Umasikini wetu ni wa fikra sio Mali angalia hapa.

Umasikini wetu ni wa fikra sio Mali angalia hapa.

Mwanahisa

JF-Expert Member
Joined
Jun 29, 2012
Posts
1,382
Reaction score
513
Hivi majuzi taarifa ya Idadi ya watu Tanzania imetolewa na Mh. Rais, idadi hii kwa ukamilifu inasema nchi ina watu milioni 44.9 hii ni makadirio ya watu milioni 45.

Nchi ina hecta milioni 44 za aridhi inayofaa kwa kilimo, ila mpaka sasa ni asilimia 23% tu ndio imetumika yaani hecta 10.12 tu.
Hecta milioni 29 zinafaa kwa kilimo cha umwagiliaji ila ni asilimia 1% tu ndo imetumika.

Ng'ombe milioni 19, idadi inayotupa nafasi ya tatu kwa bara la Afrika.
Mbuzi na Kondoo milioni 17,
Mito na Maziwa yenye ukubwa wa kilomita za mraba 62,000.
Ukanda wa pwani ya bahari kilomita za mraba 1,424.

Ukanda maalum wa kiuchumi baharini (Exclusive Economic Zones) EEZ kilomita za mraba 223,000.

hapa sijaweka yaliyomo chini ya aridhi hii, gesi madini na mengineyo. Kutuita watu wa Tanzania maskini lazima uainishe ni umasikini wa mali au FIKRA?



Chanzo cha data hizi; tovuti ya Serikali.
 
Mfumo wa huduma muhimu kwa jamii,urasimu ndio tatizo
 
Mfumo wa huduma muhimu kwa jamii,urasimu ndio tatizo
Mifumo inafanaya kazi kulingana na wakati Mkuu, hatuwezi kukalia mfumo mmoja kwa miongo 5, dunia inasonga mbele ni ngumu kubakia tulipo. Na sisi tumeshikilia mashua inayojaa maji na itazama muda wowote.
 
Mkuu kwa kifupi Hapa Bongo hata Ungetoa Ushauri wa Aina gani ni sawa na Kutwanga maji tu, kwa kifupi ni kila mtu aone anatoka vipi na kwa wakati gani, make mambo mengine ndo kama haya,

Sisi tulisha kuwa ni watu wa kulaumu tu wakati hizo furusa zinazadisha wengine na sisi tumekomaa na biashara za Uchuzi, na kumbuka niliwahi shirki washa fulani ya kutafuta mawazo bora ya biashara kwa vijana, kwa kweli inasikitisha sana,

Ni kweli kuna Ngo'ombe, Mbuzi na mito na kila kitu, Ila Je watanzania tunafanya biashara za aina ipi? Na zani Kariakoo ni jawabu tosha, na hapa tutaanza kulaumu Serikali haijafanya hiki mara kile,

So Mkuu wewe kama Mjasirimali songa Mbele na wazo lako, kwa sababu mwisho wa siku haya Maisha yata muhusu kila mmoja na hakuna aliyepo kwa ajili ya wengine
 
Mkuu kwa kifupi Hapa Bongo hata Ungetoa Ushauri wa Aina gani ni sawa na Kutwanga maji tu, kwa kifupi ni kila mtu aone anatoka vipi na kwa wakati gani, make mambo mengine ndo kama haya,

Sisi tulisha kuwa ni watu wa kulaumu tu wakati hizo furusa zinazadisha wengine na sisi tumekomaa na biashara za Uchuzi, na kumbuka niliwahi shirki washa fulani ya kutafuta mawazo bora ya biashara kwa vijana, kwa kweli inasikitisha sana,

Ni kweli kuna Ngo'ombe, Mbuzi na mito na kila kitu, Ila Je watanzania tunafanya biashara za aina ipi? Na zani Kariakoo ni jawabu tosha, na hapa tutaanza kulaumu Serikali haijafanya hiki mara kile,

So Mkuu wewe kama Mjasirimali songa Mbele na wazo lako, kwa sababu mwisho wa siku haya Maisha yata muhusu kila mmoja na hakuna aliyepo kwa ajili ya wengine
Mkuu Chasha, ukitaka kuifanyia dunia jambo usianze kwa kuelezea jambo husika, fanya jambo ili ukifika wakati wakuelezea uwe na chakuonyesha. Experience is the best teacher. A hero dies once, coward many times.... Uchaguzi ni wa mtu binafsi.:shut-mouth:
 
Hivi majuzi taarifa ya Idadi ya watu Tanzania imetolewa na Mh. Rais, idadi hii kwa ukamilifu inasema nchi ina watu milioni 44.9 hii ni makadirio ya watu milioni 45.

Nchi ina hecta milioni 44 za aridhi inayofaa kwa kilimo, ila mpaka sasa ni asilimia 23% tu ndio imetumika yaani hecta 10.12 tu.

Hecta milioni 29 zinafaa kwa kilimo cha umwagiliaji ila ni asilimia 1% tu ndo imetumika.

Ng'ombe milioni 19, idadi inayotupa nafasi ya tatu kwa bara la Afrika.

Mbuzi na Kondoo milioni 17,

Mito na Maziwa yenye ukubwa wa kilomita za mraba 62,000.

Ukanda wa pwani ya bahari kilomita za mraba 1,424.

Ukanda maalum wa kiuchumi baharini (Exclusive Economic Zones) EEZ kilomita za mraba 223,000.

hapa sijaweka yaliyomo chini ya aridhi hii, gesi madini na mengineyo. Kutuita watu wa Tanzania maskini lazima uainishe ni umasikini wa mali au FIKRA?

Chanzo cha data hizi ni tovuti ya Serikali.

Ungehitimisha kwa ushauri wa nini kifanyike mkuu! Nafikiri huu ni wakati wa kuchukua hatua, sio bla bla tena.

Mkuu Mwanahisa, naungana nawe 100%.

Umasikini wetu ni wa FIKRA, sio MALI hata kidogo. Tukiuondoa kwanza umasikini huu wa fikra, ni rahisi kuondokana na umasikini wa kipato. Self Education / Personal Development ndio tiba SAHIHI katika kuondokana na UMASIKINI WA FIKRA, NA HATIMAYE KIPATO. Hakuna njia ya mkato zaidi ya kupenda kujisomea/ kusikiliza vitabu / machapisho au cd mbalimbali zinazungumzia maisha ya watu waliofanikiwa au kanuni za mafanikio. Hakuna mbadala.

Karibu kila mtu huwa anataka kuwa tajiri. Tatizo, wengi wetu hatupo tayari kulipa gharama (we are not ready to leave the comfort zone).

Ndugu Wanajamvi, tafuteni vitabu hivi na kuvisoma kwa kuanzia, mapema iwezekanavyo;

  1. THE CASHFLOW QUADRANT
  2. THE BUSINESS SCHOOL &
  3. THE BUSINESS OF THE 21ST CENTURY vyote vikiwa vimeandikwa na Robert T. Kiyosaki.

Vinapatikana kwenye maduka yafuatayo: Scholastic Bookshop (Mlimani City & Posta), Dar es Salaam Printers, Saramanda, n.k. Pia, kwa wauza vitabu stand ya mabasi ubungo vinapatikana.

Ninasema kwa kuanzia, kwa maana kwamba kuna vitabu vingi vizuri (sio vya Robert Kiyosaki peke yake) lakini vitabu hivi vitakusaidia kukupa mwanga zaidi juu ya Biashara na Ujasiriamali katika karne hii ya 21 katika mambo yafuatayo:

  • Tofauti (Faida na Hasara) kati ya Sole Prorietor (Small business), Limited Company (Business Owners), Wawekezaji (Investors), na Waajiliwa (Employees)
  • Utaratibu wa kodi uliopo kati ya Sole proprietor (Small busines) na Limited Company (Big Business / Corporations)
  • Fursa za mikopo zilizopo kati ya Sole proprietor (Small busines) na Limited Company (Big Business / Corporations)
  • Fursa / Uwezekano wa kukua hivyo kuajiri watu wengi zaidi na kusaidia tatizo la ukosefu wa ajira nchini, uliopo kati ya Sole proprietor (Small busines) na Limited Company (Big Business / Corporations)
  • Nafasi zilizopo ya biashara kukua vizazi hadi vizazi (business sustainability) kati ya Sole proprietor (Small busines) na Limited Company (Big Business / Corporations)
  • Nguvu ya mtandao / mfumo (kuwa na watu wanaokufanyia kazi) inayopatikana kwenye Limited Company ukilinganisha na Sole proprietor ambaye kimsingi, unakuwa ni mtumwa wa hela (working for money) kitu ambacho hakina tofauti na Kuajiriwa.
  • Namna ya kuondokana na changamoto za Usimamizi na Mitaji ya mawazo ya Biashara zetu bila kusahau Ofisi/Eneo (premisis) la kufanyia biashara na Stadi /Mbinu za Biashara.
  • Zaidi, vitakupa muongozo mzuri namna unavyoweza kuutumia muda wako wa ziada (part time) kujenga TIMU ya watu watakaokuwa wanakufanyia kazi (SYSTEM/ NETWORK) kama ambavyo Bakheresa, Mengi, Manji, Bill Gates, Donald Trump, n.k walivyo na wanavyoendelea kufanya.


Kwa mawasiliano zaidi, piga 0713 366 473 au 0767 277 223.

So, Mkuu John L. Mihambo, CHUKUA HATUA.

KILA LA KHERI WAKUU.
 
Back
Top Bottom