bryan2
JF-Expert Member
- Jun 8, 2016
- 3,323
- 4,679
Shule za Msingi burudani sana kuna watu kila siku lazima mifuko ya Kaptula au sketi inatuna.
Wengine walikua wakija na mahindi ya kukaanga/Ruketo hapa palikua pazuri mwalimu anapiga pindi nyie mnatafuna mahindi ya kukaanga ngojea asikie harufu mtakataana.
wengine mahindi ya kuchoma kapuchukua katia kwenye mfuko au mzima mzima hivyo hivyo
wengine Sukari hapa wengi hii walikua wanaiba nyumbani sidhani kama wazazi walikua wanawapa tena enzi zile sukari ni kama jiwe la tanzanite.
wengine Maandazi/Mikate hapo utakuta mfuko umejaa mafuta tu
Hili wachache watakua wanalijua Kuna kitu ilikua inaitwa KONGO huu ni unga wa mahindi unalowekwa na kukaangwa kabla ya kupikia pombe ya kienyeji aina ya BUZA kuna mafundi walikua wanakuja nao unachanga na sukari kitu kinakua poa ila inabidi mlie nje ya darasa manake hiyo harufu yake ni hatari.
Wengine mpaka ukoko wa ugali aisee na bado wana wanaomba wapewe.
Wengine wanakuja na Pipi halafu hapo unakuta kakwapua pesa ya mzazi kikinuka anataja wote waliokula pipi viboko kwa sana.
Wengine mpaka Nyama za kukaanga,Bana bana ilikua powa haya mambo ya ubuyu sijui kashata,sijui barafu,popcorn hayakuwepo kabisaa.
Wewe mfuko wako wa kaptula/Sketi ulikua haukosi nini??
Twende kazi.
Wengine walikua wakija na mahindi ya kukaanga/Ruketo hapa palikua pazuri mwalimu anapiga pindi nyie mnatafuna mahindi ya kukaanga ngojea asikie harufu mtakataana.
wengine mahindi ya kuchoma kapuchukua katia kwenye mfuko au mzima mzima hivyo hivyo
wengine Sukari hapa wengi hii walikua wanaiba nyumbani sidhani kama wazazi walikua wanawapa tena enzi zile sukari ni kama jiwe la tanzanite.
wengine Maandazi/Mikate hapo utakuta mfuko umejaa mafuta tu
Hili wachache watakua wanalijua Kuna kitu ilikua inaitwa KONGO huu ni unga wa mahindi unalowekwa na kukaangwa kabla ya kupikia pombe ya kienyeji aina ya BUZA kuna mafundi walikua wanakuja nao unachanga na sukari kitu kinakua poa ila inabidi mlie nje ya darasa manake hiyo harufu yake ni hatari.
Wengine mpaka ukoko wa ugali aisee na bado wana wanaomba wapewe.
Wengine wanakuja na Pipi halafu hapo unakuta kakwapua pesa ya mzazi kikinuka anataja wote waliokula pipi viboko kwa sana.
Wengine mpaka Nyama za kukaanga,Bana bana ilikua powa haya mambo ya ubuyu sijui kashata,sijui barafu,popcorn hayakuwepo kabisaa.
Wewe mfuko wako wa kaptula/Sketi ulikua haukosi nini??
Twende kazi.