Wakuu kuna siku 2009 nilipatwa na mshangao usio wa kawaida, nakumbuka ilikuwa naishi Mtoni kwa Azizi Ally siku hiyo ilikuwa saa 6 usiku nikiwa na mshkaji gheto, nilikuwa nimesharoll wigi[emoji377] nasubiri kuliripua ili tupate stimu za kulalia, kumbe mlango wa gheto tulikuwa hatujafunga. Ghafla kaingia mdada mbio ndani huku anaomba hifadhi "Kaka zangu nawaomba mnihifadhi kuna mtu anataka kunibaka" huku akiwa analia. Ikabidi mshkaji afunge mlango kwanza ili tumuulize vizuri kulikoni. Yule dada alikuwa mzuri, kiportable flani hivi miguu ya chupa ya bia na ana macho ya nyege, akatueleza kuwa anaitwa Joyce (Sio jina lake halisi) ametokea Mwananyamala na amekuja hapo Kwa Azizi Ally kwa mwanaume wake. Lakini siku hiyo alikuja kumtembelea tu kwa vile alikuwa period, hivyo mwanaume wake akawa anataka mlango wa nyuma, ndipo akakimbia, yule mdada jamani alituomba sana hadi alifika hatua ya kufunua top yake na kutuonesha K alivyoivisha pedi.
Mshkaji akanibonyeza ili kama vipi tulale nae, ila siku hiyo nilikuwa mwema sana, nikamwambia hapana. Nikamuuliza vizuri yule dada kama labda alipigwa au kujeruhiwa popote, akajibu alikabwa shingoni kidogo na hana jeraha lolote jingine mwilini. Aisee! Nikamwambia mshkaji tumsindikize kituoni tumpe na nauli ili apande gari aondoke zake. Basi tulimpa 5000 na kumsindikiza hadi Kituo (Kwa Azizi Ally kituo cha kupandia kuelekea kariakoo) likaja gari la Msasani akapanda na kutushukuru kwa msaada tuliompatia.
Funzo: Muda mwingine toa msaada bila kuweka lengo maalum au kuhitaji malipo kwa msaada uliotoa
Baada ya hapo tukapitia chipsi pale tukachukua kiepe na kurudi gheto, tukala, tukavuta bangi yetu na kulala [emoji38][emoji38][emoji38][emoji23][emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji377][emoji377][emoji377][emoji2445][emoji2445][emoji2445]