Umasikini ule ulitutesa sana, Isijirudie tena...

Umasikini ule ulitutesa sana, Isijirudie tena...

Nakumbuka zama zile za miaka ya 1983 hadi 1984, niko tunaishi mitaa ya Makutano Mabibo jijini Dar es salaam na Kadi yangu ya Rangi ya Kijani ikiwa na maelezo ya Kaya yetu ndani Mwake.

Mchana wa jua kali la Darisalama tukiwa tumekaa barabarani kusubiri gari la "Ugawaji" litaelekea mwelekeo upi na sisi tulifukuzie kwa nyuma. Hakuna aliyejua leo ni zamu ya duka gani kupelekewa chakula ama mahitaji mengine muhimu ili wakazi wa eneo letu waende wakanunue.

Shuleni wanafunzi wanavaa nguo zisizo na rangi maarufu kama "Maradufu" kutokana na viwanda vya kuzalisha nguo kukosa rangi za kuweka ili vitambaa hivyo viwe na rangi ya Bluu Maalum zama hizo kwa sare za shule za msingi.

Mitaani watu wanavuta sigara kwa "Puff" kwa hela ulizo nazo. Watu wanafua nguo zao kwa kutumia majani ya mpapai, sukari inakaangwa ili kutengeneza chai kwa kuwa hakuna majani ya chai na wenye majani ya chai wanaweza kutumia sukari guru badala ya sukari ya kawaida kama kiungio.

Unakwenda kwenye duka la ushirika kwa mfano kununua Sukari unalazimshwa kununua na kitu kingine kwa mfano Chujio la chai ama birika. Watu wa Darisalama tuliteseka sana na wanawake wengi walibakwa na watu waliojifanya wana bidhaa hizo "adimu" majumbani mwao..

Wakati ule Mgambo na wenyeviti wa maduka ya Ushirika walikuwa kama ni Miungu watu. Sisi kwetu kulikuwa na mgambo aliyetembea na wake za watu alivyopenda kisa yeye ana nafasi kubwa sana ya kupata vitu kwenye duka la Kaya la Mtaani kwetu.

Hayo yote yalisababishwa na Ugomvi wa Mwalimu JK Nyerere na wakubwa wa IMF na World Bank. Umaskini ule ulitutosha hatutaki hali ile ijirudie tena kwenye kizazi hiki.

CC: Mshana Jr Pascal Mayalla

Mkuu, this is 2019?? Technology has gone so far, Stop being stranded in the past. Dunia haiko hivyo tena.
 
Mkuu, this is 2019?? Technology has gone so far, Stop being stranded in the past. Dunia haiko hivyo tena.
Sijaelewa unataka kumaanisha nini. Kila nyakati huwa na teknolojia ya wakati wake nayo huwa ni ya hali ya juu kwa wakati husika.

Hii mada inahusiana nini na maendeleo ya Teknolojia?
 
IMF Wakikutaa hakuna mmagharibi atakayekukopesha,atakayenunua treasury bills zako,atakayekuja kufanya uwekezaji wa maana kwako,atakayekupa msaada,kama walikuwa wanakudai na muda wa kulipa deni umefika hautapa huruma ya debt restructuring.
Sijuaji kwani hawa IMF wakiikataa nchi yoyotre kinachofuata ni ukame .
Mfano angalia Zimbabwa na Nchi nyingine ziliingia kwenye mtego huu
 
IMF na WB ni pande mbili za shilingi moja,AFDB inapata pesa zake nyingi kutoka huko huko kwa hao 'mabeberu' nchi za Scandinavian no wananchama na washirika thabiti wa WB na IMF,hivyo ulichokiandika hapa ni ugoro mtupu.
Kuhadiwa kupatiwa hiyo mikopo/misaada ni jambo moja,kupewa baada ya kutimiza vigezo na masharti ni jambo lenginie,rejea ahadi ya ule mkopo wa USD 300M kwa ajili ya elimu na wanafunzi wanaopata mimba kama umeshapatikana mpaka sasa
Kuna kitu kikubwa ambacho wengi hawajaona ktk kauli ya IMF (kama ikithibitishwa ni kweli wametoa hio kauli):

Miradi mingi ya Maendeleo inayotekelezwa na GoT inafadhiliwa/inakopeshwa na washirika wa maendlzeo kama WB, AFDB, JICA ama Scandnavian countries, na hilo hufanyika baada ya wao kuridhika na mapendekezo na mpango wa utekeleza wa GoT.

Ni muda mrefu sasa tangu IMF itoe mkopo/msaada wa aina yeyote ile kufadhili miradi ya Maendeleo ktk TZ. Hali ni tofauti kwa WB, AFDB, JICA ama Scandnavian countries ambao wako bega kwa bega na GoT na hata zikitokea tofauti hua zinamalizwa and life goes on bila kushinikizana kwa kutumia magazeti au waandishi wa habari wa Kenya.

Haingilii akilini kuona IMF ianatoa matamko yanayo pingana na washirika wengine ndani ya siku 2 tu tokea washirika hao (WB, AFDB, JICA) waingie makubaliana ya mikataba ya kukopesha TZ zaidi ya Tsh Trillion 2 za utelelezaji wa miradi ya maendeleo.

Eti IMF wanaita miradi hio kuwa haina maaana kwa Maendeleo ya TZ, swali la kujiuliza, je hivi washirika hao wengine wa maendeleo hawajaliona hilo wakati wanafanya due diligence kabla ya kukubali kutoa hizo fedha za miradi (i.e, BRT, SGR, Elimu, Steglers, Afya)?

Kwa hali ilivyo inawezekana kabisa:

  1. Kuwa IMF wanafanya maksudi ili kutengeneza hali ya hofu na kuchafua investment climate ya TZ duniani ili wabia wetu wa maendleo na wawekezaji waogope kushirikiana na GoT. Then tuwapigie magoti wao waje na bail-outs kutuokoa at their own terms; ama
  2. kuwa kuna watu walioko ndani ya TZ na nje wanashirikiana kwa kupeleka habari hasi IMF ili kuishinikiza GoT ibadili misimamo yake kwenye mambo kama sera za madini, energy (umeme), etc, ili GoT ikubali kuweka sera za kunufaisha makampuni yao.
Ikumbukwe kuwa IMF ni chombo amabacho kimekuwa kikutumiwa kuharibu uchumi wa nchi nyingi duniani kuanzia Latin Amerika (Brasil, Argentina) , Ulaya (Greece, etc), Asia na hata Afrika (Kama OP ulivyoeleza enzi za Mwl. Nyerere au hata Kenya miaka ya hivi karibuni). Huwa wanashinikiza nchi husika kufuata maelekezo yao kama vile kuuza viwanda vya ndani, kubinafsisha SOEs etc na baada ya hapo hali huwa inabadlika kuwa mbaya zaidi nya awali na huleta uasi na machafuko ya kijamii.

Cha muhimu ni kwa GoT kuhakikisha Kuwa haichukui mkopo wa aina yeyote toka IMF period. Kama tayari mikopo hio ilikuwepo toka zamani basi wendelee kuilipa lakini kamwe wasikuckue mikopo yao mipya.
 
Brain-app kuna watu hawajui kwamba hata hiyo China tunayoiona kama ndiyo mkopeshaji wetu salama na yenyewe inakopa huko kwa mabwana wakubwa hao WB/IMF.
 
Nakumbuka zama zile za miaka ya 1983 hadi 1984, niko tunaishi mitaa ya Makutano Mabibo jijini Dar es salaam na Kadi yangu ya Rangi ya Kijani ikiwa na maelezo ya Kaya yetu ndani Mwake.

Mchana wa jua kali la Darisalama tukiwa tumekaa barabarani kusubiri gari la "Ugawaji" litaelekea mwelekeo upi na sisi tulifukuzie kwa nyuma. Hakuna aliyejua leo ni zamu ya duka gani kupelekewa chakula ama mahitaji mengine muhimu ili wakazi wa eneo letu waende wakanunue.

Shuleni wanafunzi wanavaa nguo zisizo na rangi maarufu kama "Maradufu" kutokana na viwanda vya kuzalisha nguo kukosa rangi za kuweka ili vitambaa hivyo viwe na rangi ya Bluu Maalum zama hizo kwa sare za shule za msingi.

Mitaani watu wanavuta sigara kwa "Puff" kwa hela ulizo nazo. Watu wanafua nguo zao kwa kutumia majani ya mpapai, sukari inakaangwa ili kutengeneza chai kwa kuwa hakuna majani ya chai na wenye majani ya chai wanaweza kutumia sukari guru badala ya sukari ya kawaida kama kiungio.

Unakwenda kwenye duka la ushirika kwa mfano kununua Sukari unalazimshwa kununua na kitu kingine kwa mfano Chujio la chai ama birika. Watu wa Darisalama tuliteseka sana na wanawake wengi walibakwa na watu waliojifanya wana bidhaa hizo "adimu" majumbani mwao..

Wakati ule Mgambo na wenyeviti wa maduka ya Ushirika walikuwa kama ni Miungu watu. Sisi kwetu kulikuwa na mgambo aliyetembea na wake za watu alivyopenda kisa yeye ana nafasi kubwa sana ya kupata vitu kwenye duka la Kaya la Mtaani kwetu.

Hayo yote yalisababishwa na Ugomvi wa Mwalimu JK Nyerere na wakubwa wa IMF na World Bank. Umaskini ule ulitutosha hatutaki hali ile ijirudie tena kwenye kizazi hiki.

CC: Mshana Jr Pascal Mayalla
Uzi wa wakongwe tu huu
 
Kiwango kikubwa cha raia wetu hawana elimu ya zaidi ya darasa la saba,waliofanikiwa kufika elimu ya juu wana uelewa finyu sana kwenye eneo la elimu ya uraia,basics za uchumi na global affairs ambayo ni mambo ya msingi sana kwa mtu yeyote aliyefika angalau elimu ya juu pasipo kujali taaluma yake.
Brain-app kuna watu hawajui kwamba hata hiyo China tunayoiona kama ndiyo mkopeshaji wetu salama na yenyewe inakopa huko kwa mabwana wakubwa hao WB/IMF.
 
IMF na WB ni pande mbili za shilingi moja,AFDB inapata pesa zake nyingi kutoka huko huko kwa hao 'mabeberu' nchi za Scandinavian no wananchama na washirika thabiti wa WB na IMF,hivyo ulichokiandika hapa ni ugoro mtupu.
Kuhadiwa kupatiwa hiyo mikopo/misaada ni jambo moja,kupewa baada ya kutimiza vigezo na masharti ni jambo lenginie,rejea ahadi ya ule mkopo wa USD 300M kwa ajili ya elimu na wanafunzi wanaopata mimba kama umeshapatikana mpaka sasa
Mku si unajua hakuna anayekubali kufanya yasiyo na faida kwake.
Tukumbuke kila kinachozalishwa Afrika kama soko liko kwao bei hatupangi sisi Wafrika
 
Ni kweli, hakuna mtu mwenye akili anayekubali kufanya biashara au mahusiano yasio na faida kwake, muhimu ni kuangalia na sisi tunanufaikaje na kama kuna makosa yalifanyika yarekebishwe kwa utaratibu sahihi pasipo ugomvi usio na ulazima.
Katika uchumi wa soko huria duniani kote sio mzalishaji pekee anayepanga bei ya bidhaa,ni nguvu za soko na ushindani ndizo zinaamua bei ya bidhaa zako. Dhahabu inazilishwa Tanzania,Ghana, South Africa,Russia,Mali,USA n.k zote zinakutana katika soko mwenye bei ya chini na bora ndiyo inanunuliwa,vivyo hivyo kwa kahawa kutoka Tz, Uganda,Brazil, Vietnam n.k,vivyo kwa maghari kutoka US, Japan na Ulaya kuja kwetu
Mku si unajua hakuna anayekubali kufanya yasiyo na faida kwake.
Tukumbuke kila kinachozalishwa Afrika kama soko liko kwao bei hatupangi sisi Wafrika
 
Watu hawali principle mzee, watu wanahitaji mahitaji muhimu!
Hayo mambo ya Nyerere kujifanya mwanafalsafa, mwenye misimamo, eti isiyoyumba ilitusaidia nini sisi wakati wa njaa kali?
Ni nani aliyekufa njaa Tanzania.
Kuna huna unaloliamini na kulisimamia maishani mwako, wewe ni binaadam; una tofauti gani na ng'ombe au nguruwe?
Nashangaa sana kwa uelewa wako ambao nimeuona hapa JF mara kwa mara, unaweka mawazo kama hayo hapo juu!
 
Lakini kilichochangia pia uchumi kuwa mbaya siyo IMF bali ni mis-management kwenye mashirika ya umma...uzalishaji ulikuwa wa ovyo kabisa kwenye mashirika ya umma ..wanyakazi wengi kwenye mashirika lakini hawazalishi...inefficiency ilikithiri kwenye mashirika na serikalini na kadhalika na kadhalika.
Huwa hatutaki kukubali udhaifu wetu huu. Sio wakati ule tu, bali hadi sasa. Kama taifa hili ndilo tatizo letu kubwa.
 
Ni nani aliyekufa njaa Tanzania.
Kuna huna unaloliamini na kulisimamia maishani mwako, wewe ni binaadam; una tofauti gani na ng'ombe au nguruwe?
Nashangaa sana kwa uelewa wako ambao nimeuona hapa JF mara kwa mara, unaweka mawazo kama hayo hapo juu!

Hata misimamo isiyo na maana nayo ni misimamo, lakini madhara yake ni makubwa sana
 
Acha bange za mchana wewe chokoo... Washamba wenzenu wameharibu uchumi kutokana na fikira pimbi, leo unazungumzia TL kwa lipi? Kweli watu wasipokuwa na elimu wanakuwa hawana faida kwa nchi
Mwambie sasa Tundu Lisu aache ujinga anaoufanya kama kweli unamaanisha na hutak turud huko.
A
 
Back
Top Bottom