utopolo og
JF-Expert Member
- Nov 29, 2022
- 575
- 1,575
Baada ya kuwakanda Simba S.C katika mchezo uliopita wa ligi ya NBC, mabingwa watetezi na vinara wa ligi kuu, Yanga Afrika leo tena watashuka dimbani mida ya saa 10 kamili jioni kuzisaka point tatu dhidi ya Jkt Tanzania.
Ikumbumbwe katika mchezo wa raundi ya kwanza, Yanga ilipata ushindi wa 5-0, hivyo Jkt wataingia wakiwa na shauku ya kulipa kisasi.
Mchezo utapigwa katika dimba la Meja Jenerali Isamuhyo huko mbweni nje kidogo ya jiji la Dar es salaam na utaanza saa 10 kamili jioni.
Usikae mbali.
=====
UPDATES:
=====
PWANI: Mchezo wa Ligi Kuu Bara kati ya JKT Tanzania dhidi ya #YangaSC uliokuwa uchezwe kwenye Uwanja wa Meja Jen. Isamuhyo Mkoani Pwani, leo Aprili 23, 2024, umeahirishwa kutokana na uwanja kujaa maji.
Taarifa ya Kamishna wa Mchezo huo, Kamwanga Tambwe imeeleza kuwa maamuzi ya mchezo huo utachezwa linin a wapi yatatangazwa baadaye na Bodi ya Ligi Kuu.
Yanga inaongoza Ligi ikiwa na pointi 58 katika michezo 22, JKT ina pointi 22 katika michezo 22 na ipo nafasi ya pili kutoka mwisho kwenye msimamo (nafasi ya 15).
Ikumbumbwe katika mchezo wa raundi ya kwanza, Yanga ilipata ushindi wa 5-0, hivyo Jkt wataingia wakiwa na shauku ya kulipa kisasi.
Mchezo utapigwa katika dimba la Meja Jenerali Isamuhyo huko mbweni nje kidogo ya jiji la Dar es salaam na utaanza saa 10 kamili jioni.
Usikae mbali.
UPDATES:
=====
PWANI: Mchezo wa Ligi Kuu Bara kati ya JKT Tanzania dhidi ya #YangaSC uliokuwa uchezwe kwenye Uwanja wa Meja Jen. Isamuhyo Mkoani Pwani, leo Aprili 23, 2024, umeahirishwa kutokana na uwanja kujaa maji.
Taarifa ya Kamishna wa Mchezo huo, Kamwanga Tambwe imeeleza kuwa maamuzi ya mchezo huo utachezwa linin a wapi yatatangazwa baadaye na Bodi ya Ligi Kuu.
Yanga inaongoza Ligi ikiwa na pointi 58 katika michezo 22, JKT ina pointi 22 katika michezo 22 na ipo nafasi ya pili kutoka mwisho kwenye msimamo (nafasi ya 15).