ROHO, NAFSI NA MWILI
Ndugu msomaji,
Je, mwanadamu ni nani?
Kwa kifupi ninaweza kusema kuwa Mwanadamu ni Roho, ina Nafsi na inakaa ndani ya Mwili.
Ukisoma 1 Wathesalonike 5:23 Inatusaidia Kuona maeneo yote matatu ya mwanadam/mtu;
"Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi NAFSI ZENU na ROHO ZENU na MIILI YENU Mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo"
Hapa unaona Nafsi, Roho na Mwili vimetajwa kwenye hiyo aya.
ROHO NI NINI?
Roho ambayo inahusisha mambo ya Mungu.
Ni ile sehemu ya mtu yenye ufahamu wa Mungu, ambayo hufanywa hai na hutiwa nguvu na Roho wa Mungu wakati wa Wokovu. Kabla ya mtu Kuokoka, sehemu hii, haifanyi kazi kwa utimilifu kabisa kwa sababu ya dhambi. Dhambi huifanya kuondolewa nguvu ya kutenda kazi sawa sawa, kwa Amani na Roho ya Mungu. Lakini kupitia Ubatizo wa Roho Mtakatifu, mwanadamu hupokea nguvu ya kiroho, inayomwezesha kuishi maisha ya Kristo.
Roho inahusika na:-
i) Maombi na Ibada na Mungu,
ii) Ushirika na Mungu,
iii) Mapokezi ya karama za Roho,
iv) Vita vya kiroho,
v) Kuunda Mawazo na Ndoto,
vi) Dhamira, Kupambanua,
vii) Udadisi, Kuuliza,
viii) Ufahamu, Kutafsiri,
ix) Shuhuda kwa Wanadamu
NAFSI NI NINI?
Katika Biblia, neno “nafsi” limetafsiriwa kutoka kwa neno la Kiebrania neʹphesh na neno la Kigiriki psy·kheʹ. Katika Kiebrania neno hilo kihalisi linamaanisha “kiumbe kinachopumua,” na katika Kigiriki linamaanisha “kiumbe kilicho hai.”
Nafsi inahusika na mambo ya mtu.
Ni ile sehemu ambayo ina ufahamu wamtu mwenyewe au kiini cha ubinafsi wa mtu. Kazi yake ni:-
i) Kufikiri – Kutafakari, kuona
ii) Hisia – Kujisikia kuwa na tamaa na Upendo
iii) Utashi – Nia, Kuamua
MWILI NI NINI?
Mwili unahusika na mambo ya Ulimwengu.
Ni ile sehemu ya mwanadamu ambayo inafahamu na kukubaliana na ulimwengu wa nje. Inafanya yafuatayo:-
i) Utambuzi wa Ulimwengu, - yaani ile hali ya mwili kupokea habari kutoka Ulimwenguni kwa njia ya Ufahamu.
ii) Urejeshi – yaani ile hali ya Mwitikio wa kutenda kutokana na kutendewa kitu, kupitia utaratibu wa Maneno na Matendo.
iii) Udhihirisho – yaani ile hali ya Mwili ya kutoa habari za Ulimwengu kwa Mawazo, Kujisikia na Maamuzi ya Nafsi.''
Hivyo basi, Mtu ni Roho.
1) Mungu alimuumba mwanadamu kwanza kama roho ( Mwanzo 1:26) hapo bila mwili ndiyo maana Biblia inasema Mungu alimuumba mwanadamu kwa mfano wake kwa sababu Mungu ni Roho.
Mtu ambaye Mwanzo 1:26 inamuongelea, Biblia yenyewe inathibisha kuwa ni roho lakini yenye mwili wa rohoni (1 Korintho 15:44) ikiwa kuna mwili wa asili basi kuna mwili wa rohoni pia.
2) Mungu aliumba roho ya Mwanadamu kwanza ndio akaumba mwili wa nyama na nafsi baadae.
(Mwnzo 2:7) Mungu akauumba mwili wa Adamu kwa udongo akaichukua ile roho (kumbuka ina mwili wa kiroho) akaiweka/
ingiza katika mwili kwa kuipulizia ndani ya ule udongo alio uumba, na mtu akawa nafsi hai.
Hivyo basi;
Mwanadamu amegawnyika mara tatu
1) Roho yenye ufahamu wa mambo ya Mungu. Chakula cha Roho ni neno la Mungu.
2) Nafsi ni shemu yenye ufahamu ambapo vitu vya kujifunza au elimu au kumbukumbu vinakaa. Roho huitia nafsi nguvu au kuwa mahiri kwenye eneo fulani ambalo rohoni umebarikiwa ili hicho kitu kithiirike kwenye ulimwengu wa mwili.
3) Mwili ni sehemu ya mwanadamu inayo onekana na imebeba roho na nafsi.
Bonus question.
KUFA NI NINI?
Kufa ni kitendo cha roho kuachana na mwili, kama huyo mtu(roho) alipokuwa ndani ya mwili aliishi maisha matakatifu roho yake itakwenda kwa Mungu na kama aliishi maisha yasiyompendeza Mungu huyo mtu(roho) atakwenda kuzimu.
Hivyo basi itunze sana Roho yako maana wewe ni Roho una nafsi na unaishi kwenye mwili
Hii ndiyo maana wakristo wanahangaikia sana Roho maana wanajua Roho ndiyo inaenda kwa Mungu sio Mwili .
.
Ndugu yangu, maelezo yako haya ni miongoni mwa sababu za kuwazezetesha Waafrika. Hivyo napenda kusema haya....
==============================
MTAZAMO WA KIFALSAFA KUHUSU ULIMWENGU WA MWILI NA ROHO
Kifalsafa, na hasa kwa mujibu wa Plato, maneno ulimwengu wa roho ni kinyume cha maneno ulimwengu wa mwili. Plato anaongelea "sensible world (ulimwengu wa mwili)" dhidi ya "intelligible world (ulimwengu wa roho)." Katika sulimwengu wa mwili, tunapata maarifa kwa kutumia milango mitano ya fahamu--kuona, kunusa, kusikia, kulamba, na kugusa.
Na katika ulimwengu wa roho tunapata maarifa kwa njia tatu kuu. Kwanza, kuna kusafiri katika barabara kwa kuanzia kwenye upande wa ushahidi mpana kuelekea upande wa ushahidi mwembamba (deductive reasoning).
Pili, kusafiri katika barabara kwa kuanzia kwenye upande wa ushahidi mwembamba kuelekea upande wa ushahidi mpana (inductive reasoning).
Tatu, kuna kusafiri katika barabara mbili zilizo sambamba huku ukiwa unafananisha yale unayoyaona katika barabara hizo mbili (analogical/analytical reasoning).
Na njia ya nne, ambayo haikubaliki tangu mapinduzi ya kisayansi yalipobisha hodi duniani, ni ile ya ndoto na maoni. Ndoto ni maarifa yasiyoweza kuthibitika wala kukanushwa, ama na mtu yule yule aliyeota, au watu bado. Kwa maneno mengine ni ushirikina.
Kwa hiyo, hivi leo, maneno ulimwengu wa roho yanamaanisha ulimwengu wa akili inayofanya kazi kwa mujibu wa kanuni za kimantiki. Kanuni hizi ni za makundi matatu--inductive logic, deductive logic and analogical/analytical logic. Hilo ni somo rasmi katika vianga vya falsafa.
Hivyo, wale jamaa wanaosema kuwa wanaingia katika ulimwengu wa roho kwa njia ya ndoto na maono, lakini sio kwa kupitia kanuni za mantiki (logic), ni washirikina kama sio matapeli. Na wale wanaoyakubali yale wanayoambiwa na huyo anayedai kuota kuhusu yaliyoko katika ulimwengu wa roho ni wajinga. Wanahitaji kukombolewa.
Kilichowapata ni collective imbecilisation, yaani wamefanywa kuwa halaiki ya misukule inayoweza kuamurishwa ifanye inavyoagizwa, kila wakati na kila mahali. Huo ndio mtazamo wa kifalsafa kuhusu swali "ulimwengu wa roho ni kitu gani?"
Na kuhusu habari ya kifo, kisayansi tunasema hivi: Kifo ni tukio ambamo mwili wa kiumbe hai unapoteza nishati inayouwezesha kufanya haya: movement, excretion, respiration, reproduction, irritation, nutrition, growth.
Ni kama ambavyo sumaku ikigongwa kwa nyundo inapoteza nishati ya sumaku. Ni kama ambavyo flush ya kompyuta inapoteza data ikifomatiwa. Ni kama ambavyo kompyuta inapoteza program pale inaposhtuka kwa sababu ya umeme kukatika.
Programu, data na nishati ya sumaku haviendi mbinguni. Vinahama kwa mujibu wa kanuni zianazoongoza uhusiano uliopo kati ya maada na nishati, kama alivyoeleza Albert Eisntein katika mlinganyo wake huu: E=MC*C.
Miduara ya kibailojia, kijiolojia na kikemia (miduara ya bayojiokemia-biogeochemical cycles) kama vile mduara wa kabonidioksiadi (CO2), mduara wa nitrojeni dioksaidi (NO2), mduara wa Oksijeni (O2) na kadhalika, ni mifano hai kueleza jinsi protein za babu yako aliyekufa zinavyoingia kwenye mimea, ukala mimea na kupokea protein hiyo mwilini mwako. Matter is neither created nor destroyed.
Kwa hiyo habari ya kwenda "mbinguni" inaweza kuwa na maana moja tu: nishati kuingia katika miduara ya bayojiokemia kuanzia mwilini mwako, kwenye miamba, kwenye mimea, angani na kisha kurudi kwenye mwili wako. Kama mbingu inayoongelewa ni anga, nakubaliana na hoja ya "roho kwenda mbinguni."
Mchana mwema.