Ulimwengu wa digitali ni changamoto kwa magazeti

Ulimwengu wa digitali ni changamoto kwa magazeti

OLS

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2019
Posts
426
Reaction score
685
Miaka kadhaa iliyopita kabla ya kuja kwenye digitali watu walilazimika kununua magazeti kwa sababu nyingi tofauti tofauti, jambo kubwa halikuwa kupata habari kujua yanayoendelea pekee

Sababu za kununua magazeti
Kwanza ilikuwa kuhabarisha lakini pia kujua matangazo ya serikali kama zabuni au minada, pia ilikuwa zitokea teuzi au watumishi kupata kitu fulani basi magazeti yalitumika

Vijana walinunua magazeti kuangalia nafasi za kazi au kutafuta wachumba(Pen Pals)

Wanafunzi walihitaji magazeti ili kupata mitihani au kupata majibu ya mitihani waliofanya

Kwenye ulimwengu wa digitali, habari inapatikana na kusambaa mara tu baada ya kitu kitokea, au ukitaka kukijua vizuri unaweza kuingia mitandao kama jamiiforums.com ukapata habari kiundani na sio kusubiria kesho yake, mambo mengi hufanyika kwenye websites husika, ajira zinapatikana kwenye portals, mitihani inapatikana kwenye apps na mengine mengi yamebadilika

Nini Kilifanyika
Hali hii ililazimisha magazeti kuwa na websites ili kuwahabarisha wateja wake, lakini websites ni gharama kwa anayeiendesha, Kwa ulimwengu wa sasa website inaongeza jina lakini ziko changamoto kadhaa katika nafasi hiyo

Kifupi naona usomaji wa magazeti umepungua kwa kuwa watu wamehamia kwenye ulimwengu wa digital

Baadhi ya makampuni yaliuza magazeti mtandaoni kupitia apps ili mtu aweze ku-subscribe na kupata huduma, lakini wabongo tabia za kununua vitu ni duni sana, fikiria kama mtu anataka antivirus ya bure anaweza kutoa hela kununua habari wakati anaweza kuisoma twitter nk, lakini pia walioko mtandaoi hawajui kuhusu vitu vingi vya mtandaoni na hii huleta changamoto nyingine

SULUHU NINAYOIONA

Kutokana na kuathirika kimapato magazeti yawe biashara huria, kusiwe na malipo serikalini ili kuwawekea uwanja mzuri wa watu kushindana katika kuhabarisha na kuburudisha

Badala ya kusaka habari, magazeti yawe ni ya kutoa vitu vyenye fikra(Makala) kwa kuwa katika uwanja huo ndio watu wanaeza kuona haja ya kununua, mnakumbuka umaarufu wa magazeti yaliyokuwa na makala zaidi kuliko habari kama Mwanahalisi, Tazama Tanzania, Rai, nk

NB: Maelezo haya hayatokani na tafiti bali yanasimama kama hypothesis
 
Nasikitika umekuja na haya Maelezo yako marefu sana huku ukiwa umeshindwa Kutambua jambo dogo tu la kwamba hivi Vyombo vya Habari baada ya Kuiona Siku nyingi na Kugundua 'Changamoto' hii na wao upesi mno walibadilika na kuamua kuja katika upande wa 'Online' ambapo bado wanafanya vyema. Mfano Hai wa hili ni Gazeti la MWANANCHI na NIPASHE bila kusahau mengineyo baadhi.

Hata hivyo 'Wabobezi' wa Masuala ya Habari wanasema pamoja na ujio wa Mitandao bado 'Magazeti' yataendelea Kupendwa na Kununuliwa sana.
 
Nasikitika umekuja na haya Maelezo yako marefu sana huku ukiwa umeshindwa Kutambua jambo dogo tu la kwamba hivi Vyombo vya Habari baada ya Kuiona Siku nyingi na Kugundua 'Changamoto' hii na wao upesi mno walibadilika na kuamua kuja katika upande wa 'Online' ambapo bado wanafanya vyema. Mfano Hai wa hili ni Gazeti la MWANANCHI na NIPASHE bila kusahau mengineyo baadhi.

Hata hivyo 'Wabobezi' wa Masuala ya Habari wanasema pamoja na ujio wa Mitandao bado 'Magazeti' yataendelea Kupendwa na Kununuliwa sana.
Kipande cha online nimekizungumza, uhaba wa watu ku-subscribe kutokana na wabongo kutokuwa watu wanaopenda huduma za kulipia, utakuta nimeweka mfano wa mtu kushindwa kununua kitu muhimu kama antivirus

Kwa hiyo nimegusa huko.

Ila bado nasema ni hypothesis, it has to be tested kwa critical data analysis
 
Juzi nmeona Kampuni ya New Habari 2006 Ltd ambayo inazalisha magazeti ya Mtanzania, Dimba, Rai, Bingwa kusitishauzalishaji wa magazeti hayo kwa sababu ya Biashara kuyumba.

Naamini tunakoelekea magazeti hayakua unakuwepo, ila mitandao ndo itatamba zaidi.

IMG-20201204-WA0037.jpg
 
Enzi zile hili gazeti lilikua chini ya Jenerali lilikua na heshima sana. Mtu akikosa Rai au Dimba alikua haoni raha. It was a force to reckon with.

Alipoliuza na kuendeshwa na makanjanja ndio ukawa mwanzo wa mwisho wake. Huwezi kumfanya mpishi asimamie hospitali ukategemea matokeo chanya.
 
Swali la kijinga kabisa! Ungeuliza kwa nini magazeti kwa sasa hayatengenezi faida? Hapo angalau ungeonyesha unatumia kichwa chako kufikiri badala ya kufugia nywele!
 
Kila kitu mtandaoni sasahivi.. Hakuna mtu ananunua gazeti kusoma Habari za Jana.. Wakati 24 hours mtu anapata Habari kiganjani .... Pili magazeti hayana mvuto yanaandika Habari za upande mmoja tu..

Pia wenye magazeti wamekosa ubunifu na wamelala, wanaishi Jana... Wangecreate other source of income plus kuendana na mabadiliko......
Bado TV stations zijipange tu ,sasahivi mtu ana YouTube channel kumaliza kila kitu.. wewe TV station umeajiri engineers and other cost of operations
 
Habari za one side , nadhani nimesomeka , uccm ndo umewatia nuksi.
 
Ni mambo ya nyakati, hata huko online sio kivile (japo sina data)... mitandao ya kijamii inatosha kutuhabarisha.

Tunapenda kupata taarifa bure na kirahisi, kama kuna malipo ni labda indirect... binafsi kulipia kitu online sijui ku-subscribe huwa naonaje sijui. Siwezi!
 
Enzi zile hili gazeti lilikua chini ya Jenerali lilikua na heshima sana. Mtu akikosa Rai au Dimba alikua haoni raha. It was a force to reckon with.

Alipoliuza na kuendeshwa na makanjanja ndio ukawa mwanzo wa mwisho wake. Huwezi kumfanya mpishi asimamie hospitali ukategemea matokeo chanya.
Duuh haya magazet ya Rai ya enz hizo yalikuwa na hadhi ya kitabu, hulitupi, unasoma unalihifadhi ndani.

saiz waandishi wanatetea matumbo yao magazeti yamejaa mapambio kuogopa komeo...nyakati znakimbia kwa kasi.
 
Instagram imekuja kuua magazeti yote ya udaku.
 
Mchawi wa kifo cha magazeti anajulikana.Hakuna mtu mwenye akili timamu ambae atanunua magazeti ambayo yapo busy kumuimbia mapambio mtu mmoja tena ambae ni paralysed mind!
0659010.jpg
 
Back
Top Bottom