Wacha1
JF-Expert Member
- Dec 21, 2009
- 16,681
- 8,241
Hii ni Taarifa kutoka kwa John Mrema ambaye ni mkurugenzi wa Itifaki wa Chadema, Ikumbukwe kwamba Chadema iliweka utaratibu kwa wanachama wake wote wanaotaka kugombea nafasi hizi kujitokeza mapema kutia nia kwenye chama chao ili usaili ( Vetting ) juu yao uanze mapema, lengo likiwa ni kutoa nafasi kwa viongozi kuwafahamu kiundani Wagombea hawa kabla ya kuwapa nafasi za kugombea.
Nafasi zote za ubunge na udiwani kwenye majimbo na kata zote nchi nzima, hakuna mtia nia ambaye yuko peke yake, yako majimbo ambayo kuna watia nia ya ubunge kuanzia watatu hadi watano!
Kwa aina ya siasa za Tanzania za sasa Umati huu wa watia nia wa Chadema una maana gani?
# TUENDELEE KUNAWA MIKONO ILI KUJIKINGA NA VIRUSI VYA CORONA .
Kwa hiyo John Mrema kakufuata wewe na kukupa hizi taarifa na wewe umeona uweke hapa JF? Je, nitakuwa namekosea nikisema wewe ndio John Mrema? Je, nitakuwa nimekosea nikisema JF imenunuliwa kihalali na Chadema? Je, nitakuwa nimekosea nikisema kwamba hiyo ndio sababu kubwa michango na thread nyingi huhamishwa kwa maelekezo ya John Mrema?