JamiiTalks
JF Advocacy Team
- Aug 7, 2018
- 685
- 1,124
Tanzania inatarajia kufanya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Novemba 2024, je, utashiriki katika Kupiga Kura?
Kama ndiyo/hapana kwanini?
JamiiForums inakukaribisha kushiriki katika Mjadala utakaohusu Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Novemba 2024, utakaofanyika kupitia XSpaces, leo Agosti 22, 2024 Saa 12:00 Jioni hadi Saa 2:00 Usiku ukiangazia kilichotokea kwenye Chaguzi za 2014 na 2019 na hali iliyopo sasa.
Kushiriki mjadala kupitia XSpaces ya JamiiForums bofya hapa
UPDATES:
JAFARI S. MNEKE, MKURUGENZI WA MAMBO YA NJE, SERA NA BUNGE - CUF
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ni Msingi wa Mamlaka, Utawala, Uwajibikaji na Maendeleo ya Nchi
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ni Msingi muhimu wa Demokrasia unaowezesha Wananchi kuchagua Mamlaka itakayowaongoza
Wote tunajua Mwaka 2019 tulipaswa kuwa na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa lakini sote tunajua kilichotokea
Ule haukuwa uchaguzi bali Uchafuzi wa Demokrasia
Novemba 27, 2024 tunatarajia kuingia kwenye Uchaguzi wa Serikali za MitaaNinapata Matumaini kuwa wa Mwaka huu utakuwa ni uchaguzi tofauti na Uliopita ambao siuiti Uchaguzi bali Uchafuzi wa Demokrasia
Kwanza tumeona dhamira njema ya Rais wa Awamu ya 6 kupitia 4R zake
Pia, kuna ushirikishwaji, Wadau wa Demokrasia wakiwemo Viongozi wa Vyama vya Siasa, walishiriki katika Vikao ambapo tulitoa mapendekezo ya kuboresha Uchaguzi
DEDAN CHACHA WANGWE
Vijana tunatamani sana tuwe miongoni mwa wale watakaoshiriki katika Uchaguzi hata kwa mara ya kwanza
Mnakumbuka CHADEMA tulitoa msimamo wa kutoshiriki katika Uchaguzi huu hadi pale Katiba Mpya itakapopatikana lakini Vijana tunaweka presha ili Chama kishiriki
Ni rahisi kuwaongoza watu wenye njaa lakini ni ngumu zaidi kuwaongoza watu wenye njaa kali
Kwa jinsi hali ilivyo ni kama tunapoteza matumaini na chaguzi hizi ambapo sitamani tufike hapo kama Vijana
GWAMAKA MBUGHI
Nchi yetu tunachangamoto kubwa, kwamba Uongozi wa Serikalini ni lazima utokee kwenye Vyama vya Siasa
Kwamba mtu hawezi kugombea nafasi za uongozi kama hatokani na Chama, lazima adhaminiwe na Chama cha SiasaSasa mtu kama ana sifa lakini hayupo kwenye Chama cha Siasa, mfumo unawatupilia nje
Katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa tunapambana na Chama kimoja ambacho kimejigeuza 'Refferee' wa Uchaguzi
Mazingira kama haya yanavunja Watu moyo kushiriki katika Chaguzi za Serikali za Mitaa
Ndio maana kuna watu bado wanapambana kwamba Uchaguzi wa Serikali za Mitaa usimamiwe na Tume Huru ya Uchaguzi badala ya TAMISEMI
Tusiposhiriki Uchaguzi hatuwezi kutambua udhaifu wa Mifumo iliyopo. Tunapaswa kushiriki uchaguzi pamoja na changamoto zilizopo ili tujue matatizo na changamoto za chaguzi zetu
Tunapaswa kuendelea kudai Mifumo na Sheria bora lakini wakati huo huo bado tunashiriki Uchaguzi
GERVAS MAIKO
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaohusisha Vyama vingi vya Siasa tunajua haujawahi kuwa wa Haki kwasababu ya nani anayeendesha Uchaguzi
Hapo tulipo, hata baada ya kutengeneza wanachokiita Tume Huru ya Uchaguzi bado tatizo lipo palepale kwasababu Uchaguzi unasimamiwa na Mkurugenzi na TAMISEMI, ambao wote wapo kwenye Mfumo wa Chama cha Mapinduzi
Kanuni za Uchaguzi zinazotungwa na Waziri zina mapungufu makubwa na zinazokusudia kukipa Ushindi Chama cha Mapinduzi
Mazingira haya hayajabadilika kwa nia ovu, kwa maana hiyo tunapoenda ni giza neneNakubaliana na walioenda Mahakamani kupinga
Wakati wa Uchaguzi ni wakati pekee unapeleka Elimu ya Uraia kwa Wananchi Ukisusa ni furaha kwa Chama cha Mapinduzi. Na Sheria ya Uchaguzi inasema kama kuna mgombea mmoja anapita bila kupingwa
Kwahiyo sio vizuri kususa. Tushiriki tuwaeleze Wananchi ili wakihujumu, Wananchi watajua ni kwasababu ya Mazingira mabovu ya Uchaguzi
Wanaopuuza Uchaguzi ni wasomi, saa nyingine hata hawapigi kura lakini wajue kuwa Kiongozi atakayechaguliwa bado ni Kiongozi waoNdio pale tunabaki na usiposhiriki kuchagua Kiongozi utaongozwa na Kiongozi mjinga
Tunalaani dola kuwatisha Watu kushiriki Uchaguzi. Matukio ya kamatakamata yameanza, hii sio nzuri Watu wapo tayari kushiriki Uchaguzi lakini changamoto ni mfumo wa Dola, wameanza kuwatisha
THE GENERAL (MDAU)
Ni ngumu sana kushiriki katika uchaguzi kama hakuna misingi mizuri ya Uchaguzi, pia hakuna umoja wa Vyama, mfano uchaguzi huu kama wangekuwa na nia ya mabadiliko ya kweli wangeweza kuungana na hiyo ingeleta matumaini
NTEGHENJWA HOSEAH (TAMISEMI)
Kuna tofauti kati ya Daftari la Kupiga Kura na Daftari linalotumika kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mtaa
Uboreshaji unaoendelea hivi sasa Mikoa tofauti unakupa sifa za kushiriki kwenye Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 lakini haukupi sifa za kupiga kura kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mtaa
Orodha ya Wapiga Kura kwaajili ya Serikali za Mtaa ni kuanzia Oktoba 2024, baada ya hapo ndio watakuwa wana sifa ya kupiga kura-Hivyo, inatakiwa Watu waelewe kuwa kuna madaftari mawili tofauti, kuna la Kupiga Kura katika Uchaguzi Mkuu na Uchaguzi wa Mtaa
Tumefanya mchakato shirikishi kuelekea katika mchakato huu wa Chaguzi, kulikuwa na Wadau mbalimbali zikiwemo Taasisi mbalimbali pamoja na Wananchi
Tumeshirikisha Mawazo na michango iliyotolewa na Wadau mbalimbali, hakuna haja ya kuwa na hofu, tumejipanga kuwa na Uchaguzi Huru na Haki, kama ambavyo tumeanza kwa Utulivu basi tumalize kwa Amani na Utulivu
JAFARI S. MNEKE, MKURUGENZI WA MAMBO YA NJE, SERA NA BUNGE: CUF
Ukilinganisha tulipotoka na tulipo, kuna dhamira njema inaoneshwa na Serikali iliyipo madarakani
Kama Rais wa sasa anakiri kuwa kulikuwa na changamoto huko nyuma na anaonesha dhamira njema, mimi ni nani nipinge?
Mimi sio mtu wa kuwaza ‘hasi’ napenda kuwa Mtu ninayefikiri ‘chanya’, kila zama zina kitabu chake, kila kiongozi ana zama zake
Demokrasia haizaliwi ikakua na kukomaa siku moja, lazima ipite katika mchakato, sitaki kuwa mtumwa wa Historia kuwa kilichotokea Mwaka 2019 basi kitatokea sasa hivi tena kisha nianze kukata tamaa
Nina imani kwa ushirikishwaji huu kupitia Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) na katika vikao mbalimbali tunapata matumaini kuwa tunapokwenda kuna nafuu, sisemi kuwa Chaguzi zitakuwa na haki kwa asilimia 100 lakini naamini kutakuwa na nafuu kubwa
Tumeshawaambia Serikali mapungufu yaliyopo katika mchakato wa kuelekea katika Chaguzi zijazo na wameahidi kutekeleza hilo baada ya muda mfupi
Demokrasia ina uwanja mpana, hivyo inapotokea kuna Watu wanaenda Mahakamani ndio Demokrasia yenyewe hiyo
Sisi CUF tunataka Siasa za hoja sio Siasa za chuki, nchi yetu inaamana kubwa kuliko maslahi ya Mtu mmoja mmoja, CUF ni wahanga wa Siasa za chuki, hatutaki kurudi huko tulipotoka
WAKILI WILLIAM MADUHU (LHRC)
Mwaka 1972, Mwalimu Nyerere alifuta Mamlaka za Serikali za Mtaa zote kwa maelezo kuwa hazikutimiza majukumu yao sawa sawa. Mwaka 1976 kukaibuka Kipindupindu ambapo baadhi ya Mamlaka zikarejeshwa
Mamlaka hizo zilirejeshwa Mwaka 1982, huko ndipo tulipotoka, lakini tulipo sasa Viongozi wengi wa Serikali za Mitaa hawana mishahara na hawana posho nyingine tofauti na ilivyo kwa Wabunge
Mbali na hapo Viongozi wa Serikali za Mitaa wamekuwa wakiingiliwa katika majukumu yao, mfano inaweza kutokea Mkuu wa Mkoa au Waziri anamuondoa kwenye nafasi yake Kiongozi wa Serikali za Mtaa, mamlaka ambayo hayapo kwake kwa kuwa Wananchi ndio waliomuweka madarakani
Kwa ufupi Serikali za Mitaa zinachukuliwa poa licha ya kuwa zina umuhimu mkubwa wa kuendesha Jamii na Wananchi kwa jumla, hili jambo sio sawa
Viongozi wa Mtaa hawana maslahi mazuri, hawana ofisi na wengine mazingira yao ya kufanya kazi sio mzuri
Kama ndiyo/hapana kwanini?
JamiiForums inakukaribisha kushiriki katika Mjadala utakaohusu Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa Novemba 2024, utakaofanyika kupitia XSpaces, leo Agosti 22, 2024 Saa 12:00 Jioni hadi Saa 2:00 Usiku ukiangazia kilichotokea kwenye Chaguzi za 2014 na 2019 na hali iliyopo sasa.
Kushiriki mjadala kupitia XSpaces ya JamiiForums bofya hapa
UPDATES:
JAFARI S. MNEKE, MKURUGENZI WA MAMBO YA NJE, SERA NA BUNGE - CUF
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ni Msingi wa Mamlaka, Utawala, Uwajibikaji na Maendeleo ya Nchi
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ni Msingi muhimu wa Demokrasia unaowezesha Wananchi kuchagua Mamlaka itakayowaongoza
Wote tunajua Mwaka 2019 tulipaswa kuwa na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa lakini sote tunajua kilichotokea
Ule haukuwa uchaguzi bali Uchafuzi wa Demokrasia
Novemba 27, 2024 tunatarajia kuingia kwenye Uchaguzi wa Serikali za MitaaNinapata Matumaini kuwa wa Mwaka huu utakuwa ni uchaguzi tofauti na Uliopita ambao siuiti Uchaguzi bali Uchafuzi wa Demokrasia
Kwanza tumeona dhamira njema ya Rais wa Awamu ya 6 kupitia 4R zake
Pia, kuna ushirikishwaji, Wadau wa Demokrasia wakiwemo Viongozi wa Vyama vya Siasa, walishiriki katika Vikao ambapo tulitoa mapendekezo ya kuboresha Uchaguzi
DEDAN CHACHA WANGWE
Vijana tunatamani sana tuwe miongoni mwa wale watakaoshiriki katika Uchaguzi hata kwa mara ya kwanza
Mnakumbuka CHADEMA tulitoa msimamo wa kutoshiriki katika Uchaguzi huu hadi pale Katiba Mpya itakapopatikana lakini Vijana tunaweka presha ili Chama kishiriki
Ni rahisi kuwaongoza watu wenye njaa lakini ni ngumu zaidi kuwaongoza watu wenye njaa kali
Kwa jinsi hali ilivyo ni kama tunapoteza matumaini na chaguzi hizi ambapo sitamani tufike hapo kama Vijana
GWAMAKA MBUGHI
Nchi yetu tunachangamoto kubwa, kwamba Uongozi wa Serikalini ni lazima utokee kwenye Vyama vya Siasa
Kwamba mtu hawezi kugombea nafasi za uongozi kama hatokani na Chama, lazima adhaminiwe na Chama cha SiasaSasa mtu kama ana sifa lakini hayupo kwenye Chama cha Siasa, mfumo unawatupilia nje
Katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa tunapambana na Chama kimoja ambacho kimejigeuza 'Refferee' wa Uchaguzi
Mazingira kama haya yanavunja Watu moyo kushiriki katika Chaguzi za Serikali za Mitaa
Ndio maana kuna watu bado wanapambana kwamba Uchaguzi wa Serikali za Mitaa usimamiwe na Tume Huru ya Uchaguzi badala ya TAMISEMI
Tusiposhiriki Uchaguzi hatuwezi kutambua udhaifu wa Mifumo iliyopo. Tunapaswa kushiriki uchaguzi pamoja na changamoto zilizopo ili tujue matatizo na changamoto za chaguzi zetu
Tunapaswa kuendelea kudai Mifumo na Sheria bora lakini wakati huo huo bado tunashiriki Uchaguzi
GERVAS MAIKO
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaohusisha Vyama vingi vya Siasa tunajua haujawahi kuwa wa Haki kwasababu ya nani anayeendesha Uchaguzi
Hapo tulipo, hata baada ya kutengeneza wanachokiita Tume Huru ya Uchaguzi bado tatizo lipo palepale kwasababu Uchaguzi unasimamiwa na Mkurugenzi na TAMISEMI, ambao wote wapo kwenye Mfumo wa Chama cha Mapinduzi
Kanuni za Uchaguzi zinazotungwa na Waziri zina mapungufu makubwa na zinazokusudia kukipa Ushindi Chama cha Mapinduzi
Mazingira haya hayajabadilika kwa nia ovu, kwa maana hiyo tunapoenda ni giza neneNakubaliana na walioenda Mahakamani kupinga
Wakati wa Uchaguzi ni wakati pekee unapeleka Elimu ya Uraia kwa Wananchi Ukisusa ni furaha kwa Chama cha Mapinduzi. Na Sheria ya Uchaguzi inasema kama kuna mgombea mmoja anapita bila kupingwa
Kwahiyo sio vizuri kususa. Tushiriki tuwaeleze Wananchi ili wakihujumu, Wananchi watajua ni kwasababu ya Mazingira mabovu ya Uchaguzi
Wanaopuuza Uchaguzi ni wasomi, saa nyingine hata hawapigi kura lakini wajue kuwa Kiongozi atakayechaguliwa bado ni Kiongozi waoNdio pale tunabaki na usiposhiriki kuchagua Kiongozi utaongozwa na Kiongozi mjinga
Tunalaani dola kuwatisha Watu kushiriki Uchaguzi. Matukio ya kamatakamata yameanza, hii sio nzuri Watu wapo tayari kushiriki Uchaguzi lakini changamoto ni mfumo wa Dola, wameanza kuwatisha
THE GENERAL (MDAU)
Ni ngumu sana kushiriki katika uchaguzi kama hakuna misingi mizuri ya Uchaguzi, pia hakuna umoja wa Vyama, mfano uchaguzi huu kama wangekuwa na nia ya mabadiliko ya kweli wangeweza kuungana na hiyo ingeleta matumaini
NTEGHENJWA HOSEAH (TAMISEMI)
Kuna tofauti kati ya Daftari la Kupiga Kura na Daftari linalotumika kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mtaa
Uboreshaji unaoendelea hivi sasa Mikoa tofauti unakupa sifa za kushiriki kwenye Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 lakini haukupi sifa za kupiga kura kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mtaa
Orodha ya Wapiga Kura kwaajili ya Serikali za Mtaa ni kuanzia Oktoba 2024, baada ya hapo ndio watakuwa wana sifa ya kupiga kura-Hivyo, inatakiwa Watu waelewe kuwa kuna madaftari mawili tofauti, kuna la Kupiga Kura katika Uchaguzi Mkuu na Uchaguzi wa Mtaa
Tumefanya mchakato shirikishi kuelekea katika mchakato huu wa Chaguzi, kulikuwa na Wadau mbalimbali zikiwemo Taasisi mbalimbali pamoja na Wananchi
Tumeshirikisha Mawazo na michango iliyotolewa na Wadau mbalimbali, hakuna haja ya kuwa na hofu, tumejipanga kuwa na Uchaguzi Huru na Haki, kama ambavyo tumeanza kwa Utulivu basi tumalize kwa Amani na Utulivu
JAFARI S. MNEKE, MKURUGENZI WA MAMBO YA NJE, SERA NA BUNGE: CUF
Ukilinganisha tulipotoka na tulipo, kuna dhamira njema inaoneshwa na Serikali iliyipo madarakani
Kama Rais wa sasa anakiri kuwa kulikuwa na changamoto huko nyuma na anaonesha dhamira njema, mimi ni nani nipinge?
Mimi sio mtu wa kuwaza ‘hasi’ napenda kuwa Mtu ninayefikiri ‘chanya’, kila zama zina kitabu chake, kila kiongozi ana zama zake
Demokrasia haizaliwi ikakua na kukomaa siku moja, lazima ipite katika mchakato, sitaki kuwa mtumwa wa Historia kuwa kilichotokea Mwaka 2019 basi kitatokea sasa hivi tena kisha nianze kukata tamaa
Nina imani kwa ushirikishwaji huu kupitia Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) na katika vikao mbalimbali tunapata matumaini kuwa tunapokwenda kuna nafuu, sisemi kuwa Chaguzi zitakuwa na haki kwa asilimia 100 lakini naamini kutakuwa na nafuu kubwa
Tumeshawaambia Serikali mapungufu yaliyopo katika mchakato wa kuelekea katika Chaguzi zijazo na wameahidi kutekeleza hilo baada ya muda mfupi
Demokrasia ina uwanja mpana, hivyo inapotokea kuna Watu wanaenda Mahakamani ndio Demokrasia yenyewe hiyo
Sisi CUF tunataka Siasa za hoja sio Siasa za chuki, nchi yetu inaamana kubwa kuliko maslahi ya Mtu mmoja mmoja, CUF ni wahanga wa Siasa za chuki, hatutaki kurudi huko tulipotoka
WAKILI WILLIAM MADUHU (LHRC)
Mwaka 1972, Mwalimu Nyerere alifuta Mamlaka za Serikali za Mtaa zote kwa maelezo kuwa hazikutimiza majukumu yao sawa sawa. Mwaka 1976 kukaibuka Kipindupindu ambapo baadhi ya Mamlaka zikarejeshwa
Mamlaka hizo zilirejeshwa Mwaka 1982, huko ndipo tulipotoka, lakini tulipo sasa Viongozi wengi wa Serikali za Mitaa hawana mishahara na hawana posho nyingine tofauti na ilivyo kwa Wabunge
Mbali na hapo Viongozi wa Serikali za Mitaa wamekuwa wakiingiliwa katika majukumu yao, mfano inaweza kutokea Mkuu wa Mkoa au Waziri anamuondoa kwenye nafasi yake Kiongozi wa Serikali za Mtaa, mamlaka ambayo hayapo kwake kwa kuwa Wananchi ndio waliomuweka madarakani
Kwa ufupi Serikali za Mitaa zinachukuliwa poa licha ya kuwa zina umuhimu mkubwa wa kuendesha Jamii na Wananchi kwa jumla, hili jambo sio sawa
Viongozi wa Mtaa hawana maslahi mazuri, hawana ofisi na wengine mazingira yao ya kufanya kazi sio mzuri