Umati mikutano ya wadhamini wa Tundu Lissu inaitangaza Tanzania kimataifa, watalii njooni Tanzania hakuna corona

Umati mikutano ya wadhamini wa Tundu Lissu inaitangaza Tanzania kimataifa, watalii njooni Tanzania hakuna corona

JERRY

JF-Expert Member
Joined
Feb 18, 2009
Posts
630
Reaction score
502
Tangu aanze kuzunguka kutafuta wadhamini Tundu Lissu amekuwa akipokewa na umati mkubwa sana wa watu tena hawajavaa hata mabarakoa.

Vyombo vya habari vya nje mnaofuatilia harakati za Tundu Lissu kusaka Urais wasiishie tu kutaka kumhoji Lissu bali pia watende haki kwa kuutangazia ulimwengu kwamba Tanzania hakuna corona na kuwahimiza raia wa huko kuja kuona maajabu ya Tanzania.

Ila na Tundu Lissu unapomwaga sera zako ongea yote tunaweza kukuelewa ila hili la CORONA usijaribu kumsema JPM kiukweli mimi binafsi sitakuelewa hata kwa asilimia 200% maana kwa namna JPM alivoli handle kwa busara ya hali ya juu na kwa kumtanguliza Mungu anastahili pongezi kubwa.
 
Na angesema bado kuna corona kwa dalili za umati ambao unampokea Lissu na Maalim Seif angeahirisha uchaguzi angalau akae madarakani hata mwaka mwingine moja! Ataungana na Trump mitaani.
 
mkuu kama huijui corona fuatilia yaliyotokea Italy, Tanzania ushayaona hayo? kama si Mungu alietuepusha baada ya KUMUOMBA atuondolee janga hili
Tunajiendea tu ila Corona siyo upepo kusema unapita na kujiendea zake!
 
JERRY,

Naunga mkono hoja, Kama sio Raisi Magufuli kuongozwa na hekima ya MUNGU juu ya hili janga Tanzania ingekuwa habari nyingine; Naweza kuamini kuwa Magufuli aliletwa na Bwana Mungu wa majeshi kusudi atuvushe ktk hali Ngumu za majanga mbalimbali na yeye pekee ndiye aliyemteua kuweka Hekima ndani yake.

Kama tangu hapo awali watu wa Dini mbalimbali kila mahala Tanzania waliomba kwaajiliyake Mungu amtumie kwa makusudi yake, Tuendelee kumuombea Hekima ya Roho Mtakatifu isipunguke juu yake na amtumie kutuvusha kwa mengi hatujui mbele kuna nn, Mungu pekee ndio ajuaye.
 
JERRY,

We umati mkubwa umeuona wapi wakati luninga hazionyeshi hayo unayosema?
Utakuwa mzushi wewe!
 
Back
Top Bottom