Haiwezi kwenda dunia bila haramu kuwepo hata pig kitimoto mkuu wa meza anaitwa haramu na baadhi ya imani ila wanaokula hawapelekwi mahakamani hata siku moja
Haramu na iheshimiwe
Juzi nilikua kijiwe kimoja nimepoa na wadau, sasa kumbe mmoja wetu kwenye kijiwe hapo alikua na kiloba cha bangi mimi nilikua sijui maana ndio siku ya kwanza nmeenda kutulia niangalie wanavyocheza draft
Mara ghafla akaja kijana mmoja akaongea na yule jamaa mwenye kiloba, walichoongea mimi sikujua basi wakaelewana jamaa akaelekea kwenye kiloba akaanza kutoa bidhaa zimefungwa kwenye bahasha za kaki akampa
Jamaa akachukua ila hajakaa vizuri naona wametokea Jamaa wengine wawili wakiwa na pingu eeeh hatujakaa vizuri Jamaa katiwa pingu kawekwa chini kukaa sawa gari la polisi hili hapa
Wakamchukua mpaka central akawekwa huko wakaelewana na ilipofika jioni Jamaa akawa amerudi yupo kijiweni na kiloba chake cha bangi anauza pale pale km kawaida
Waliongea nini central wanakubariana nini mimi sijui ila itoshe kusema kwa kweli hakuna haramu ila wewe na Imani yako ndio inatafasiri ya hiki ni haramu na hiki sio haramu
Naweka karumu chini...