Hakikisha unanunua na kodi ya chumba kabisaUlikosea sana kurudi nyumbani.
Mimi bado nipo chuoni Mwaka wa mwisho ila ninaishi getto, nitanunua kila kitu kadri ya uwezo, ili nikimaliza chuo nisirudi home.
KujengaNatamani sana kujitegemea lakini nataka nikitoka Kwa wazazi niende kwangu kabisa kero za kupanga sitoweza.
Kati ya kujenga na kununua nyumba kipi nafuu Kwa wazoefu?
maana nataka nisepe home soon[emoji120]
Aiseee very interesting mkuu...Mimi miaka kadhaa iliyopita tulipishana na mzee wangu akanifukuza nikamwambia kama ni kuondoka nitaondoka na vitu vilivyopo chumbani kwangu, akasema wee thubutu wakati nanunua ulijua nilipataje hela, na mm nikakomaa kwamba nimelala kwenye chumba hicho miaka zaidi ya ishirini, nimevitunza I've earned them, hata mke akiachana na mwanaume wanagawana pasu hata kama alikuja na nguo tu mana alivitunza, mzee akadinda, nikatega siku wameenda kanisani nikachukua godoro la 5×6, kabati la nguo subwoofer ndogo pamoja na tv ya chumbani kwake, nilikua na kama laki tano ndo nimetoka kupiga dili nikaipata, nikaondoka nikaenda kupangisha nikiwa sina mishe yoyote nikalipa kodi ya miezi 3 nikanunua sufuria jiko la gesi na vyombovyombo nikaishi, nikawa sipokei simu mpaka mzee akaacha kupiga, mama hakuwahi kuacha kupiga nikawa napokea baada ya muda.
Nikapata kazi kwa wahindi flani maisha yakasonga kodi nalipa na maisha yanaendelea, kwa vile nazungumza na mama akawa ananipa feedback kwamba hapa home tunakumiss mana nilikua ndo nashughulika na usafi wa nje kuweka garden fensi maua maua yakae mkao, kazi zile zinazomhitaji mwanaume, sasa hakuna mtu na mze kazeeka, kwaiyo ananikumbuka sana hata alishanisamehe, nikapata mchumba ndio kwa mara ya kwanza tangu kuondoka nyumbani nikarudi kumtambulisha, nikachinja mbuzi ilikua shangwe sana.
Tangu hapo nikaoa nina watoto na kila jumapili lazima twende kwa wazee kushinda huko, watoto wangu wakifunga shule wanaenda huko wanaishi kabisa, mdogo ndio kahamia huko yani humtenganishi na babu yake. Mzee akanipa kiwanja kati ya vingi alivyokuwa navyo nikajenga nyumba simple tu room 3.
Ila nisingefukuzwa siku ile nisingekuwa hapa mana nilikua naogopa sana maisha ya kupangisha, hasa ukiimagine kila kitu unapata
Wakati mwingine jambo zuri linawezakutokea kwenye jambo baya
Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Unaambiwa una pata K's Sita halafu unaleta ujeuri... Maana yake
Kula bure
Kulala bure
Kunywa bure
Kutibiwa bure
K..u....n..y..a.. bure
Kufugwa bure
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwani ukomo wa kukaa kwa wazazi ni wapi?
Asante mkuu kwa ushauriNilianza kutafuta hela ghetto nikahamia,katika mishe nilikuwa natafuta kabla hela ya miezi 6 kwanza,nikipata ndo naanza sasa kutafuta hela ya mipango,miezi inavyozidi vitu vinazidi kuwa vingi,friji ,meza ,sofa ,tv ,kitanda,ikafika hamna mda nafasi ni finyi,nikahamia chumba moja self ,sebule na jiko.
Nimepambana kununua kiwanja now najenga Mungu akipenda mwezi wa 8 nahamia kwangu.
Wapambanaji msikae kwa wazazi ukisikia mishe nenda kabiliana na changamoto njia itatokea tu siku moja.
Sent using Jamii Forums mobile app
😂😂😂Utakuwa ni mhanga tu kwa vyovyote vile hata mwandiko wako unaonyesha kuwa umetafunwa kama nyama
Yaani ye ametafunwa kama nyama anaashum kila mtu hivyo hivyo. Mwambie apambane na hali yakeUtakuwa ni mhanga tu kwa vyovyote vile hata mwandiko wako unaonyesha kuwa umetafunwa kama nyama
Embu tuacheWadada wa jf inamana hamna mageto au nyie tayar mshajenga? [emoji2]
Sent from my SM-G9550 using Tapatalk
[emoji23][emoji23][emoji23] Nimecheka Sana hapo kwenye haki ya utunzaji vituMimi miaka kadhaa iliyopita tulipishana na mzee wangu akanifukuza nikamwambia kama ni kuondoka nitaondoka na vitu vilivyopo chumbani kwangu, akasema wee thubutu wakati nanunua ulijua nilipataje hela, na mm nikakomaa kwamba nimelala kwenye chumba hicho miaka zaidi ya ishirini, nimevitunza I've earned them, hata mke akiachana na mwanaume wanagawana pasu hata kama alikuja na nguo tu mana alivitunza, mzee akadinda, nikatega siku wameenda kanisani nikachukua godoro la 5×6, kabati la nguo subwoofer ndogo pamoja na tv ya chumbani kwake, nilikua na kama laki tano ndo nimetoka kupiga dili nikaipata, nikaondoka nikaenda kupangisha nikiwa sina mishe yoyote nikalipa kodi ya miezi 3 nikanunua sufuria jiko la gesi na vyombovyombo nikaishi, nikawa sipokei simu mpaka mzee akaacha kupiga, mama hakuwahi kuacha kupiga nikawa napokea baada ya muda.
Nikapata kazi kwa wahindi flani maisha yakasonga kodi nalipa na maisha yanaendelea, kwa vile nazungumza na mama akawa ananipa feedback kwamba hapa home tunakumiss mana nilikua ndo nashughulika na usafi wa nje kuweka garden fensi maua maua yakae mkao, kazi zile zinazomhitaji mwanaume, sasa hakuna mtu na mze kazeeka, kwaiyo ananikumbuka sana hata alishanisamehe, nikapata mchumba ndio kwa mara ya kwanza tangu kuondoka nyumbani nikarudi kumtambulisha, nikachinja mbuzi ilikua shangwe sana.
Tangu hapo nikaoa nina watoto na kila jumapili lazima twende kwa wazee kushinda huko, watoto wangu wakifunga shule wanaenda huko wanaishi kabisa, mdogo ndio kahamia huko yani humtenganishi na babu yake. Mzee akanipa kiwanja kati ya vingi alivyokuwa navyo nikajenga nyumba simple tu room 3.
Ila nisingefukuzwa siku ile nisingekuwa hapa mana nilikua naogopa sana maisha ya kupangisha, hasa ukiimagine kila kitu unapata
Wakati mwingine jambo zuri linawezakutokea kwenye jambo baya
Sent using Jamii Forums mobile app
Mbona umefuta picha