OLS
JF-Expert Member
- Oct 12, 2019
- 426
- 685
Miaka kadhaa iliyopita kabla ya kuja kwenye digitali watu walilazimika kununua magazeti kwa sababu nyingi tofauti tofauti, jambo kubwa halikuwa kupata habari kujua yanayoendelea pekee
Sababu za kununua magazeti
Kwanza ilikuwa kuhabarisha lakini pia kujua matangazo ya serikali kama zabuni au minada, pia ilikuwa zitokea teuzi au watumishi kupata kitu fulani basi magazeti yalitumika
Vijana walinunua magazeti kuangalia nafasi za kazi au kutafuta wachumba(Pen Pals)
Wanafunzi walihitaji magazeti ili kupata mitihani au kupata majibu ya mitihani waliofanya
Kwenye ulimwengu wa digitali, habari inapatikana na kusambaa mara tu baada ya kitu kitokea, au ukitaka kukijua vizuri unaweza kuingia mitandao kama jamiiforums.com ukapata habari kiundani na sio kusubiria kesho yake, mambo mengi hufanyika kwenye websites husika, ajira zinapatikana kwenye portals, mitihani inapatikana kwenye apps na mengine mengi yamebadilika
Nini Kilifanyika
Hali hii ililazimisha magazeti kuwa na websites ili kuwahabarisha wateja wake, lakini websites ni gharama kwa anayeiendesha, Kwa ulimwengu wa sasa website inaongeza jina lakini ziko changamoto kadhaa katika nafasi hiyo
Kifupi naona usomaji wa magazeti umepungua kwa kuwa watu wamehamia kwenye ulimwengu wa digital
Baadhi ya makampuni yaliuza magazeti mtandaoni kupitia apps ili mtu aweze ku-subscribe na kupata huduma, lakini wabongo tabia za kununua vitu ni duni sana, fikiria kama mtu anataka antivirus ya bure anaweza kutoa hela kununua habari wakati anaweza kuisoma twitter nk, lakini pia walioko mtandaoi hawajui kuhusu vitu vingi vya mtandaoni na hii huleta changamoto nyingine
SULUHU NINAYOIONA
Kutokana na kuathirika kimapato magazeti yawe biashara huria, kusiwe na malipo serikalini ili kuwawekea uwanja mzuri wa watu kushindana katika kuhabarisha na kuburudisha
Badala ya kusaka habari, magazeti yawe ni ya kutoa vitu vyenye fikra(Makala) kwa kuwa katika uwanja huo ndio watu wanaeza kuona haja ya kununua, mnakumbuka umaarufu wa magazeti yaliyokuwa na makala zaidi kuliko habari kama Mwanahalisi, Tazama Tanzania, Rai, nk
NB: Maelezo haya hayatokani na tafiti bali yanasimama kama hypothesis
Sababu za kununua magazeti
Kwanza ilikuwa kuhabarisha lakini pia kujua matangazo ya serikali kama zabuni au minada, pia ilikuwa zitokea teuzi au watumishi kupata kitu fulani basi magazeti yalitumika
Vijana walinunua magazeti kuangalia nafasi za kazi au kutafuta wachumba(Pen Pals)
Wanafunzi walihitaji magazeti ili kupata mitihani au kupata majibu ya mitihani waliofanya
Kwenye ulimwengu wa digitali, habari inapatikana na kusambaa mara tu baada ya kitu kitokea, au ukitaka kukijua vizuri unaweza kuingia mitandao kama jamiiforums.com ukapata habari kiundani na sio kusubiria kesho yake, mambo mengi hufanyika kwenye websites husika, ajira zinapatikana kwenye portals, mitihani inapatikana kwenye apps na mengine mengi yamebadilika
Nini Kilifanyika
Hali hii ililazimisha magazeti kuwa na websites ili kuwahabarisha wateja wake, lakini websites ni gharama kwa anayeiendesha, Kwa ulimwengu wa sasa website inaongeza jina lakini ziko changamoto kadhaa katika nafasi hiyo
Kifupi naona usomaji wa magazeti umepungua kwa kuwa watu wamehamia kwenye ulimwengu wa digital
Baadhi ya makampuni yaliuza magazeti mtandaoni kupitia apps ili mtu aweze ku-subscribe na kupata huduma, lakini wabongo tabia za kununua vitu ni duni sana, fikiria kama mtu anataka antivirus ya bure anaweza kutoa hela kununua habari wakati anaweza kuisoma twitter nk, lakini pia walioko mtandaoi hawajui kuhusu vitu vingi vya mtandaoni na hii huleta changamoto nyingine
SULUHU NINAYOIONA
Kutokana na kuathirika kimapato magazeti yawe biashara huria, kusiwe na malipo serikalini ili kuwawekea uwanja mzuri wa watu kushindana katika kuhabarisha na kuburudisha
Badala ya kusaka habari, magazeti yawe ni ya kutoa vitu vyenye fikra(Makala) kwa kuwa katika uwanja huo ndio watu wanaeza kuona haja ya kununua, mnakumbuka umaarufu wa magazeti yaliyokuwa na makala zaidi kuliko habari kama Mwanahalisi, Tazama Tanzania, Rai, nk
NB: Maelezo haya hayatokani na tafiti bali yanasimama kama hypothesis