Umeshawahi kutake risk gani unayoikumbuka?

Aisee wewe ndiye Principal Risk Taker, yaani Ulikiweka Rehani Kiwanda!
 
Basi, ilikuwa hivi:

Nilikuwa nafanya kazi kwenye kampuni moja ya mjini, lakini boss wangu alikuwa na tabia za kunikera daily. Siku moja, baada ya misunderstanding kubwa, nikaamua ku-resign pale pale bila hata forward plan.

Kuacha kazi ghafla ilikuwa noma sana. Nilijikuta mtaani nikisaka job mpya bila immediate success. Ilikuwa kipindi kigumu, lakini nilijifunza kuwa na perseverance na kujituma zaidi.

Baada ya kuhangaika kwa muda, hatimaye nilipata job kwenye kampuni nyingine yenye mazingira bora zaidi. Uamuzi wa kuacha kazi kutokana na conflict na boss wangu ulikuwa na risk kubwa, lakini uliniwezesha kukua professionally na kujifunza umuhimu wa kufanya kazi kwenye mazingira yenye ushirikiano mzuri.
 
Wakati Nipo form two nakumbuka nilipewa ada nikatoa elfu 🤣🤣🤣 nikijua ni hela ndogo tu account ata-adjust iwe ada kamili bwana, risiti nikapewa huku narudi home ile Elfu 2000 nikaificha kwenye tochi zile bati enzi hizo. Ilikaa miezi, kila niikingia stoo naingalia kama ipo, siku ya siku list wasiolipa ada inatajwa nimo bwana, kwenda ofisini naogopa na home siwezi watasemaje nikanyuti kimya..kumbe matokeo ya mitihani yangu wamezuia ubaoni jina sioni, nikarudi kufata alfu mbili nikaikuta ishaanza kukauka kidogo na kupauka sababu joto maana sikuitumia nilitest zali 🤣🤣🤣, nikapewa matokeo yangu 🤣🤣🤣

Hadi sasa silambi hata mia nikiona inazagaa 🤣
 
Enzi zangu "Sha wahi kula Ada ya term nzima..na nlikuwa nadaiwa bado mtihani nilifanya ..siku tuna itwa wenye madeni hawapew chet mpaka walipe
Nikacheza trick moja kuna jamaa jina zinaendana kasoro lawazazi ye hadaiwi..alipo tajwa tu hajaskia vzr nikajichomeka nikaambiwa saini hapa nikasaini jina langu halisi cheti umepata..nilitoka nduki hatar
 
Kuna ya shule ya Kupeleka MZAZI FEKI ile ni VERY RISK ACTION.

Nilipeleka mzazi FEKI mwenye machachari sanaa,

Kufika akawa anajitia yeye ndo ana hasira ya kunilipia ADA kuliko baba angu, akawa ananizaba makofi kila nikitaka ongea ananipa MBATA la uso.

Hadi walimu wakawa wanaona BABA angu mkali...

Picha lilikuja HARIBIKA baada ya MWALIMU mmoja ambae ananijua na ni family FRIEND akawa anapita anakuta naadhibiwa ndio anapewa maelekezo kwamba mzazi wangu ananipga sana.

Nilipomuona tu yule TICHA nilishajua hapa tumeishaa kuliko aibu ya kudundwa mbele ya shule nzima acha tugoe NDUKI

Nikamkonyeza BABA FEKI yeye hanielewi anajitia anajua fatilia maendeleo yangu sana kwa walimu wengine.

Mimi nilichomoka kama BUNDUKI nikakimbizwa ila sijadakwa..

BABA feki alitaitishwa kesi ikaenda ishia POLISI walimpeleka.

Ile shule nilifukuzwa na mtaani BABA FEKI akawa ananitafuta.

ASANTE baba yangu mzazi kwa kunihamishia mkoani ambapo aliniepusha na adhabu ya yule baba feki maana naskia alinipania sana na nlikua sijamlipa hela yote nlimpa advance tu
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Nimecheka hadi baas, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Mwaka 2000 mida ya jioni maeneo ya ITV pale navuka barabara na mdogo wangu tulitokea upande wa ile baa moja maarufu ya Mwenge jina nimesahau kidogo ilikuwa opposite na kituo ITV, kabla hata sijavuka naona katikati ya lami kuna shilingi mia mia na hamsini hamsini zimetapakaa chini, nilivuka na dogo nikabaki nyuma simamisha magari yote 🤣🤣🤣 mwendo wa kuokota tu kuna watu 2 wakaja kujoin feast niliondoka kama na 1100 hivi, naona waligopa magari 🤣🤣. Dogo nikampa 400 nakumbuka, ingawa zilikuwa na michubuko sababu ya kupitiwa na tairi za gari, kuna coin nilifata karibu na bumper mwenye gari akatoa shingo nje alihisi anchomolewa taa sijui 🤣🤣🤣
 
Nimecheka hadi baas, [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
DO NOT TRY THIS AT HOME

wanafunzi na wasikie, ila bahati mbaya wanaotakiwa jifunza hatupo nao hapa JF

Tumebaki wote wa TBT tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…