tpaul
JF-Expert Member
- Feb 3, 2008
- 24,225
- 22,632
Nimewaza sana kuhusu umuhimu wa ulevi wa pombe na sigara kwa walevi nikagundua kwamba ulevi huu hauna umuhimu wowote kwa wahusika, uwe wa kiafya au kiuchumi. Madhara ya pombe na sigara kwa mtumiaji yanajulikana kwa kila mtu mwenye akili timamu.
Pombe humfanya mnywaji ashindwe kufanya maamuzi sahihi na kumdhuru kiafya. Ina madhara kwa ini na viungo vingine muhimu. Hii ni sehemu tu ya madhara yatokanayo na unywaji pombe.
Sigara husababisha kansa ya mdomo, koo au mapafu.
Kila siku tunasikia serikali ikiwaita wawekezaji kujenga viwanda vya pombe kila mkoa katika nchi hii. Na uwekezaji kwenye pombe unalipa sana kwa sababu ya uwepo wa soko la uhakika (walevi) nchini.
Siku ya maadhimisho ya uvutaji sigara, utawaona serikali wanawaasa raia waache kuvuta sigara. Siku inayofuata utasikia wanapeleka tani kadhaa za mbolea kwa wakulima wa tumbaku huko Ruvuma na Tabora.
Ni kweli kwamba pombe na sigara huuingizia serikali fedha nyingi za kigeni. Lakini je, tutaendelea kudhuru afya za watanzania mpaka lini?
Tafakari!
Pombe humfanya mnywaji ashindwe kufanya maamuzi sahihi na kumdhuru kiafya. Ina madhara kwa ini na viungo vingine muhimu. Hii ni sehemu tu ya madhara yatokanayo na unywaji pombe.
Sigara husababisha kansa ya mdomo, koo au mapafu.
Kila siku tunasikia serikali ikiwaita wawekezaji kujenga viwanda vya pombe kila mkoa katika nchi hii. Na uwekezaji kwenye pombe unalipa sana kwa sababu ya uwepo wa soko la uhakika (walevi) nchini.
Siku ya maadhimisho ya uvutaji sigara, utawaona serikali wanawaasa raia waache kuvuta sigara. Siku inayofuata utasikia wanapeleka tani kadhaa za mbolea kwa wakulima wa tumbaku huko Ruvuma na Tabora.
Ni kweli kwamba pombe na sigara huuingizia serikali fedha nyingi za kigeni. Lakini je, tutaendelea kudhuru afya za watanzania mpaka lini?
Tafakari!