Sikusifii kwa jinsi ulivyowakaza hao wanawake ila nikupongeze tu wa jambo moja toka nimeanza kusoma visa vya wadau kwenye huu uzi naona angalau wewe unakumbuka kutumia zana.
Hamu ya siku moja tu inaweza kukuharibia future nzima ya maisha yako, sijui wengine wanapata wapi unajasiri wa kufanya mapenzi bila kinga, aiseh Mungu awasaidie sana.
*Wakati fulani kuna bar moja nilikua napenda sana kwenda kuangalia mpira (Epl) ila bar acha masihara, ina wanawake wazuri wenye kila sifa (wahudumu) waliokamilika kila idara, kuanzia sura, shape, makalio makubwa ndio usiseme, kifupi walikua kama kivutio cha utalii, ile bar wazungu wengi walikua wanapenda kufika sana kifupi ilikua classic kwenye kila kitu.
Kufuatia kwenda na kushinda pale kila weekend, nilitokea kuzoeana na dada mmoja hivi, mrembo balaa, since hakuna mtu ambaye hajawahi ku watch porn yule dada alikua anafanana sana na "Cherise Roze" mwanzo yule dada alikua anajibebisha (mdangaji) alitaka nikamtafune kwa elfu 60, nikamwambia hio pesa sina, tulivyotokea kua ma best akawa anataka hata bure tu nikamkaze. Nilimwambia kwa kazi yake na aina ya maisha anayoishi hata kwa kondom mia siwezi, nashukuru mwisho wa siku alinielewa na tukaishia kua marafiki, na katika urafiki huo nilikua na lengo la kumsaidia aachane na aina hiyo ya maisha aliyokua nayo, bahati mbaya sikufanikiwa kwa sababu baada ya muda fulani mkataba wake wa kazi uliisha akahamia sehemu nyingine tukaishia kuwasiliana kwa simu.
Lengo la kuandika hili bandiko, ni hili, katika siku tulizojuana na yule dada nilijifunza kitu kimoja kutoka kwake, yule dada alinieleza ukweli (uhalisia) aliniambia hivi namnukuu
"Katika maisha yako yote usimuamini mwanamke hata kama akiwa mke wako wa ndoa, mimi ni mwanamke na nimefanya kazi bar mbalimbali katika uzoefu wangu wa kazi hii nimekutana na nimeona mambo mengi, nimeona wake za watu wakigongwa, wanavyuo wakidanga, watoto wa kike wa mitaani, ma house girl wakiliwa kifupi nimeshuhudia uchafu mwingi kwa wanawake mbalimbali, japo waaminifu wapo ila katika mia moja unaweza kukuta hata kumi hawafiki, akaniambia tena katika maisha yako yote "USIFANYE MAPENZI NA MWANAMKE YOYOTE YULE BILA KINGA, HATA AWE BIKRA (wapo wanaozaliwa navyo)" utakuja kufa kwa ukimwi.
Nakumbuka nilimuuliza mfano kama nimeoa hata mke wangu nitumie kinga, alinijibu "Kwa mkeo sawa nenda dry ila usimuamini kabisa kama inawezekana siku ukiwa na familia jenga mazoea ya kupima afya kila baada ya kipindi fulani.
Yule dada alinipa elimu kubwa sana mambo mengine mengi siwezi kuyaandika hapa. Ila nitoe wito kwa kaka zangu, wengi humu familia zetu zinatutegemea uwe umeoa au ujaoa "ukiacha mke na watoto bado wazazi wetu pia wanatutegemea tuwape back up ili wa survive, siwasemi vibaya watu wenye maambukizi hapana, ila kijana ukiupata huu ugonjwa kuna energy fulani ya kupambana na maisha inapungua.
Msisahau kutumia zana, pamoja na ugwadu sio kila msichana na wa kupita nae.
Samahani sana kama nimeharibu uzi ila wakati tunafurahi kula tunda kimasihara tusijisahau tukaja kufa kimasihara.