Umekosea Prof. Adolf Mkenda: Utendaji mzuri popote sio haki

Umekosea Prof. Adolf Mkenda: Utendaji mzuri popote sio haki

Kamundu

Platinum Member
Joined
Nov 22, 2006
Posts
7,823
Reaction score
10,857
Hakuna jamii yeyote Duniani ambayo kuna usawa kwenye kila kitu. Hata hapa Marekani watoto wa George H Bush wamekuwa maarufu na kuwa Governors na mmoja Raisi kwasababu babu yao alikuwa tajiri, baba akawa tajiri akaweza kuwasomesha shule nzuri sana na kuwapa elimu bora. Hii haina maana kwamba hawa watoto ambao wamekuja kuwa Maraisi wanavipaji kuliko wengine lakini wameweza kupata fursa ambazo ni ngumu kupata mtoto wa masikini.

Hii hipo sehemu nyingi sana. Yule mtoto wa Kikwete ingewezekana asiwe lawyer kama angezaliwa Mtwara vijijini kwa familia masikini lakini haibadilishi ukweli kwamba mtoto wa Kikwete kamaliza Chuo Kikuu cha Dar law school. Na kwakutumia hili huwezi kusema mtoto wa Kikwete ambaye kamsomesha ni sawa tu na yule ambaye hajapata elimu kijijini kwasababu wana vipaji vya kuzaliwa sawa!

Kwa namna hii huwezi kuacha kutangaza shule na matokeo kwasababu tu wanafunzi wengi wa shule hizo na walimu wanapitia magumu sana kulinganisha na wengine.

Mimi mfano nilisoma Ilboru O-level wakati tulivyokuwa Ilboru watoto wa kutoka Arusha School walikuwa wanatuzidi mwanzoni kwasababu ya mazingira yao lakini sisi tuliongeza jitihada na kulingana na hata kuwapita. Huwezi kutumia kisingizio hiki kuacha kutangaza ukweli. Sasa ina maana tutaanza kupeleka watoto kusoma Udaktari ambao hawajafaulu? Au kuendesha ndege ambao hawajafaulu kwasababu kama hizi?

Wabunge wamekuwa kama vilaza anadanganya eti utaratibu wa kupima na mitihani haupo popote. Si kweli. Shule zinapimwa na mitihani hapa USA ndiyo hivyo. Sasa tutaanza kupima watu kwa background! huu ni uongo.

 
Huko Marekani wana utaratibu huo wa kutangaza Shule kutoka ya kwanza mpaka ya mwisho?
Yes, lakini shule zetu zinaenda kwa majimbo. Mimi kama mlipa kodi nataka kujua shule ya hapa kwangu ina matokeo gani. Watu wengi sana wanahamia sehemu kutokana na uzuri wa shule
 
Kwamba ubora wa Shule lazima utangazwe na Serikali?
 
Nakukatalia mawazo na mitazamo yako,kwa mifano tafuta,shule zilizofutiwa matokeo na kukatazwa kuba vituo vya kufanyia mitihani, kwa utafiti wangu mdogo ni yenye majina mazuri mazuri, yenye kushawishi na kuvutia kwa maana ya ubora wa kazi au huduma wanazotoa,iwe kibiashara au wanachokiita coincidence 🤔
 
Hakuna jamii yeyote Duniani ambayo kuna usawa kwenye kila kitu. Hata hapa Marekani watoto wa George H Bush wamekuwa maarufu...
Nyie ndio wale walikuwa wanaleta ubaguzi kwenye Elimu kwa kuchagua wanafunzi bora tu ili mradi shule ionekana inafanya vizuri .Shame on YOU
 
Hawana, huyo ni mungo mkubwa, amending uongo na upotoshaji mwingine sana kwenye huu uzi.
Huko Marekani wana utaratibu huo wa kutangaza Shule kutoka ya kwanza mpaka ya mwisho????
 
Yes lakini shule zetu zinaenda kwa majimbo. Mimi kama mlipa kodi nataka kujua shule ya hapa kwangu inamatokeo gani. Watu wengi sana wanahamia sehemu kutokana na uzuri wa shule
Kwa ukipitia matokea yaliyangazwa na serikali si unaweza ona performance ya shule yako au?
 
Prof.Mkenda huwa anafanya mambo mengi kwa akili sana na kutoa hoja zenye mashiko.
Prof. Mkenda ni waziri mwenye IQ kubwa sana, pengine ndio waziri sahihi zaidi kuwahi kutokea kwenye hii Wizara​
 
Nyie ndio wale walikuwa wanaleta ubaguzi kwenye Elimu kwa kuchagua wanafunzi bora tu ili mradi shule ionekana inafanya vizuri .Shame on YOU

Kama umefeli kwasababu umetokea familia masikini na ulikuwa huna vitabu ni jambo baya. Lakini hili haina maana kwamba mimi niliyetokea familia yenye uwezo sijafaulu!

Hawa wanasiasa wenyewe ni kwanini wanapeleka watoto wao Fedha na sio shule za kata kama matokeo ni yaleyale
 
Mifano yako yote uliyotoa hata haiendani na suala la Matokeo ya shule na wanafunzi kupangwa kuanzia namba moja mpaka mwisho kitaifa. Ni upupu mtupu umeandika hapa.
Hakuna jamii yeyote Duniani ambayo kuna usawa kwenye kila kitu. Hata hapa Marekani watoto wa George H Bush wamekuwa maarufu na kuwa Governors na mmoja Raisi kwasababu babu yao alikuwa tajiri, baba akawa tajiri akaweza kuwasomesha...
 
Kwa ukipitia matokea yaliyangazwa na serikali si unaweza ona performance ya shule yako au?

Kama ni hivyo kuna shida gani kusema ukweli badala ya kuweka siasa kwenye elimu. Hakuna njia fupi kwenye elimu ni lazima kuwe na viwango
 
Matokeo ya shule zote yapo mtandaoni, wewe huelewei hata ni kitu gani unataka.
Yes lakini shule zetu zinaenda kwa majimbo. Mimi kama mlipa kodi nataka kujua shule ya hapa kwangu inamatokeo gani. Watu wengi sana wanahamia sehemu kutokana na uzuri wa shule
 
Hakuna kitu kama hicho
Mnaongea vitu ambavyo hamfahamu. Mimi niko hapa ni shule zote kuanzia miaka 7 mpaka 18 Grade 2 mpaka 12 kuna mitihani. Kuna mpaka mitihani ya kuingia vyuo
 
Hakuna jamii yeyote Duniani ambayo kuna usawa kwenye kila kitu. Hata hapa Marekani watoto wa George H Bush wamekuwa maarufu na kuwa...
Ni kweli. Nazani ni kazi ya Serikali kuhakikisha kwamba mazingira ya shule zake yanakuwa bora kwa walimu na wanafunzi sawa sawa na hizo shule zinazofaulisha
 
Back
Top Bottom