Umewahi jiuliza kwanini tunapalilia mazao yakiwa bado ni madogo?

Umewahi jiuliza kwanini tunapalilia mazao yakiwa bado ni madogo?

Jesusfreak08

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2019
Posts
822
Reaction score
1,803
Habari zenu wapendwa natumai mnaendelea vizuri na mimi pia sijambo

Kwasababu kilimo pia ni sayansi basi hata mambo yanayofanywa kwenye kilimo huzingatia sana mambo pia yakisayansi

Kupalilia ni sehemu muhimu sana katika kusaidia mazao yako kukua na kama usipo inzingatia hii stage basi na kuhakikishia unaweza ukapelekea hata mazao yako kufa.

Sasa kuna umuhimu wa kufanya palizi pale mazao yako yanapokuwa madogo kwasababu ni kipindi ambacho mazao yanakuwa hajakua mizizi kwa kiwango ambacho ni kikubwa kwahiyo hata madini mmea unayohitaji yakiwa mbali basi sio rahisi kufanikiwa kuyapata na inaeweza kupelekea kifo cha mmea/zao lako.

Tunapongelea palizi namaanisha ni kuondoa mimea yote isiyohitajika wakati wa uukuaji wa mazao yako kwenye shamba lako sasa.

IMG_20210930_161355.jpg

Lakini magugu na majani(mimea) isiyo hitajika inahitaji madini yale yale ambayo pia mazao yako madogo yanahitaji yanaweza kutokea mambo mawili jambo la kwanza ni kuchukua madini yote au kunyang'anyana kwa madini kati ya mazao na magugu & majani

Je, kwanini uondoe?

●Ili kuhakikisha upatikani rahisi wa madini kwa mmea husika

●Ili kuondoa ushindani wa kutumia hayo madini kati ya mmea na magugu

●Kuondoa vizuizi vya mwanga wajua kwasababu magugu yanaweza kukua zaidi ya mazao

● Kuupa mmea eneo ya wenyewe kukua vizuri.

Kwaiyo palizi ni muhimu sana kwenye shamba lako usipofanya hivyo unaweza kupelekea hata shamba mimea yako kufa na baadae mavuno machache.
 
Kwaiyo palizi ni muhimu sana kwenye shamba lako usipofanya hivyo unaweza kupelekea hata shamba mimea yako kufa na baadae mavuno machache.
Nikweli mkuu shamba lako zuri sana pia nilipoona kichwa thread hii nilipeleka tafsiri katika maisha ya mwanadamu kwa maana ya malezi ni muhimu sana kwa watoto ili nao waweze kuwa wazazi bora wa baadae pia msemo wa samaki mkunje angali mbichi umenijia hivyo umegusa nyanja nyingi hongera sana ni eneo gani hilo naona una ardhi yenye rutuba nzuri, kazi nzuri.
 
Nikweli mkuu shamba lako zuri sana pia nilipoona kichwa thread hii nilipeleka tafsiri katika maisha ya mwanadamu kwa maana ya malezi ni muhimu sana kwa watoto ili nao waweze kuwa wazazi bora wa baadae pia msemo wa samaki mkunje angali mbichi umenijia hivyo umegusa nyanja nyingi hongera sana ni eneo gani hilo naona una ardhi yenye rutuba nzuri, kazi nzuri.
Nashukuru sana mkuu.
Lipo maeneo ya Njombe
 
Asante kwa kushirikisha ufahamu.

Ingawa ningetamani kujua kama tangu enzi za Mababu zetu walikuwa wanafahamu hivi, yaani walikuwa wanazingatia palizi na kujua umuhimu wake, au ilikuwa ni mwendo wa kubahatisha tu mpaka ilipokuja elimu hii? .
 
Asante kwa kushirikisha ufahamu.

Ingawa ningetamani kujua kama tangu enzi za Mababu zetu walikuwa wanafahamu hivi, yaani walikuwa wanazingatia palizi na kujua umuhimu wake, au ilikuwa ni mwendo wa kubahatisha tu mpaka ilipokuja elimu hii? .
Sidhani nafikiri ilikuwa inafanyika kama utamaduni lakini sio ile kitaalamu wakiawa na ufahamu huu
 
Wkend hii itanipendeza sana nikienda kuweka vijana w palizi shambani PWANI NANASI TIME
 
Back
Top Bottom