Anachosema
mshana jr ni kweli kulingana na bible. Biblia imeelezea predestination/kukusudiwa kimbele. Ndio maana Mungu alisema shukuruni kwa kila jambo. Liwe jema au baya tushukuru tu kwa sababu yeye ndiye kila kitu.
Ukitaka kuangalia pre destination kwenye Maisha yako chunguza hili. Ulipokuwa mtoto mdogo wakati ukikua uliwa na kupanga mambo mengi nanpengine kufikiria ungekuwa nani baadaye. Ungeoa mke yupi, watoto fulani, nyumba fulani etc.
Lakini leo almost mambo sivyo yalivyo salaaleh! Mahali ulipo hukuwahi kupawazia, status uliyonayo hukuwahi kuifikiria kabla, mke, watoto, mali na maisha kwa ujumla siyo yale uliyowazia zamani. Hii inaashiria nini??? PREDESTINATION.
Tangu unakuja Duniani ulishapangiwa njia ya kupita na huwezi kuikwepa. Hapa chini ni mfano wa pre destination unaoongelewa na Biblia:
Waefeso 1:3-5
[3]Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo;
[4]kama vile alivyotuchagua katika yeye kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu, ili tuwe watakatifu, watu wasio na hatia mbele zake katika pendo.
[5]Kwa kuwa alitangulia kutuchagua, ili tufanywe wanawe kwa njia ya Yesu Kristo, sawasawa na uradhi wa mapenzi yake.
Kwa hiyo ukijiona ni mkristo leo hujifanyi hivyo, bali ulishakusudiwa hilo tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu. Maana yake alikujua na kukuchangua kimbele ili uwe hivyo. Kwakuwa anajua mwisho kabla ya mwanzo ndio maana alikuwekea njia ya wewe kufikia kile alichokukusudia. Hilo ni kweli kabisa