Hivi ilikwisha kukutoke hii...
Umekutana na pisi ukaimba fresh nayo ikasaini barida ila baadae unakutana na breking news kuwa ni mke wa mtu. Mbaya zaidi si mtu tu bali mwanao kabisa..
Situation hii ilinipata nikiwa Musoma mjini mitaa ya Nyakato. Kwanini nilifika hapa ni story ndefu ambayo inahitaji siku nzima kusimulia. Ila kumake it short Ni kuwa nilikuwa Musoma aka Mara.
Nyumba niliyokuwa nakaa ilikuwa ile ya mzunguko alafu mnakutana mtu kati. Wapangaji tulikuwa hatufiki kumi ila kulikuwa na kavurugu fulani asbuhi na jioni. Kama kawaida yangu mimi ni mtu fulani ambaye ni ngumu kuchangamana. Hivyo nikawa kivyangu vyangu, hata majirani nikawa siwajui wengine au majina yao.
Yupo jombaa fulani ambaye tulikuwa tunakutana mpirani sana, haswa ile ya usiku. Hivyo taratibu yule mwamba akawa mshikaji wangu pekee pale maskani. Na mimi na yeye ndio tulikuwa hatuna wake, mwanzo nilidhani hivyo. Kwa kuwa pia tulikuwa tunakutana kwenye mgahawa fulani pale mtaani.
Maisha yakasonga huku ushikaji wangu na mwamba ukakuwa. Nikiwa kwenye harakati za kupigania ukombozi kutoka kwa mkoloni mweusi. Nikakutana na pisi fulani kali kimtindo. Ni upwiru tu ndio ulinifanya nimfanyie ufisi ila hakuwa anamatch na standard zangu. Kwa kuwa kiswahili changu kilinyooka hakikuwa kile cha r na l, plus sound mchicha.
Mtoto akaona kaokota dodo chini ya mnazi fasta akanidondoshe digits. Sikulaza damu mchuzi wa supu unanyewa wa moto. Si nikashusha nondo somo la kutongoza hata nekta wasahihishe ovyo sikosi banda.
Zikafuata zile simu za night to morn, plus text za siku nzima. Ilikuwa inaboa ila ningefanya Nini na fisi niliitaka minofu.
Picha lilianza kuungua mara nilipomueleza ni wapi nakaa. Nikawa kila nikitaka mtoto aibuke Ngwea ananiletea visa mikasa.
Kila siku sababu haziishi. Nikawa kama nimechoka hivyo nikajipa mapumziko kwenye ile marathon.
Sasa sina hili wala lile niko home nafua j.pili si nikafuatwa na yule mwamba. Huku akinitambulisha kwa shemeji yangu ambaye ndio ile pisi. Pozi ziliisha kwa yule pisi kwa sababu mimi nilikuwa fresh na sikujua Kama kaolewa na yeye ndio alinificha.
Ila maisha yalisonga barida pasipo kuwepo na mvutano wowote. Wala hata tunda sikupata sitaki maswali!.