Umewahi kuona umuhimu wa Himid Mao kwenye Timu ya Taifa?

Off course ana Add value kwenye timu ya Taifa...

Himid sio Talented player huyu ni wale wachezaji wa kutengenezwa + mazoezi na wachezaji wa aina hii mara nyingi huwa wakiwa uwanjani hawanaga zile moments za kukufanya mtazamaji ukabaki mdomo wazi (wow!🙊), yaani hawakupi kitu ambacho baada ya mechi mnaweza kumuongelea

Mara nyingi hawa huingia uwanjani kutekeleza ile kazi ambayo katumwa na kocha bila kuongeza hata nukta ya jambo jingine.
 
Nasikia baba ake CV zake zinambeba.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kitu gani ameshaga tekeleza uyu jamaa?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanasema wataalamu CV ya Baba ake inambeba

Sent using Jamii Forums mobile app
 
CV ya baba inambeba vipi tena? Au tukikubaliana na hii hoja kwamba CV ya mzee wake inambeba itakuwa ni hapa kwetu bongo kwasababu huyo baba tunamjua, haya vipi huko Egypt nako wanaweza vipi kumpa nafasi jamaa kwakuitumia CV ya mzee Mao Mkami?
Uko aliishiishusha daraja petrojet akanunuliwa kateam kaliko panda mfano ishuke stand United ipande biashara au Gwambina nako huko hachezi kiungo ni beki mbili Egypt pia kuna team mbovu tu mkuu .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
CV ya baba inambeba vipi tena? Au tukikubaliana na hii hoja kwamba CV ya mzee wake inambeba itakuwa ni hapa kwetu bongo kwasababu huyo baba tunamjua, haya vipi huko Egypt nako wanaweza vipi kumpa nafasi jamaa kwakuitumia CV ya mzee Mao Mkami?
Bongo kuna wachawi wengi sana ndugu yangu amini nakwambia, ikumbuke ile nyimbo ya Sam Hata kwetu wapo ndo utaelewa mkuu.

Yaani mtu hujawahi hata kupiga dana dana, hujawahi hata kufundisha timu hata ya mchangani tu, lakini unakalia kumsema Himidi Mao kuwa hamna kitu.
Makocha wote wanao kuja kuanzia timu ya taifa ya vijana, Azam, Stars wenyewe hadi huko Eygpt kila wanapopanga vikosi panga pangu lakini Himidi Mao Yumo tu, alafu mtu anakuja kuropoka tu et hamna kitu.

Kama sio uchawi kumbe ni nini?
Hawa wadau wengine wa soka hawa tukiwasikiliza sana soka la bongo tutalizika hivi hivi tunaona.
 
Ata takwimu tu sizani ata uyo jamaa kama ameshakuwaga man of the match ata mara moja.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi ni shabiki wa Man City pale EPL lakini ukiniuliza ni lini Fernandinho alikuwa Man of the match nitashindwa kukujibu labda hadi nikagoogle, pia pale La Liga napenda sana Barca lakini ukiniuliza ni lini Arturo Vidal alikuwa man of the match vile vile nitashindwa kukujibu.

Sasa kuhusu Himid ndio sikumbuki kabisa ata nikigoogle sidhani kama nitapata kama unavyojua sisi sio watu wa kuweka takwimu
 
Uko aliishiishusha daraja petrojet akanunuliwa kateam kaliko panda mfano ishuke stand United ipande biashara au Gwambina nako huko hachezi kiungo ni beki mbili Egypt pia kuna team mbovu tu mkuu .

Sent using Jamii Forums mobile app
Team haishushwi daraja na mtu mmoja mkuu, team inashuka daraja kwa kufail kama team + bench la ufundi na Management nzima kwa ujumla....

Team yake kushuka daraja na kisha yeye kupata team nyingine inayoshiriki league kuu inathibitisha ubora wake na inaonyesha kabisa kuwa ana kitu ....

Kubadilishwa namba kutoka kiungo hadi beki namba mbili pia inadhihirisha uwezo wake mwingine alionao wa kutumikia namba zaidi ya moja....
 
Uko ni kushuka ngazi utakubariana na mimi tu japo nakujua wewe ni mbishi sana ukiwa na vijana wako kwenye like na comments

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…