Ulishawahi kunusurika kifo? Nini kilikuwa chanzo na njia gani ulitumia kujinisuru?

Ulishawahi kunusurika kifo? Nini kilikuwa chanzo na njia gani ulitumia kujinisuru?

Chambichambi

Senior Member
Joined
May 23, 2022
Posts
139
Reaction score
229
Habari Watanzania!

Leo nina stori ya kweli ambayo imetokea katika maisha nikiwa mkubwa hivi. Basi bwaana baada ya kumaliza masomo nilianza vijikazi vya hapa na pale kuendesha maisha yangu. Nilipigana kama miezi 5 bila mafanikio.

Niliamua kwenda mwambao wa ziwa Victoria kuangalia fursa zingine za kufanya ili kutimiza ndoto yangu ya kumiliki mihela. Nikafikia kambi moja ya uvuvi wa dagaa nikajieleza kwa wavuvi kuhusu kutaka kujifunza uvuvi.

Nilifanikiwa kupata mtu ambaye alikubali kunifundisha japo nilikuwa sifahamiani na yeye. Basi jamaa alinitambulisha kwa wenzake wanaotega nao mtumbwi mmoja. Baada kula saga nilienda nikakaa sehemu nikalia sana lakini nikasema yote maisha.

Basi baada ya siku mbili ilifika mbala mwezi ya saa 5. Tukaenda ziwani sasa siku ya kwanza. Nakumbuka siku hiyo tulienda maji ya meli, ziwa lilikuwa limetulia kama mkeka. Tukatega kesho yake mimi mwanafunzi nilipewa Tsh 27,000 na mboga kama sado ya dagaa mbichi. Badae nikawa mzoefu nakaanza kwenda visiwani.

Nakumbuka ilikuwa mwaka jana nikiwa kisiwa fulani niliugua miguu mpaka hata kutembea nikawa siwezi. Nilijikaza kisabuni lakini wapi. Nikatumia kila kitu miguu bado. Nikaomba msaada nyumbani nikapewa nauli nikaenda home.

Aiseee nilivyofika kila mtu alikuwa anashangaa na kuniuliza kuwa nimefanya nini? Dah! Kwakweli sitosahau kipindi hicho nilikuwa sipati usingizi usiku miguu ilikuwa inauma kinoma.

Baada ya hiyo hall kuna ndugu baadhi walianza kunichukulia kama mtu ambaye sijiwezi kwani nilidhihirisha kuwa kazi za uvuvi ni kazi za watu duni. Sasa kila siku ikawa ni mabango na kauli za kejeli kama, "elimu yako haikusaidii kitu". Sema niliumia sana mpaka nikaamua kujaribu kujua. Niliamua kula vidonge 26 na konyagi kubwa ili nife.

Asikwambie mtu nilikaa ndani siku 5 nikisubili kufa bila mafanikio. Badaye nilijikuta nimetundikiwa drip za maji huku nikiuliza huku nimefikaje?
 
Kwamba umepiga konyagi bapa nzima, na vidonge 26 vya paracetamol, kisha ukakaa ndani kwa siku 26 bila kufa?😂😂😂

Oyaa, unatuoanaje jombaa?

Hebu tafuta chai nyingine ambayo kidooooogoo in sound.
 
We nawe tego lako kubwa na Kali sana, yaani vidonge 26 na mzinga mkubwa wa konyagi na Bado umesavaivu?
 
Me nilikunywaga banana kumi nilihisi roho inachomoka sijanywa Tena pombe ile Bora gongo asee
 
2004 nilivutwa na wajinga ( kama 5 ivi ) kwa nguvu kwenda kina kirefu cha maji,
nilikunywa vikombe vya kutosha, macho mekundu, kabla ya 'kazin' kuja kuniokoa
 
Siku 5 na siyo 26
Kwamba umepiga konyagi bapa nzima, na vidonge 26 vya paracetamol, kisha ukakaa ndani kwa siku 26 bila kufa?😂😂😂

Oyaa, unatuoanaje jombaa?

Hebu tafuta chai nyingine ambayo kidooooogoo in sound.
 
Kijijini huko, tulikua tunalala chini, mlango unafungwa na mchi wa kutwangia makopa, unakua mkbwa mara nyingi ni mchungwa uliokomaa.
Sasa nimelala nashtuka nakuta mchi (mtwangio) umeanguka pembeni ya kichwa changu, ni inchi kadhaa ungenipiga kichwani na lazima ningepasuka.

Here i am now living in my own beautiful house. Life can change so dramatically. All in all glory to God
 
Kijijini huko, tulikua tunalala chini, mlango unafungwa na mchi wa kutwangia makopa, unakua mkbwa mara nyingi ni mchungwa uliokomaa.
Sasa nimelala nashtuka nakuta mchi (mtwangio) umeanguka pembeni ya kichwa changu, ni inchi kadhaa ungenipiga kichwani na lazima ningepasuka.

Here i am now living in my own beautiful house. Life can change so dramatically. All in all glory to God
Pole sana but skul si jepesi kama yai so ni wasi wasi wako tu kuwa huo mwichi ungeliwezapasua fuvu lako.
 
2004 nilivutwa na wajinga ( kama 5 ivi ) kwa nguvu kwenda kina kirefu cha maji,
nilikunywa vikombe vya kutosha, macho mekundu, kabla ya 'kazin' kuja kuniokoa
Haya mambo ya kuogelea haya kuna mwamba tulimkuta mtoni na crew yake hawezi kuogelea alikunywa vikombe tumbo kubwa macho mekundu anaelea akafa na crew alienda nayo hakuna anayejua kuogelea kwenye kundi letu kuna mwamba aliwahi kwenda kumuokoa ila ilikua too late

Wahuni tulinyembu ndukii nani anataka ushahidi tukaacha wana na mzoga wao
 
Kijijini huko, tulikua tunalala chini, mlango unafungwa na mchi wa kutwangia makopa, unakua mkbwa mara nyingi ni mchungwa uliokomaa.
Sasa nimelala nashtuka nakuta mchi (mtwangio) umeanguka pembeni ya kichwa changu, ni inchi kadhaa ungenipiga kichwani na lazima ningepasuka.

Here i am now living in my own beautiful house. Life can change so dramatically. All in all glory to God
Duh! Hatari sana
Haya mambo ya kuogelea haya kuna mwamba tulimkuta mtoni na crew yake hawezi kuogelea alikunywa vikombe tumbo kubwa macho mekundu anaelea akafa na crew alienda nayo hakuna anayejua kuogelea kwenye kundi letu kuna mwamba aliwahi kwenda kumuokoa ila ilikua too late

Wahuni tulinyembu ndukii nani anataka ushahidi tukaacha wana na mzoga wao
😀😀😀
 
Back
Top Bottom