Umbea na Kiherehere cha Kutangaza kuwa MO anajiondoa Simba wamtokea puani Mchambuzi Mnafiki Shaffih Dauda wa CMG

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Kama kawaida yake mara nyingi amekuwa ni Mtu mwenye Chuki za waziwazi dhidi ya Simba SC baada ya Kunyimwa Ulaji wa Kuwa Msemaji wake leo hii Mchambuzi Mnafiki na Mtangazaji wa hovyo hovyo kutoka CMG Shaffih Kajuna Dauda amezusha kuwa Mohammed Dewji anajiondoa Simba SC kama Mwekezaji taarifa ambayo Tajiri mwenyewe MO Dewji ameikanusha na amesikitika mno.

Sasa imetosha Uongozi wa Simba Umshtaki Shaffih Dauda ili akome na ajifunze.
 
Wewe ni msemaji wake?
 
Kwa nn wamshitaki kama ni uongo si waachane nae tu!? Hili suala limewatisha sana eti?
 
Tunaomba utupe source ya Mo kukanusha either kwa video au post yoyote
 
Nikajua tayari ishatokea puani kumbe hata mguuni bado [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hilo kanusho la Mo kalitolea kwenye platform ipi?
 
Hapo anawesema akina Kilomoni
 
Acha wafu wazikane,Dauda ni mwanamsimbazi mwenzenu, ila kumbukeni mficha maradhi kifo humuumbua

Tokea atoswe nafasi ya Usemaji wa Simba SC aliyokuwa akiitaka na hadi leo anaitaka mno tu amekuwa ni Mtu mwenye Chuki zaidi na Simba SC na Kuizushia mambo mengi tu na nadhani kwa sasa Uvumilivu Kwake unaelekea Kufikia Ukingoni na asije akawalaumu Wana Msimbazi kwa Maamuzi yao watakayoamua Kuchukua ambayo yatakuwa ni ya Kisela zaidi.
 
Watu aina ya Shafii ni Wapiga deal tu kupitia soka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…