Umewahi kufanya ukauzu gani kwa mpenzi wako?!


Hehehehehe ikitokea siku tumekutana nidai msimbazi/lakumi/10000.... Umenkosha sana yani we ndo dume... I hate faking (yanini kumfurahisha shetani wakati kiti anaumia)
 
@maryketi

kuna kujikuta umechemsha siku ya kwanza bila hata kujua ni kwa nini.

Bora hata huyu alichemka kwa kukosa hela, wengine tukielezea yalotupata mtasema tulivuta bangi. Things happen, sijui for what reason.

funguka baba!!
 

hii hata kama ni changa la macho...bado imekaa vyema sana!...ila mkuu ni kwamba tumekariri sisi vidume siku zote ndo wakutoa huduma!...tunajikamua mpaka damu...tunaingia madeni sugu...kisa uonekane uko juu...hatujui WANAWAKE ni waelewa sana...hili ni bonge la PINDI yani!...BIG UP MAN...
BTW mikasa yangu ni midogo midogo tu!..
 

Simpo, hapo red ingekwama ningeapply hiyo blue
 

Tatizo lako ni dogo tu; umeshazoea kwamba ni mwanaume tu ndo wa kupigwa mzinga!!
 

Mkuu,
Unafikiri ni changa la macho basi, ni true story! Ni kweli, mwanamke ndiye anajiona kwamba ana haki ya kuhudiwa kila kitu na mwanaume nae anajiona kama ndo mwenye wajibu wa kila ki2!
 
wewe ni jembe kaka, mimi ningeenda kukopa. ila usiniulize kwanini na wala usinilaumu
 
Mimi niliacha simu gesti, meneja aliniambia gest buku tatu mimi sikumuelewa kumbe ni kwa lisaa.
Bajeti yangu ilikua buku kumi na tano kila kitu.
Ilikua J'pili moja mtoto kanipigia simu anakuja getto. Siku hiyo ilikua noma maana mwenye nyumba anashinda nyumbani na kodi yake nshapitisha mwezi na nusu hivyo lazima angenikoromea.
Akili ya haraka haraka ilikuja niingie gest za uchochoroni. Saa saba na nusu hivi pale studio kituoni mtoto kashuka anaona tunaelekea kusiko.. kuniuliza kulikoni nikamwambia getto soo maji hamna alafu choo kinatoa harufu.
Tukafika hiyo gest kwa nje kuna mangi anakaanga chips kuku. Kuwa na uakika nikaenda kuuliza chumba nikaambiwa buku tatu ila nisubiri kidogo ataniita.
Wakati tunasuburi nikaagiza kuku chips 2 nikaona ngoja nipige na kamzika kadogo ka konyagi ili kuongeza kasi.
Mtoto alipiga soda yeye. Mangi kuleta bili nikakuta ninabakiwa na buku nne unusu, ambayo bado niliona nika vizuri kutokana na bei ya gest.
Meneja akanishtua tukaingia ndani... basi siku hiyo nilipiga gemu balaa. Tuliingia kwenye saa tisa tukatoka saa moja na nusu ivi
mtoto katangulia nje wakati mimi namalizana na meneja... mzee natoa buku tatu yangu jamaa aniambia bado buku 9..Du! alafu anaongea kwa nguvu na corido za gesti zilivyo na mwang'wi nikaona leo yamenikuta.
Nikamshtua mtoto nje vipi unapesa kidogo uniongezee... ananijibu hata nauli ya kurudi chuo ananitegemea, kidogo nianguke kwa presha.
Fasta fasta nikajifanya naongea na simu kumbe namfata mangi muuza chips barazani... nilikua nina Nokia kwa kipindi hicho ilikua ina thamani kama ya laki 2 unusu... nikatoa line yangu nikamwambia mangi anipe pesa.
Akasema hana shida ya simu ila kwa kunisaidia atanipa elfu thelathini kesho nimrudishie hamsini.
Basi nikavuta mkwanja nikalipa gest na mtoto nikamvutia buku kumi... akaniuliza hny umepata wa pesa.
Nikamwambia kuna jamaa nilimpigia alikua karibu ndo ameniletea.
Mpaka leo ni mke wangu na tuna watoto watatu hajawai kujuaga niliuza Nokia kwa elfu thelathini kulipia gest na nauli yake.
THIS IS TRUE STORY.
 

sasa hapo ukaudhu uko wapi mkuu wangu?
 

Dah!!!!!!!!! Hii yenu kiboko, kwa hiyo walijidai wezi, kumbe nyie ndo mlikuwa wezi zaidi yao.
 
nilichokupendea ni kua mkweli. na binti hakufata pesa kwako, alikupenda wewe ulivyo...
 

hongera kwa kuwa mwaminifu kwake hadi umeoa.big up
 
kuna mshikaji wangu ni eng. Pale tanga cement. Yeye alipata mtoto wa kishua mutoto ya kihaya kwao mboga saba na kazi nzuri anayo. mshikaji naye mkwanja upo. Mtoto akawa anakuja Tanga. Anakaa wknd yote kuanzia ijumaa hadi j2 jion anarudi bongo. Ila demu alikuwa ni mvivu wa kipika hvyo mara nyingi alimtaka msikaji wakale kwa hotel au baa, jaama alimpeleka kama mara mbili tu kwwa zile wk za ugeni. Alivyoona mtoto anazoea alianza kumpeleka kwenye misosi ya kina mama ntile wanaojipanga jioni na meza zao kuanzia pale maeneo ya stendi ya tanga njini taifa road kunziapale brbr ya 13 hdi brbr ya 18,.misosi ya bukubuku kwa mia saba. Akitoka hapo anampeleka kunywa juisi ya miwa kwa wapemba. Ilibidi demu baada ya muda ajivue asepe tu baada ya kuvumilia hako kamtindo kwa miezi 5.jamaa akasema alishamstukia demu sio mvumilivu hivyo alikuwa anampima kuwa kafata hela na status au ni mapenzi ya dhat?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…