EMANUEL JOHN JOHN
JF-Expert Member
- Jul 31, 2018
- 502
- 461
Kaeni pamoja tu,kwenye room yako ya elfu40.Wakuu naombeni ushauri katika maisha Yangu.
Kwanza Hongereni sana na mapambano, ila katika maisha ya Ghetto jitahidi sana kuweka uvumilivu katika Muda.
Tukumbuke sisi ni Wapambanaji, hatutegemei msaada kutoka kwa mjomba au shangazi. Usitake mambo mengi kwa wakati mfupi...(power of delayed Gratification)
Kwa upande wangu Iko hivi.
Nina ishi na msichana ambae tupo kwenye uhusiano almost miezi 10 Sasa.
Kiukweli uyu manzi ananikubali sana, na Mimi pia namkubali kinyama. Hii ni kwasababu amenisaidia mambo mengi sana. Katika kutimiza ndoto zangu..(amenisaidia sana)
Sasa kwakuwa nakaaa nae bila ndoa, Kuna changamoto ya mwezi mtukufu wa ramadhani. Mana kijamii na kidini sio sahihi kukaa kiunyumba bila ndoa..
Sasa huyu dada akasema yeye atahama ila mwezi ukiisha itabidi nihamie hapo alipopata chumba mana mama mwenye nyumba hawaelewani(udhaifu wa wanawake))
Sasa Mimi naomba ushauri
Nikae nae au tukae tofauti ila tutakuja kufunga ndoa au tuanze kupambana kuanzia chini mpaka juu??
Je hustle za kupambana uku unaishi na msichana ambae utakuja kumuoa inaakaaje??
Naombeni ushauri wa kina mana nikimwambia tukae tofauti lazima aanze kulia..
Naomba ushauri!
Ninapokaa Kodi inaisha mwezi wa tano(40000) tutakapo Amia ambapo amelipa yeye Kodi ni (70000) amelipa miezi 4.
Naomba msaada