Ulinzi Shirikishi/ Polisi Jamii ni kuwasumbua Wananchi

Ulinzi Shirikishi/ Polisi Jamii ni kuwasumbua Wananchi

Nasema Uongo Ndugu Zangu

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2020
Posts
279
Reaction score
779
Katika mambo ya kipuuzi ambayo jeshi letu la polisi linayafanya ni hiki kitu kinaitwa ulinzi shirikikishi.

Sote tunajua maisha ya watanzania yalivyo, unakuta kijana anayejishughulisha na shughuli za kilimo jioni anarudi nyumbani hoi halafu unamtaka aingie mtaani eti kufanya doria ili kukomesha matukio ya uhalifu.

Kumbuka kuwa hana mafunzo yoyote ya kujihami, hana silaha ya maana zaidi ya zile za jadi na tochi matokeo yake ikitokea vijana hawa wamekutana na raia aliyelewa wanampiga na kujisifu kuwa wamepiga kibaka.

Sulala la usalama wa raia na mali zake ni jukumu la jeshi la polisi Tanzania, kama vile suala la ulinzi wa mipaka lilivyo chini ya jeshi letu la wananchi.

Haiwezekani tulipwe mishahara na serikali halafu tuwasumbue watu kutusaidia majukumu yetu.

Ipo siku vikundi hivi vya ulinzi vitakitana na wahalifu wenye silaha za moto na kwakuwa havina mafunzo vitapelekewa moto mpaka vikiambiwa viseme ubwabwa vinasema Wawa.

Nashauri serikali iajiri askari wakutosha tuachane na hii biashara haramu ya kuwasumbua watu usiku, tuwaache wapumzike baada ya mikiki mikiki ya utafutaji.

Tunawachukulia kodi, tunachukua tozo, tumeshindwa kuwasaidia kudhibiti mfumuko wa bei bado tunataka kuwaibia muda wao na ku risk maisha yao?

Hii ni dhambi Nasema Uongo Ndugu Zangu?
 
Nireteeni Gwaji Boy, akawakifo cha mende 19 MPS.
 
Hii kitu iko sehemu nyingi duniani.

Wenzetu wana national neighbourhood watch.

Mbona nyie wabongo mnataka kukaa kibwelelele.

Ova
 
Mgome, msubiri hadi watakapoajiriwa Polisi wa kutosha.
 
Katika mambo ya kipuuzi ambayo jeshi letu la polisi linayafanya ni hiki kitu kinaitwa ulinzi shirikikishi.

Sote tunajua maisha ya watanzania yalivyo, unakuta kijana anayejishughulisha na shughuli za kilimo jioni anarudi nyumbani hoi halafu unamtaka aingie mtaani eti kufanya doria ili kukomesha matukio ya uhalifu...
Nyie ndio wasumbufu kulipia ulinzi shirikishi. Sehemu nyingi option ni kulipia au kuamka kulinda. Kuna maeneo bila ulinzi shirikishi hali ingekuwa mbaya zaidi.

Ulinzi shirikishi unakwamishwa na watu wabishi kama nyie! Wengine ni wahalifu mnataka ulinzi ufe muwe huru!
 
Pole mkuu kwa kupigwa usiku wakati ukiwa umelewa chakari
 
Nyie ndio wasumbufu kulipia ulinzi shirikishi. Sehemu nyingi option ni kulipia au kuamka kulinda. Kuna maeneo bila ulinzi shirikishi hali ingekuwa mbaya zaidi.

Ulinzi shirikishi unakwamishwa na watu wabishi kama nyie! Wengine ni wahalifu mnataka ulinzi ufe muwe huru!
Kuna by law Sasa hivi usipochangia ulinzi shirikishi unapekekwa Polisi faini laki tatu.

Sasa utachaguwa mwenyewe uchangie hizo bukubuku Kwa mwezi au ukalipe faini laki tatu.

Kuna wajinga wengi sana nchi hii,vsiyo kila jambo ni siasa, halafu haohao ndio wanaosumbuliwa na vitoto vidogo tu eti panya road mpaka wabunge wa Magufuli akili zimewaruka wanataka binge lijadili huu upuuzi wa pants road wakati kuna Kamati za ulinzi na usalama kila kila Kata, wilaya na mkoa, ni ujinga mtupu.
 
Back
Top Bottom