Ulipo bei ya dagaa sh ngapi?

😆😆😆😂😂🙌Kumbe walala hoi tuna shida huko kwa washua
 
Hii margin ni ndogo sana. Mwenye mtaji wa gunia chini ya 20 kukatika ni kugusa tu.
Amini mkuu, huku visiwani wanaopiga hela ni wale wanaonunua wabichi kutoka kwa wavuvi then wanaanika wakikauka wanauza asee wanapiga hela ila ndo uwe na roho mvua ikipiga hupati hata mia wengi hua wanazimia kabisa
 
Dogo ajui kama mtaani watu wanabadilisha tu kama sio ugali dagaa basi ugali fulu
 
Bi mkubwa mstaraabu sana
 
Familia za kishua mbwa hawali dagaa mzee wanakula fresh meat kutoka buchani na chakula chao special " pedigrees" huyo maza maisha yake ya kawaida
 
Bongo kutoboa ni mziki
Kuna jamaa alikua anaaminika na maboss zake wa mikoani wanamtumia hela ananunua dagaa wakavu anawatumia siku moja kaingiwa na tamaa alitumiwa zaidi ya 2m za dagaa si akaona bora anunue wabichi aanike ndio awatume ili apige cha juu asee ilipiga mvua kaka sio poa jamaa akazima peleka dispensary then akatoka basi simu za maboss zake kuhusu mzigo hazikati jamaa alidata walikuja wakamzoa sijui walimpeleka wapi.
 
Lazima uzimie aiseee
 
Dagaa ni wa ziwa victoria, mchanga kuwepo ni waandaaji wanawaanika kwenye sehemu zenye mchanga tu. Hata mwanza (igombe) wanaanikwa sehemu isyo na mchanga
Mbn wakigoma huanikwa ktk mchanga na hawana mchanga
 
Hapa Mwanza Dagaa wa jero mnashiba sana na zinabaki
 
Ila dagaa wabichi ni watamu,unawachemsha unaweka pilipil na chumvi tu.

Mara ya mwisho sikumbuki nilikula lini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…