Umaarufu wa 'Godzilla' baada ya Kifo!

Pazi na Jogoo

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2016
Posts
331
Reaction score
494
Msanii maarufu wa muziki wa Hip Hop Golden Mbunda maarufu Godzilla baada ya kufariki ndipo wengi watamfahamu na kutaja sifa zake.

Ni tabia ya 'kipuuzi' iliyozoeleka Mara mtu anapofariki ndipo tunakumbuka umuhimu na mchango wake katika nyanja inayomuhusu na wengine wana kwenda mbali na kuthubutu kupokea michango ya rambirambi kwa ajili ya manufaa yao binafsi, hii ni aibu isiyo na kifani!

Nimeona katika mitandao mbalimbali watu wame-publish video clip za interview na michano ya Godzilla wakiwa na maana ya kukumbuka, kutambua na kuthamini kazi na mchango wake katika muziki, na hii imetokea baada ya Kifo chake!

Hoja yangu ni kuwa kwa nini mambo Haya yasifanyike angali mtu akiwa hai, kwani kwa jinsi inavyofanyika sasa haiwezi kumnufaisha kwa jinsi yoyote,,,,,Tunaweza kujifunza!!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu huo ni utamaduni wa mwafrika ... ndo mana ukiweza kuishi afrika hata motoni unaishi bila wasiwasi.. ndo mana mtu akiwa ni mgonjwa taabani watu huwa wanamkimbia hata ukiambiwa uchangie hela za matibabu watu hawatoi ila ukifa sasa watu kibao wanachanga... so ni utaratibu wa kiafrika
 
Kwani ww hujui wanavyosema ukitaka kutambua umuhimu wa mtu mpaka aondoke?
 
Mkuu watu weupe wao wametosutishwa na sisi? Ndicho unajaribu kumaanisha?
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimefuatilia nyuzi zako zote za humu JF hakuna hata mmoja unaozungumzia sanaa au wasanii zaidi ya ule wa amberruti kufaa kuigiza filamu za ngono.
Inshort na wewe ni walewale tu.
 
Mbona Godzilla ni msanii mkubwa tu binafsi nilikuwa namsikiliza muda mrefu sana tangu miaka ya 2010 ila ni kawaida ya wasanii wa mziki wa aina yake kuwa na umaarufu wa kawaida

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona iko hivyo duniani kote..unamjua Xxtentacion aliyefariki mwaka jana na album yake ikawa kwenye top chart za billboard??

United Fan
 
Acha unafiki, kwani Zilla kabla hajafa alikuwa hapewi sifa anazostahili?

Hilo jina la King Zilla a.k.a mfalme wa free style ukipenda muite rais wa Salasala alipewa kipindi yupo hai au marehemu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…