Umewahi kufanya prank gani?

Umewahi kufanya prank gani?

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Pranks si vitu vigeni. Tumefanya toka utotoni. Social media ni zimezifanya ziwe maarufu sana. Mimi ilikuwa hii.

Tulikuwa na jamaa yangu tumetoka chuo Muhimbili tunaelekea Mabibo hostel. Ndiyo tunaanza shule. Tunatembea hadi mtaa wa Congo kuchukua gari za kutoka Mnazi Mmoja.

Sasa kufika jengo la soko la Kariakoo kulikuwaga na wazee machinga wengi wanauza suruali za mtumba. Jamaa akataka suruali lakini wakajaa wengi sana kumzunguka. Ghafla akaanza kuongea kiingereza. Jamaa wakaanza kubabaika. Wananiuliza jamaa anavyosema mimi nawatafsiria.

Nikawaambia jamaa ni Mzambia. Basi wanataja bei kubwa, mimi namtafsiria jamaa. Jamaa anajidai, "Too expensive, too expensive." Wazee walihangaika sana wale.😀😀
 
Pranks si vitu vigeni. Tumefanya toka utotoni. Social media ni zimezifanya ziwe maarufu sana. Mimi ilikuwa hii.

Tulikuwa na jamaa yangu tumetoka chuo Muhimbili tunaelekea Mabibo hostel. Ndiyo tunaanza shule. Tunatembea hadi mtaa wa Congo kuchukua gari za kutoka Mnazi Mmoja.

Sasa kufika jengo la soko la Kariakoo kulikuwaga na wazee machinga wengi wanauza suruali za mtumba. Jamaa akataka suruali lakini wakajaa wengi sana kumzunguka. Ghafla akaanza kuongea kiingereza. Jamaa wakaanza kubabaika. Wananiuliza jamaa anavyosema mimi nawatafsiria.

Nikawaambia jamaa ni Mzambia. Basi wanataja bei kubwa, mimi namtafsiria jamaa. Jamaa anajidai, "Too expensive, too expensive." Wazee walihangaika sana wale.😀😀
ikawaje baada ya wazee kuhangaika
 
Daah mambo mengine ujinga sana

Ilikuwa ikifika usiku saa tano saa sita tunaenda kuchukua mashuka ya kulalia yalikuwa meupe tunajifunika gubi gubi na tunakaa kwenye kichochoro jirani na home chenye giza giza tulikimbizaga sana watu daah walevi ndio usiseme

Ila tulipokuja kufahamika tulijuta kuzaliwa
 
Kuna Ex wangu mwingine nilimtext na namba ngeni aje Hotel flani nina project inahitaji wanawake kwahiyo aje tuzungumze nimpe kazi àtalipwa

Nilimwambia akifika aagize msosi ale ili asiwe bored nipo hotel hiyo hiyo kwenye conference room kuna kikao so nikitoka nitamkuta

Alifika na akaagiza kweli msosi na akaweka status kuringishia watu full kujisnap anapost tu,hapo mimi nipo ghetto sipo kwenye kikao wala nini

sijui nini kiliendelea maana nilimblock nikawasha Pc na kucheza game
 
Ilikuwa 1st April. Nikadanganya home nimeteleza chuoni/ hostel kwa tiles. Nimeanguka, natoka damu puani.

Mama akachanganyikiwa 😂
Pesa zikatumwa..
Nilivyorudi likizo nikamwambia ukweli. Tokea hapo nikisema naumwa anataka uthibitisho wa Dr
 
Daah mambo mengine ujinga sana

Ilikuwa ikifika usiku saa tano saa sita tunaenda kuchukua mashuka ya kulalia yalikuwa meupe tunajifunika gubi gubi na tunakaa kwenye kichochoro jirani na home chenye giza giza tulikimbizaga sana watu daah walevi ndio usiseme

Ila tulipokuja kufahamika tulijuta kuzaliwa
Mlikuwa vizuri sana. Waliwafanyaje walipowajua?
 
Back
Top Bottom