Uliyeajiriwa na unaamini maisha bila ajira magumu sana, ungeishi kipindi cha ujima ungekuwa nani?

Uliyeajiriwa na unaamini maisha bila ajira magumu sana, ungeishi kipindi cha ujima ungekuwa nani?

Mc cane

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
5,570
Reaction score
10,517
Habari wakuu,

Ni swali ambalo nimekuwa nikijiuliza, kwamba kuna watu wanasema kuacha kazi na kuamua kufanya mambo yako ni kujiingiza kwenye mkenge ambao maisha yako yote utajutia

Najiuliza na ninawauliza watu wenye mentality hii, enzi za ujima (ingekuwa tupo ujimani kwa sasa) hawa watu wangekuwa nani?

1. Wabeba nyama za wawindaji, ili na wao wapate kamgao kao ikifika jioni muda wa kurudi nyumbani?

2. Walinzi wa nyama za wawindaji maarufu katika jamii yao?

3. Waokota matunda na wabeba matunda ya mabwana wakubwa ili nao jioni wapate mgao wao?

4. Watengeneza mitego ya wanyama ili jioni wapate ujira wao?

Najiuliza tu wakuu
 
Kwenye maisha issue sio kuajiriwa issue ni unaingiza kiasi gani.
Wapo maelfu ya watu wamejiajiri faida yao kwa Siku kwa biashara zao ni zaidi/chini ya laki 5 wanafanya kazi masaa 12 Siku 7 za wiki.......wapo waliajiriwa wanakula zaidi ya M wanafanya kazi Siku 5 za wiki masaa 8.
Wapo walioajiriwa na wamejiajiri vile vile, mtu ni jaji take home M5 ana masupermarket town amewaajiri vijana.
Kwenye maisha mjanja ni anayeingiza income kubwa.
Ujinga unajisifu umejiajiri/umeajiriwa unafanya kazi 12 hours 7 days a week,unazidiwa na waliojiajiri/walioajiriwa wanafanya kazi 8 hours 5 days wanakula mpunga mara 3 zaidi yako.
Mwisho sio kila MTU anaweza kujiajiri ama kuajiriwa.
 
Hao walioajiriwa na wanalipwa 1,000,000± ni wachache mno ukilinganisha na waliojiajiri na wanaopata 1,000,000± hapo bado kodi ambazo TRA wanachukua kabla fedha haijatua mikononi mwako. Na wengi (hapa nimesema wengi, siongelei waajiriwa wachache ambao kwa Serikalini wapo kwenye government parastatals) wanaopata hicho kiasi wapo jioni kwenye vibarua vyao hivyo

Kufanya kazi siku 5 kati ya 7 kwa wiki ni kudanganyana, kufanya kazi masaa 8 kati 24 kwa siku ni kujazana uongo. Ukweli ni kwamba walioajiriwa wanafanya kazi zaidi ya muda uliandikwa kwenye makaratasi.

Umeajiriwa unapata hiyo 1,000,000+ kwa mwezi at what expense, kujipendekeza, kudhalilishwa, kusimangwa n.k. Kuna vitu hatuwezi kuvi calculate financially lakini ni gharama kubwa, ikiwamo kukosa furaha

Nakubaliana na wewe cha msingi ni unaingiza kiasi gani, lakini kimoja ninachojua aliyejiajiri ana potential ya kutengeneza kuliko aliyeajiriwa, mlamba miguu wa mabwana wakubwa

spleen,
 
Duniani kote wapo waliojiajiri wapo pia wanaofanya kazi kwenye serikali.....chaguo ni lako..........
After all hata machinga,wanaouza vitu barabarani nao wamejiajiri
Pia haikatazwi kuajiriwa ukawa umejiajiri una duka lako ukitoka kazini unauza.......haikatazwi,na haina haja ya kushindana na mtu.....dunia huru hii






Mc cane,
 
spleen, Kiukweli ujanja nikuingiza pesa ndefu. Mimi binafsi nimejiajiri naninafanya kazi siku 7 katika wiki yaani wiki yote nipo kijiweni kwangu namasaa kwasiku nafanya kazi zaidi yamasaa 12 maana nafungua ofisi saa 2 asubuhi nafunga saa2 usiku ila kipato changu nikidogo hakiendani namda namasiku nayofanya kazi.
 
Pole na hongera

Lakini kwa maelezo yako unaonekana huna miaka zaidi ya 3 kwenye hizo shughuli zako

Ukikaa angalau miaka 5, utaweza kufanya shughuli zako kwa ku relux zaid
Kiukweli ujanja nikuingiza pesa ndefu. Mimi binafsi nimejiajiri naninafanya kazi siku 7 katika wiki yaani wiki yote nipo kijiweni kwangu namasaa kwasiku nafanya kazi zaidi yamasaa 12 maana nafungua ofisi saa 2 asubuhi nafunga saa2 usiku ila kipato changu nikidogo hakiendani namda namasiku nayofanya kazi.
 
Sio lazima kuna wadau kibao toka miaka ya 2008 nawafahamu hadi leo ni machinga pale mchikichini.
OK kumbe unazungumzia kurelax tu na si kuingiza mkwanja mnene
Pole na hongera

Lakini kwa maelezo yako unaonekana huna miaka zaidi ya 3 kwenye hizo shughuli zako

Ukikaa angalau miaka 5, utaweza kufanya shughuli zako kwa ku relux zaid

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukitengeneza mfumo thabiti, wakati mkwanja unaendelea kuingia, kwanini usi relux

Kama tangia unaanza ujasiriamali unaamka saa 10 alfajiri na kulala saa sita usiku mpaka unastaafu ujasiriamali ratiba yako ni hiyo hiyo, unapaswa kujichunguza na ikibidi upimwe mkojo
Sio lazima kuna wadau kibao toka miaka ya 2008 nawafahamu hadi leo ni machinga pale mchikichini.
OK kumbe unazungumzia kurelax tu na si kuingiza mkwanja mnene

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Swala la kuajiriwa nilishakataa,mimi ni mchapa kazi sana so siko tayari kuona natumia ubunifu na uchapa kazi wangu alafu nalipwa robo ya nguvu niliyoiweka,kikubwa wanakula mapimbi fulani huko,then mafao yangu wanitese kama sikufanya kazi..noo way...pia mimi naamua niwe wapi muda gani.

Maisha ni kuchagua,no offense kwa mlioajiriwa naimani kuna faida pia mnazipata,binafsi nilpima hasara tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom