Umekula tunda gani leo?

Nimesomaa, mwishoni nimetafuna ndizi... Shukrani kwa andiko hili
 
Suala la Afya bora ni suala la muhimu sana katika Maisha ya kila mmoja wetu na taifa kwa ujumla. Bila afya hakuna furaha,amani wa shughuli yoyote ile ya maendeleo.Afya ndio msingi wa maisha yetu ya kila siku.Siku hizi si ajabu sana kusikia au hata kushuhudia watu wengi wakisumbuliwa na matatizo mengi sana ya kiafya, suala hili linachangiwa na mambo mengi hali ya mazingira au tabia za watu.

Upuziaji wa matumizi ya matunda na mboga mboga unachangia kwa kiasi kikubwa matatizo ya mengi ya kiafya. Matunda ni moja ya zawadi kutoka kwa Mwenyezi Mungu binadamu tuliopewa japo tunaidharau licha ya faida yake katika maisha yetu.

Kuna sababu kadhaa za kwa nini watu hawatumii matunda mara kwa mara , baadhi ya hizo ni Kutokujua faida ya matunda kiafya, na Ukosefu wa uwezo wa kumudu gharama za kula matunda mara kwa mara. Ikiwa wewe ni miongoni mwa watu wanaoshindwa kutumia matunda kwa moja ya sababu hizi basi taarifa hii inakuhusu na uyajue matunda yenye gharama nafuu sana wakati huo huo yakiwa na faida tele kiafya kwa mwili wako.

#1.

MACHUNGWA


grapefruit

Haya ni matunda matamu sana ,rahisi sana kupatikana na yenye faida nyingi mno kwa afya yako.Matunda hayab hupatikana kwa wingi bila gharama kubwa mfano kwa wale waliofika Morogoro na Tanga wanajua uwingi wa matunda haya. kama hujui tazama virutubisho muhimu sana viliyomo katika machungwa.

Vitamin C __________________ 93%
Fiber __________________ 13%
vitamini B1 __________________ 9%
Pottasium __________________ 7%
Calcium ___________________ 5%
Na virutubisho vingine vingi sana huku vikiwa na faida muhimu zaidi ikiwemo:

Vitamic C ya machungwa husaidia kuimarisha ulinzi wa Antioxidant na ulinzi dhidi ya magonjwa
Machungwa husaidia kuzuia ugonjwa wa mawe katika figo(kidney stones)
Machungwa huzuia kansa na vidonda vya tumbo
Machungwa husaidia na kuboresha afya ya mfumo wa upumuaji.
Yapo mengi na faida nyingi sana za machungwa …Machungwa sio gharama ,ni rahisi kupatikana yatumie mara kwa mara uone faida yake kwa afya yako.

#2.

NANASI


pineapple.jpg

Nanasi ni tunda maarufu na linalopatikana karibu maeneo yote kwa urahisi.Tunda hili lina virutubisho vya kusaidia ubora wa afya yako.Baadhi ya faida ya nanasi ni;

Husaidia kwa kiasi kikubwa ulinzi wa mwili.
Husaidia seli na tishu mwilini kwa vitamini c iliyomo katika tunda hili suala linalopelekea kujengwa kwa sehemu muhimu ya protini iitwayo COLLAGEN ambayo huimarisha mishipa ya damu,ulinzi wa ngozi,ogani na mifupa mwilini.
Husaidia sana kukukinga na kansa kwa kuupatia mwili wako vitamini A na C zenye uwezo mkubwa wa kupambana na kansa mwilini.
Nanasi ni tunda lenye faida kubwa sana mwilini mwako hizo ni chache kati ya nyingi, hivyo tumia fursa ya gharama ndogo ya matunda haya kwa faida ya afya yako.

#3.

PARACHICHI


avocado.jpg

Parachichi ni tunda rahisi sana kupatikana hasa sehemu za baridi. Watu wanaoishi maeneo haya wana ushahidi juu ya hili.Huuzwa nchi nzima kwa bei ndogo na ya kawaida kabisa huku likiwa na faida kubwa sana kiafya.Baadhi ya virutubisho muhimu vinavyopatikana kwenye tunda hili ni;

Vitamini K __________ 26%
Folate __________ 20%
Vitamini C __________ 17%
Potassium __________ 14%
Vitamin E __________ 14%
Vitamin B5 __________ 14%
Vitamin B6 __________ 13%
Kwa orodha ya virutubisho hivyo hapo juu Parachichi litasaidia sana mwili wako kurekebisha msukumo wa damu, Tunda hili lina 77% ya protini kitu kinachofanya tunda hili liwe mmea wenye protini kuliko mwingine wowote ule.Husaidia macho kuona vizuri zaidi, zaidi husaidia nywere na ngozi yako, Na faida nyingine nyingi sana.Hauna budi kutumia parachichi mara kwa mara.

#4.

PAPAI


paw-paw

Papai ni moja ya tunda zuri,tamu likiwa vilevile linapatikana kwa urahisi na gharama nafuu.Kama ulikuwa hujui faida za papai kwa afya yako ngoja nikuibie siri. Papai ndio tunda lenye utajiri wa madini mengi sana ukilinganisha na matunda mengine pamoja na virutubisho vingine vingi.Baadhi ya faida za tunda hili ni kama vile;.

Husaidia sana kupunguza uzito (weight loss), Ikiwa kila nusu kipande kikiwa na Calories 120.Tunda hili ni la muhimu sana kwenye suala la kupunguza uzito …kama unashida ya uzito usiotakiwa tumia tunda hili mara kwa mara litakusaidia sana.
Husaidia sana kinga ya mwili kwa zaidi ya 200%.Utajiri wa Vitamini C papai lililonao husaidia kinga ya mwili kuwa imara pindi unapotumia mara kwa mara.
Ni tunda nzuri kwa wagonjwa wa kisukari.Papai lina kiwango kidogo cha sukari(8.3 gram kwenye kikombe cha papai zilizokatwakatwa vipande vidogo).Juisi yake ni nzuri sana kwa sukari huku ikiwa na Vitamini nyingi zenye kusaidia mgonjwa wa sukari kuepukana na magonjwa ya Moyo.
Faida za papai ni nyingi sana ,Husaidia kurainisha na kurinda ngozi,husaidia macho kuona vizuri,huasidia mfumo wa usagwaji wa chakula mwilini n.k, hivyo litumie mara kwa mara.





#5.

EMBE


mango

mangos

Tunda hili ni maarufu na rahisi sana upatikanaji wake huku likiwa na bei ya kawaida sana.Maeneo kama ya mubende, kampala, Tommy, kent,mashamba ya Capsicum ,Embu ishiara ,karurumo,Tabora, Tanga, Morogoro, Kigoma, na maeneo mengine mengi sana ya Afrika mashariki, tunda hili hulimwa na kustawi kwa wingi sana. Licha ya hilo bado watu wanapuuza kutumia tunda hili kiafya, Ila wewe unatakiwa ujue faida za tunda hili mfano,

Linasafisha ngozi, linaimarisha sana afya ya macho.
Lina virutubisho venye Antixiodant vinavyosaidia kukukinga na kansa kwenye mwili wako.
Hongeza hamu ya tendo la ndoa na nguvu za kiume.
Kubwa zaidi hukuepusha na ugonjwa wa mshituko wa moyo (heart stroke)
Ni baadhi ya faida chache na muhimu sana kwa ajiri ya mwili wako …. Jenga mazoea ya kula maembe kwenye milo yako na ufurahie afya bora.



#6.

NDIZI


banana.jpgNdizi ni tunda maarufu sana lenye faida tele kwa mwili wako huku likipatikana kwa gharama ndogo na kwa urahisi. Ndizi ina virutubisho vingi venyefaida nyingi sana kwa afya yako ikiwemo.

Potassium ______________ 9%
Vitamin B6 ______________ 33%
Vitamin C ______________ 11%
Protein _______________ 1.3 grams
Fat _______________ 0.4 grams
Na vingine vingi sana kiasi cha kutotaja vyote huku vikiwa na faida kwa mwili wako kama vile,

Kurekebisha kiasi cha sukari mwilini (ndizi ina Kalories 105 pekee).
Inapunguza uzito usiotakiwa (weight loss).
Potassium iliyopo kwenye ndizi Inaboresha afya ya moyo.
Husaidia Insulin na figo kufanya kazi vizuri .
Na faida zingine nyingi sana hupatikana kwa kutumia ndizi mara kwa mara.



#7.

TIKITI MAJI



Tikiti maji naamini ni tunda linalofahamika na watu wengi sana ,Tunda hili licha ya watu wengi kutokujua lakini lina faida nyingi mno kiasi cha kushauriwa kutumika mara kwa mara na wadau mbalimbali wa masuala ya afya. Hizi ni baadhi ya faida muhimu sana za tunda hili

Pamoja na tikiti maji kuwa tamu kwa ladha lakini tunda lina Karolies chache sana (105 Calories), wakati huo huo 92% ya tunda hili ni maji. Kitu hiki kina faida mno kiwenye mwili wako hasa baadhi kazi zile ambazo maji hufanya mwiulini hufanywa na tunda hili.Fibers na Maji ya tunda hili hukupa afya bora wakati huo huo likiwa na calories.
Lina vitamin C , Vitamini A, Vitamin B1, Vitamin B5, Vitamin B6 na virutubisho vingine vingi vyenye faida nyingi sana kama vile , kukukinga na kasa, kuboresha afya ya moyo,Ni tunda zuri sana kwa afya ya ngozi na nywere n.k .
Litumie mara kwa mara uone faida hizi kwenye mwili wako.

#8.

PASSION





Matunda sio tu mazuri kwa harufu nzuri sana yaliyonayo.LA hasha !!!! Tunda hili linafaida kubwa sana kiafya .Tunda hili lina viritubisho muhimu sana kwa afya ya mwili wako mfano,

Energy ____________ 97 kcal
kabohydrate ____________ 23.38 grams
protini ____________ 2.2 grams
Vitamin A ____________ 1274 IU
Magnesium ____________ 29 grams
Madini chuma ____________ 1.6 Milligramu
Na virutubisho vingine vingi sana vinavyokulinda na kansa, shinikizo la damu na shmbulio la moyo, magonjwa ya macho, Anemia, Ulinzi wa mwili dhidi ya magonjwa na matatizo mengine mengi ya kiafya. USIPUZIE tunda hili lina faida sna kwa mwili wako.



#9.

MAPEAZI



Matunda matamu sana na yenye faida kubwa sana kwenye mwili wa binadamu.Tunda hili lina vurutubisho muhimu sana kwa afya kama ifuatavyo;

Fiber ________________ 23%
Copper ________________ 17%
Vitamin C ________________ 10%
Vitamin K ________________ 9%
Takwimu hizi kwa mujibu wa Orodha ya mfumo wa ubora wa vyakula yaani Food Rating System Chart huonyesha matunda haya kuwa %DV ikimanisha kuwa peazi ndio tunda lenye uwiano sahihi sana wa virutubisho kuliko matunda mengine.

Matunda haya husaidia sana mwili wa binadamu kuepukana na magonjwa ya moyo na sukari, Hupunguza hatari ya kupata kansa, na faida nyingine nyingi sana kiafya.

JE WAJUA ?!……… Kwa mujibu wa Shirika la Marekani la udhibiti wa magonjwa U.S Center for diseases control Peazi ndio tunda lenye mzio mdogo kuliko mengine (most low allergy fruit). Unasubiri lini wakati ushafahamu faida ya tunda hili ?! fanya kulitumia walau hata mara kadhaa kwa kila mwezi, Naongea hivi kwa sababu matunda haya hupatikana kwa wingi katika sehemu na sehemu lakini hii haimanishi kwamba hayapatikani.



#10.

TANGO



Hili ni tunda (Cucumber) sio mtandao maarufu wa kijamii wa “Tango meesenger”. Tunda hili lina faida nyingi mno kuliko unavyoweza kufikiria ! Hebu tazama baaadhi yake >>>

Hulinda ubongo ,Tango lina kirutubisho kinachoitwa Fisetin ambacho huupa ubongo afya bora sana, kwa kukusaidia kutunza kumbukumbu,na kuzidisha uhai wa seli mbalimbali kwenye ubongo.
Linakulinda na hatari ya kupata kansa, Tunda hili lina Kirutubisho kinachoitwa Lignans ambacho huweza kukusaidia kuepuka kansa ya maziwa, kibofu, via vya uzazi, vilevile Cucurbitacin ni kirutubisho muhimu sana kwa ulinzi dhidi ya kansa.
Hukupa usafi wa kinywa na hewa toka mdomoni na ulinzi wa kinywa na meno, Tunda hili linao uwezo mkubwa sana wa kuua bakteria wanaosababisha harufu mbaya ya kinywa na magonjwa ya meno.Hivyo hukuepusha na hatari za bakteria hatari kwa kinywa na meno yako.
Huwafaa sana wagonjwa wa kisukari.Tango likiwa ni tunda lenye Kalories chacche sana (calories 16 kwa kikombe cha vipande vidogo vidogo)….Hii ni habari njema sana kwa wagonjwa wa sukari kufaidi faida mbalimbali za kiafya zinazotokana na tunda hili bila hofu yoyote ya kupanda au kushuka kwa sukari.
Hizi ni baadhi ya faida nyingi za tunda hili ambalo sio adimu ukiamua kulitafuta utalipata kwa urahisi na gharama nafuu ya kuridhisha.Rafiki yangu usipuzie ni muhimu sana kuzingatia faida zake kiafya.

KWA FAIDA YAKO :

MATUNDA NI CHAKULA KITAMU, CHA GHARAMA NAFUU, RAHISI SANA KUPATIKANA. MUNGU ALIWAPATIA BINADAMU MATUNDA KAMA DAWA NA CHAKULA CHAO . NANASI MACHUGWA PAPAI PARACHICHI NDIZI TIKITIMAJI na mengine mengi sana husaidia mno kujenga na kulinda afya ya mwili wako , zingatia haya utaishi kwa afya njema.
 
Mimi kila siku lazima nile kachumbali...karoti na hoho na tangawizi ndani...ni sawa?
 
Bado sija amka maana leo ni wikendi,
Nime kula tu tunda kwa mke wangu natural

HAYO ARTIFICIAL TUNDA ngoja ntaendea gengeni....

Sent from my SM-J700H using JamiiForums mobile app
 
Na bet huu Uzi baadae utabadilika uwe wa kugegedana kimapenzi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…