Umeniharibia maisha! ...what?

Mbu unantaka mimi lakini we mwanaume!!
lol yaani hiyo ya mwisho hapo inahuu kabisa. Duh umenikumbusha mbali sana enzi hizoooo nlishanuniwa na shoga yangu mie, yaani alikuwa kila tukimwalika tutoke naye nakwambia anakubali kalini mkifika tu anaanza nuino hilooo ukimwulza mara oh kichwa chauma, mara ah sijisikii vema almradi visa.......ila toka kidogo tu wende maliwato ukirudi unamkuta anajichekesha .........ah dada yule sitomsahau kwa vituko!! mwee............ I hope shes happy huko aliko!!

ila nafikir ni ile hali ya kuwa anampenda yeye lakini kwa vile anashindwa ku'mwambia' basi analiachia gurudumu likenda kwa mwingine ndo urafiki unakufa!
 
Mkuu ODM hivi maisha yanaharibika vp?
 

Babu
M ndo nilikuwa nataka kumjengea maisha mjukuu wako, lakin yeye naona anataka kuniharibia
Ila hii mada ya Mhe. Mbu Maralia-less. Mbunge wa MMU Magharibi na M/Kiti wa Bunge wa Kamati ya Mahusiano imenifanya nigundue kwamba hakuna kitu kinachoitwa UMENIHARIBIA MAISHA kwa mahusiano tu (kabla ya ndoa) bali kuna KUJIHARIBIA MAISHA.
 
Bado hamjaanza maofu topiki?

Ngoja nisepe tena....ila mkiwaona Mbu, MTM na Klorokwini waambieni vita yetu bado haijaisha....

Wameniharibia maisha!
Hahhahah Bab...................oh samahani Asprin mie ctaki kucheka bana..eti ulibwenge makwenzi!! wapo mbona??
 
Nimejitahidi kufuatilia michango mbalimbali.

Mie ningependa niangalie mada hii katika upeo huu: mapenzi kabla ya ndoa na baada ya ndoa ( NB: kwa wale wanaoamini katika mapenzi katika ndoa):

1. Kama uko katika ndoa, nadhani ni sahihi kufikiria kwamba mwingine amekuharibia maisha. Kumbuka kwenye ndoa maana yake mtu anakuwa ametoa moyo wake, akili yake, na hata resources zake katika kufanikisha ndoto zao za maisha. Kwa hiyo sababu yeyote ( ya msingi au siyo msingi), mara nyingi inapelekea athari kwa mwingine. Labda ni mwanamke au mwanaume ameamua kumkimbia mumewe/mkewe na kumuachia watoto, uleaji unaweza ukawa mgumu, na kama uchumi haukuwa mzuri, basi mambo yanaharibika kabisa;
Pia inategemea na umri wa wanandoa. Kuna umri mwingine ndo maisha yanaweza kuwa mabaya kabisa (especially kwa wanawake kwenye 40s, 50s)

2. Kama ni mapenzi ya kawaida partners, au boyfriend girlfriend - mtu anaweza kulalamika kupotezeewa muda. Lakini pia kigezo cha umri pia kinaweza kuingia hapo;
Nafikiri pia mleta mada ulikuwa umeijenga hoja hako kulingana na mapenzi ya aina hii. Waswahili wanasema mapenzi ni kama upofu. Mimi na wewe ni mashahidi ya jinsi mapenzi yanavyotengeneza waathirika kila siku. Hapa tunaweza kujadili kinadharia (theoritically) lakini kiuhalisia si rahisi kutenganisha kuharibiwa maisha na kupotezewa muda.

Hii imechangiwa na sababu za kibailojia kwa upande mwingine. Kwa wanawake/wasichana wanapokuwa kuwa kwenye mapenzi huwa wanatengeneza mahusiano (connection, nimekosa kiswahili kizuri), yaani wanakuwa attached in emotionally kuliko wanaume. Ndo maana mara nyingi wamekuwa waathirika, na wataendelea kuwa waathirika kadiri wanavyodondokea kwenye mikono ya wajanja.

Kikubwa ni jinsi ya kuepuka kudondokea kwenye mikono ya wanyang'anyi ili kuepuka kuona kwamba 'umeharibiwa' maisha:
a) Jitahidi kumjua mtu kwa undani zaidi kabla mapenzi hayajafika mbali - ni kweli hisia za mvuto zinaweza kuwa kubwa (kwa kisingizio cha love at first sight) na hii ndo imetengeneza waathirika wengi (kwa mtazamo wangu)
b) Kujaribu kuyajua mahitaji - wengi hapa wanakuwa na shida za kimwili ( tamaa, umaskini) au elimu n.k : Point ni kwamba; kutoruhusu mahitaji yatuzidi akili na uwezo wa kuamua kama jambo ni sahihi au sio sahihi kwa wakati huo
c)
d)
e)

....baadaye

Kwa kifupi hayo ndo maoni yangu
 
Nyie watu hapo juu:

Hakuna mtu anayeharibiwa maisha na mtyu mwingine.

Mtu hujiharibia maisha mwenyewe bana!
Ndo maaana mi bado komfusdi hapa? hivi kuharibiwa maisha ni kuto kuolewa au kuoa?
 

...dah, hapo kwenye Abortion, imagine inakataa halafu kizazi nacho kinaharibika!
kila mkitu kinafall pale pale kwenye utambuzi, uchaguzi na maamuzi.

Akikubalii >> sex >> mimba >> abortion >> kukosa yote!
in reverse order;
kukosa yote >> abortion>> mimba >> sex >> asipokubali hapotezi lolote!


CPU ha ha ha!,

....pole sana bana. Unahitajika kurudia kusoma tena michango humu tangia mwanzo.
Kumbe bado una matumaini nae? Hongera sana bana, ...ila nadhani unapenda mpaka chongo unaita kengeza.
Hapo ulipo ume "pause" maisha yako ukiombea maajabu binti awasiliane nawe muanze upya!

Well, sitaingilia sana, "kitanda usichokilalia!...." ila kwa tahadhari tu nakukumbushia maamuzi yako yatokane na
utambuzi wa "Warning & Alarm bells" zote unazozisikia tangu mwanzoni mwa mahusiano yenu....kisha uchambue na kuchagua >>>uamuzi<<< ulio sahihi kwa maisha yako.
Kinyume na hapo utajiharibia maisha yako.


lol, maisha haya, kwani kuna wa kuwapeleka skul kwenye hiyo familia au ni watu wazima wanahitaji msaada wako kwa namna moja au nyingine? sema mdada nae alilielezea vibaya.

Mtihani huo! Mambo ya Extended families!
 

okay pole sana Nyamayao my dear...sasa walau UMEJUA kwamba ungekuwa umefanya jambo la kipumbavu sana aisee...
 

I can see clearly now - Jimmy Cliff
 
Reactions: Mbu
okay pole sana Nyamayao my dear...sasa walau UMEJUA kwamba ungekuwa umefanya jambo la kipumbavu sana aisee...

asante sana Kaizer, zaidi ya upumbavu swir...cjui ingekuwaje mackini.
 
Reactions: Mbu

ha ha ha, nyamayao bana...uliishi miezi tisa tumboni mwa mama yako, ukaishi miaka nenda rudi mpaka ulipokutana na huyo prince charming,...iweje uone maisha hayakuwa na thamani tena? huu UGONJWA MAPENZI NI BALAA...

Hebu leo miaka kadhaa ishapita jaribu kurudisha hisia zako siku ile ulipojiona maisha hayana thamani tena, kwanini ulifikiria hivyo?


ha ha ha, Mwj1 nimekugusa ndipo eeh? ha ha ha!

&#9835; na bado, na bado, sijafika mwisho! &#9835;
Nalia kwa furaha - Bushoke ft Klynn


Tupo Ukurasa mmoja CPU,...endelea kusikiliza na kuheshimu senses zote za mwilini mwako!
Kuna wanaozifahamu tano, wengine sita, wengine tisa...wengine mpaka ishirini na moja...la msingi, kila
response inakuashiria uchaguzi upi ni sahihi na upi ni batili...
 
Reactions: CPU
Ni kweli akifanya hivyo utakuwa umempa mwanya.., lakini in real life Marriage ni Kama Jahazi ambalo linataka watu wawili kusaidiana ili kuendesha maisha..., now kwenye marriage kuna responsibilities ambazo we all know kwamba mama huwa mara nyingi anaachiwa responsibilities za watoto kutokana na uchungu na upendo wa mama..., (its all good and most women enjoy that...) lakini maybe kama mwanaume angesaidia she could have juggled all the balls...,

I would never let someone sacrifice their life because of our love..., but if someone does am sure the blame should be on that other who let the other sacrifice their life....., na tusimlaumu mtu ambaye anakatisha furaha ya maisha yake kwa ajili ya mwenza au familia..., it takes guts.., na huenda yeye akaona kwamba its worth it (mapenzi yao na mwenzake).., kuliko her dreams...., Lakini ukweli ni kwamba anayekubali mwenzake aache dreams zake cause of himself (he is selfish) and hence amekatiza potential ya mwenzake.
 
teh teh teh kwa kweli maana kama sijatolewa roho basi maisha lazima yasonge!!

Mtu kajikwamisha mwenyewe halafu anadai Mbu ndo kasababisha nipate Maralia, akiambiwa atumie chandarua chenye dawa hataki
 

ha ha ha, Mwj1 nimekugusa ndipo eeh? ha ha ha!

&#9835; na bado, na bado, sijafika mwisho! &#9835;
Nalia kwa furaha - Bushoke ft Klynn



hahaha mkuu Mbu, just on light note, kuna ule wa Bushoke pia wa mume *****, sasa sijui Bushoke alikuwa ameharibiwa maisha in that context huh!
 
Reactions: Mbu
Mtu kajikwamisha mwenyewe halafu anadai Mbu ndo kasababisha nipate Maralia, akiambiwa atumie chandarua chenye dawa hataki
Na yule aliyeletewa magonjwa kwenye ndoa (mfano ukimwi)...,???
Au yule anayeambiwa na mwenzake kuwa kila anachofanya akiwezekani badala ya kumpa moyo
Mkuu all in all mafanikio yetu au kutokufanikiwa kwetu kunategemea the Company we Keep na ni nani tunashirikiana nae..,
 
mbu kaka, kwanza ctakagi kuamini kwamba ni mie niliruhusu fikra chafu ziniingie akilini, yaani nilikuwa mpuuzi sana kwa kweli, hii thread yako leo imenipa raha sana....
 
Reactions: Mbu
Ndo maaana mi bado komfusdi hapa? hivi kuharibiwa maisha ni kuto kuolewa au kuoa?
Hommie

Hivi maisha ili yawe maisha, ni lazima watu waoane?.........Hizi karaha zilizomo kwa wanandoa mpaka wengine kujuta kuoa/kuolewa ndio kuyapatia maisha?

Hapo kwenye red.....janaume litakalolia eti limeharibiwa maisha kwa sababu halijaoa lililotaka kumuoa...........lileteni huku nlifinye makalio yake.......wanawake lukuki mtaani wanataka kuolewa, linalia nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…