Ukweli ni upi juu ya wimbo wa Mandojo na Domokaya?

Ukweli ni upi juu ya wimbo wa Mandojo na Domokaya?

Zamani nilikuwa na mawazo kama yako, dingi anaishi maisha yake, akishakufa nanyi inakuwa zamu yenu kula bata kupitia urithi atakaouacha. Waacheni madingi wale bata.
Mzee wewe unaona ni sahihi kwa mzazi kushindwa kumhudumia mtoto kwa mahitaji basic kabisa kama shule kisa aachwe ale bata kwamba ndio muda wake?
Kama wewe ni baba inabidi uangalie vipaumbele vyako.
 
Mzee unaweza kushare kidogo, maana jamaa kazungumzia kwamba mshua alikuwa katibu mkuu wizara ya fedha, kazungumzia vile vile kuhusu kuvunjwa kwa baraza( ingawa hii naona si kweli, makatibu wakuu na wizara wapi wapi), na vipi kuhusu kupotezana na mshua wake.
Nafikri lengo la mwandishi alikua anataka upate general concept na sio specific concept
 
Domo Zaidi ya Kaya a.k.a MPIGA NDOLE.

a.k.a BABY.
Hadi Wewe unajua wapiga ndole? Bila shaka na wanyaushaji wa nyau camp unawafahamu pia...wazee wa usisahau nari na koti.
 
BC: Wapenzi wengi wa muziki, tukiwemo sisi hapa BongoCelebrity, tungependa sana kujua, je wimbo wenu ujulikanao kama Dingi ni kisa cha kweli au utunzi tu? Nani alitunga wimbo huu?
DOMOKAYA : Nyimbo hiyo ya “Dingi”
nimeitunga mimi mwenyewe hapa. Mimi kama Domo,lakini pia wakati natunga, nilikuwepo na mwenzangu
ManDojo. Ila kisa chenyewe kinanihusu mimi zaidi. Maisha yangu pamoja na nilivyoishi na baba yangu. Lakini kuna vitu venginie kidogo tumetunga kama vionjo vile ili verse itoshe na ili uweze kusikiliza. Lakini part kubwa ya lyrics ni true story. Yaani hata mama na kina mamdogo huko wanapousikia huu mwimbo
wanaona kabisa ‘huyu kamwimba baba yake huyu’ kama nilivyokwambia sisi tukitunga nyimbo tunajaribu kutunga kitu kile kile ambacho kinatokea katika maisha ya kila mtu, kama mimi yamenikuta yale yalionikuta mimi na baba yangu, kuna watu wengine yamewakuta mabaya zaidi na baba zao kuliko yalionikuta mimi ,unaona? Kwahiyo kila unapoandika na unapowakilisha wengi sana yanawagusa pia.
 
Hawa jamaa walikua balaa sana natamani wangekuwa na ubora ule kipindi hiki kazi yao ingewalipa wanachostagili
 
Hawa wasanii walifanya kazi kipindi hamna haya ma social netwek sioni kama kuna msanii wa sasa angetia miguu hapo walikuwa wanaandika sana sasa hivi mtu anaimba sijui weka mate niteleze mara anataka vya pooltable mwingine ana mandinga mapya daaaa

Kipindi hicho hamna cha wema na zari ili nyimbo yako ifanye poa sokoni
[emoji28] [emoji28] [emoji28] [emoji28]
 
Nina mshkaji wangu nilisoma nae primary, sasa baada ya kupoteana kwa muda siku moja nikamuibukia kwao. Kumuuliza kuhusu wazee wake akaniambia yupo na maza tu na wadogo zake lakini baba kasepa siku nyingi alivyoona maisha magumu.Siku hiyo mshkaji alilia sana yaani mzee kakimbia home bila hata ya kuaga hajulikani amekwenda kutafuta pande zipi na hajui kama atarudi.
Mpaka leo nikiisikiliza DINGI ya Mandojo na Domokaya basi namkumbuka mchizi
 
Back
Top Bottom