Ulishawahi kusikia kisa cha Ivan Zamorano na Ronaldo De Lima kuhusu Jezi namba 9

Greatest Of All Time

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2017
Posts
23,620
Reaction score
52,790
Wakati Ronaldo Luiz Nazario De Lima aliposajiliwa Inter Milan mwaka 1997 alikuta jezi namba 9 inavaliwa na mshambuliaji mahiri wa Chile, Ivan Zamorano.

Hivyo kutokana na sababu za kibiashara Ronaldo akaomba apewe yeye jezi namba 9, Zamorano atafutiwe namba nyingine. Kitendo hiko kikaleta mgongano mkubwa sana kwa Zamorano. Mwishoe akakubali yaishe Zamorano akaiachia jezi namba 9.

Zamorano akaomba apewe jezi namba 18 ambayo katikati ya namba 1 na 8 akaweka alama ndogo ya jumlisha ambayo jibu lake unapata namba 9. Kwa hiyo mgogoro ukawa umeishia hapo. Kazi ikaendelea ya kipachika mabao...

 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] Huyu Zamorano yuko humu?
 
Baada ya kukabidhiwa hiyo jezi namba 9 ndio ukawa mwisho wake Ronaldo. mana mpira ulimshinda kabisa pale Inter mpaka akatimka.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…