khomgodlove
Member
- Nov 17, 2018
- 33
- 22
Tusipo jibadilisha na kujiendeleza sisi kama Tanzania na Africa kwa ujumla tutakuwa watumwa wa kiteknolojia au watumwa wa kidigitali mbaya zaidi na ni bora hata ule uliopita . Kama nchi inabidi miaka hii ama ijayo ijitahidi kutenga hata kafungu kwa kiasi tu ili iwezeshe ugunduzi na uendelezaji wa ugunduzi kwa kununua teknolojia ama kutengeneza ya kwetu kwa hawahawa wasomi wetu . Lakini nchi pekee haitoshi kuyafanya haya pia itengeneze sera ambazo zitawaruhusu wazawa wenye uwezo kutengeneza vituo vya kufanyia utafiti wa kiteknolojia kwa maendeleo na ulinzi wa Taifa letu kwa sasa na vizazi vijavyo.