huu ndio ujinga mkubwa wa sisi watanzania.

Kwanini nasema hivi?

Wakati wa Mwendazake, watumishi ambao walikuwa ni wafaidika wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu, waliongezewa makato karibu mara mbili na walipolalamika, baadhi ya watanzania wenzao waliwabeza na kuwaambia walipe hizo hela ili na wengine wasome na maneno mengine mengi ya kejeli.

Si hivyo tu, watumishi wa umma walipokaa miaka sita bila kuongezewa mishahara, wako watanzania waliwakejeli na kuwaambia kama hawaridhiki na mishahara yao waache kazi.

Halikadhalika, watumishi wanapolalamika kuwa PAYE ni kubwa mno, wako watanzania wanaowaona kama walalamishi na kuwaambia wanapaswa kulipa kodi ya serikali.

Mbali na yote hayo, mwezi uliopita watumishi walipolalamikiwa kuongezewa shilingi 12.000, 20,000 n.k, kuna watanzania waliwabeza na kuwaambia kama nyongeza hiyo wanaiona ni ndogo, basi waache kazi na maneno mengine ya aina hiyo.

Funny enough, baadhi ya watanzania waliowataka watumishi wa umma waacha kazi kama wanaona mshahara ni mdogo, ndio hao hao leo hii wanamlaumu Mwigulu kwa kuwataka watanzania wanaolalamikia tozo wahamie Burundi.

Wamasai huko Ngorongoro wanaohamishwa na kupelekwa Tanga wanapolalamikia, kuna watanzania wanawabeza na kuwataka wasipinge uamuzi halali wa serikali lakini ndio hao hao leo hii wanapinga uamuzi wa serikali kuongeza tozo kwenye miamala ya mabenki, n.k.

Mifano ya aina hii iko mingi sana ila yote inadhihirisha jambo moja kubwa kuwa watanzania ni watu wasioweza kuungana kupinga uonevu wa serikali dhidi ya kundi fulani katika jamii au hata pale ukandamizaji huo utapogusa watanzania wote kama ilivyo kwenye hili swala la tozo linalotugusa watanzania karibu wote.

Sasa watanzania tujiulize, kama hatuwezi kuungana kupinga kwa nguvu uonevu au ukandamizaji unaofanywa na serikali dhidi yetu, watawala wana hofu gani ya kuendelea kutukandamiza?

Jibu rahisi ni kwamba, wakulamiwa kwa haya yanayoendelea hapa nchini si watawala tena, bali ni sisi watanzania wenyewe kwa kukosa umoja katika kupinga mambo tunayoamini sio ya haki yanayofanywa na watawala, hivyo tuendelee kuvuna tulichopanda pasipo kulalamika kwani mtu huvuna kile alichopanda na kamwe si vinginevyo.

Kama vipi, Mwigulu njoo na tozo ya kulalamika ili tukae kimya kabisa.
 
16609969152263.jpg
 
Sasa hivi mitandaoni ni kilio cha tozo na hii ni kwasababu tozo imetugusa wote na si kundi moja katika jamii otherwise kilio kingekuwa si kikubwa kiasi hiki na huu ndio ujinga mkubwa wa sisi watanzania.

Kwanini nasema hivi?

Wakati wa Mwendazake, watumishi ambao walikuwa ni wafaidika wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu, waliongezewa makato karibu mara mbili na walipolalamika, baadhi ya watanzania wenzao waliwabeza na kuwaambia walipe hizo hela ili na wengine wasome na maneno mengine mengi ya kejeli.

Si hivyo tu, watumishi wa umma walipokaa miaka sita bila kuongezewa mishahara, wako watanzania waliwakejeli na kuwaambia kama hawaridhiki na mishahara yao waache kazi.

Halikadhalika, watumishi wanapolalamika kuwa PAYE ni kubwa mno, wako watanzania wanaowaona kama walalamishi na kuwaambia wanapaswa kulipa kodi ya serikali.

Mbali na yote hayo, mwezi uliopita watumishi walipolalamikiwa kuongezewa shilingi 12.000, 20,000 n.k, kuna watanzania waliwabeza na kuwaambia kama nyongeza hiyo wanaiona ni ndogo, basi waache kazi na maneno mengine ya aina hiyo.

Funny, enough, baadhi ya watanzania waliowataka watumishi wa umma waacha kazi kama wanaona mshahara ni mdogo, ndio hao hao leo hii wanamlaumu Mwigulu kwa kuwataka watanzania wanaolalamikia tozo wahamie Burundi.

Wamasai huko Ngorongoro wanaohamishwa na kupelekwa Tanga wanapolalamikia, kuna watanzania wanawabeza na kuwataka wasipinge uamuzi halali wa serikali lakini ndio hao hao leo hii wanapinga uamuzi wa serikali kuongeza tozo kwenye miamala ya mabenki, n.k.

Mifano ya aina hii iko mingi sana ila yote inadhihirisha jambo moja kubwa kuwa watanzania ni watu wasioweza kuungana kupinga uonevu wa serikali dhidi ya kundi fulani katika jamii au hata pale ukandamizaji huo utapogusa watanzania wote kama ilivyo kwenye hili swala la tozo linalotugusa watanzania karibu wote.

Sasa watanzania tujiulize, kama hatuwezi kuungana kupinga kwa nguvu uonevu au ukandamizaji unaofanywa na serikali dhidi yetu, watawala wana hofu gani ya kuendelea kutukandamiza?

Jibu rahisi ni kwamba, wakulamiwa kwa haya yanayoendelea hapa nchini si watawala tena, bali ni sisi watanzania wenyewe kwa kukosa umoja katika kupinga mambo tunayoamini sio ya haki yanayofanywa na watawala, hivyo tuendelee kuvuna tulichopanda pasipo kulalamika kwani mtu huvuna kile alichopanda na kamwe si vinginevyo.

Kama vipi, Mwigulu njoo na tozo ya kulalamika ili tukae kimya kabisa.
Nenda popote duniani, nchi huendeshwa kwa Kodi na tozo tu labda kasoro nchi za Kiarabu zenye Pato kubwa la mafuta kama Kuwait, Brunei, Qatar etc.

Kama una njia nyingine ya kupunguza Kodi huku ukikuza Pato la Serikali ziweke hapa.
 
Nenda popote duniani, nchi huendeshwa kwa Kodi na tozo tu labda kasoro nchi za Kiarabu zenye Pato kubwa la mafuta kama Kuwait, Brunei, Qatar etc.

Kama una njia nyingine ya kupunguza Kodi huku ukikuza Pato la Serikali ziweke hapa.
Umeongea la maana sana
 
Nenda popote duniani, nchi huendeshwa kwa Kodi na tozo tu labda kasoro nchi za Kiarabu zenye Pato kubwa la mafuta kama Kuwait, Brunei, Qatar etc.

Kama una njia nyingine ya kupunguza Kodi huku ukikuza Pato la Serikali ziweke hapa.
Umeongea bila kufikiri kwa Undani.
Kuwait, Brunei na Qatar wametumia rasilimali yao kuziba gape la tozo.
Je, Kwanini serikali hii ya CCM ishindwe kutumia rasilimali hizi kuziba pengo la tozo?
 
Nenda popote duniani, nchi huendeshwa kwa Kodi na tozo tu labda kasoro nchi za Kiarabu zenye Pato kubwa la mafuta kama Kuwait, Brunei, Qatar etc.

Kama una njia nyingine ya kupunguza Kodi huku ukikuza Pato la Serikali ziweke hapa.
Baada ya kuendesha nchi kwa tozo, vip hayo maendeleo kwa kila mmoja mmoja unayaona au unaongea tu
 
Nenda popote duniani, nchi huendeshwa kwa Kodi na tozo tu labda kasoro nchi za Kiarabu zenye Pato kubwa la mafuta kama Kuwait, Brunei, Qatar etc.

Kama una njia nyingine ya kupunguza Kodi huku ukikuza Pato la Serikali ziweke hapa.
Njia rahisi ni kupunguza marupurupu tunayowalipia viongozi wetu, mfano nyumba, simu, umeme, maji, chakula, nguo na posho zote ambazo mfanyakazi wa kawaida hapati wabaki na mshahara tu
 
Unataka Nani akujengee nchi yako, kwani huoni miradi mbalimbali inayotokana na tozo ikijengwa na mingine ilishakamilika na mingi itazinduliwa hapo baadaye, hufurahi kuona huduma za kijamii zikisogezwa karibu yako, hufurahi kuona unapunguziwa adha na kero ya kuzifuata mbali huduma, unataka Nani achange na alipishwe ili wewe uishi bure na kutumia bure

Tuendelee kumuunga mkono mh Rais wetu katika dhamira yake njema ya kuijenga nchi hii
 
Hili lina ukweli kabisa, na limewapa wepesi hawa watawala kufanya wanavyojisikia.
 
Umeongea bila kufikiri kwa Undani.
Kuwait, Brunei na Qatar wametumia rasilimali yao kuziba gape la tozo.
Je, Kwanini serikali hii ya CCM ishindwe kutumia rasilimali hizi kuziba pengo la tozo?
Usidhani kama sijafikiri kwa undani bali nipongeze kwanza kwa kuziibua nchi hizo.

Nchi hizo utawala wake ni wa Kisultan/Kifalme. Mali zitokanazo na mafuta ni mali za Wafalme hao na familia zao. Kwa hiyo huwekeza wanavyodhani ni sahihi kwa nchi zao. Wananchi hawana sauti ya kubadili chochote
 
Nenda popote duniani, nchi huendeshwa kwa Kodi na tozo tu labda kasoro nchi za Kiarabu zenye Pato kubwa la mafuta kama Kuwait, Brunei, Qatar etc.

Kama una njia nyingine ya kupunguza Kodi huku ukikuza Pato la Serikali ziweke hapa.

Watumie hizo raslimali wanazosema tunazo hadi mabeberu wanazitaka.
 
Baada ya kuendesha nchi kwa tozo, vip hayo maendeleo kwa kila mmoja mmoja unayaona au unaongea tu
Mafuta ya Qatar na Gesi ni mengi mno na raia ni wachache. So far Qatar ndiyo nchi tajiri kuliko zote kwenye ukanda wa ghuba. Brunei na Kuwait ni viinchi vidogo pia ila vina raslimali za mafuta.

Kupima maendeleo kwa vigezo vya per Capita Income utakuta kuwa nchi hizi ziko juu kuliko hata France na UK lakini kimtazamo wa maendeleo ya kijamii bado hazina maendeleo
 
Back
Top Bottom