Umewahi kufilisika kwa sababu ya mapenzi?

Umewahi kufilisika kwa sababu ya mapenzi?

OMOYOGWANE

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2016
Posts
4,701
Reaction score
11,920
1644557318554.png

Miaka michache iliyopita nilipata kazi ya mkataba, nikawa nakunja milioni moja kwa mwezi, nikaona maisha si ndio haya. Bahati mbaya nikaangukia kwenye mikono ya watoto wa mjini, laki laki zilikuwa zinatoka kama vile njugu, mara ohoo nikasuke, mara nimeichoka hii Tecno nataka samsung, mara nikanunue nguo baby, yaani pesa nilikuwa nazitumbua tu, full kula bata na mademu plus mitoko, kwa mwezi nilikuwa naenda ATM hata mara 5 na nikifika nadraw kuanzia laki mbili.

Mwisho wa siku mkataba unakuja kuisha nkajikuta sina kitu, hakuna hatua niliyopiga, Mademu wote wakanitosa nikajikuta nipo zero akili za kichwa cha juu ndio zikarudi mpaka leo nikikumbuka huwa najiona mpumbavu kabisa.

Toa ushuhuda na wengine wajifunze!
 
Nakumbuka nilisapotiwa na Bi. Mkubwa kuna kiasi alinipatia nikafanikiwa kufungua kaofisi kangu cha kupatia ridhiki.

Ndani ya muda huo nilikuwa kwenye mahusiano na binti fulani ambaye nilimpenda sana. Baada kama ya miezi miwili yule binti akawa haeleweki finally akaniacha. Akawa hataki kusikia chochote kutoka kwangu hapokei simu wala hajibu SMS. Stress za mapenzi zikaanza kunitesa, nikawa mlevi ajabu pesa niliyokuwa napata pale ofisini yote nikawa nalewea Baa na Washkaji.

Nikashindwa hata kutunza pesa ya kodi ya fremu ofisi ikafilisika ikafia uko.
 
Tupo wengi mkuu, naikumbuka 2018 January nikajipigia zangu milioni 2.3. Huyu EX nilivyokuwa nampenda sijui siku nina shida ya usajili wa biashara ama chochote TRA nitakuta nadaiwa bei gani maana nilitumia jina langu kumfungulia Saloon ya kike.
 
Honestly kwangu Hapana,

ila nmeona kwa wengi wa karibu yangu wakifilisika na kubaki majuto.

(Hii imenipa funzo pia)

Kiukweli,
Bajeti yangu ya mapenzi huwa Ni kile Cha ziada tu, na sio eti najitoa kwa Hali na Mali[emoji4]

(Ndo maana hata siku Moja sijawahi kubreak up na mwanamke afu eti nikamdai nilivomnunulia au kudai fidia)

Nikiona mapenzi yanaingilia mzunguko wangu wa Ela, huwa nachukua hakua za haraka sana (ziwe mbaya au nzuri au zakuumiza) ilimradi tu kurescue situation [emoji4]
 
Back
Top Bottom