Umewahi kupigwa hadharani? Mimi yalinikuta!

Umewahi kupigwa hadharani? Mimi yalinikuta!

Mimi Mtaani kwetu walikua wananiita bluu siri maana enzi hizo ndio zmetoka jojo za chata ya bluu siri nilikua fiti sana kwa mateke, sasa bwana ilitokea kuna dogo alikuja jirani mgeni nakumbuka zilikua zmebaki siku chache krismas

Mi niliwakuta wanacheza mpira nikaomba namba wakanininyima nikaingia kwa nguvu mbaya zaidi nilikua golini nikaudaka nikaukatalia kumbe mpira ni wayule dogo

dogo akaja kuniomba mpila nikagoma huku naondokanao nikaona anavimbisha kifua nikamsukuma nikaona anakunja shati baaaasiiii nlikua mkorofi balaa nikamfata yaani sjui nlirusheje teke

Teke ya kwanza ikashikiliwa nikaanza kuburutwa kama nyoka mwishie nkaanguka jamaa kaniweka chini nikajaribu kutumia mabavu kumgeuza nikapigwa ngumi maeneo ya sikio nilijua nakufa nililia kwa nguvu huku nikiomba wamtoe nmetosha

hapo hakukua na watu wakubwa waliokuepo wote madogo tu kilichonsaidia alipita baba mmoja akatuachanisha kwa fimbo lijamaa ndo kukimbia mimi npo hoi huyo moja kwa moja nyumbani.

tokea hapo sjagombana tena


exalioth
jf geita
 
mbona wako sio mtumbwi wa vibwengo,wangu ni mtumbwi wa majini[emoji23][emoji23].
sipendi ugomvi mpaka umri huu kisa nilipigwa na mwanamke"mwanamke" nikiwa darasa la tatu tu.

shuleni nilikuwa mpenda sifa sana,halafu maarufu shule nzima nikiwa la kwanza tu.natongoza mpaka wadada wa darasa la saba wengine wanaambizana wanacheka nikipita,hwaelewi huo ujasiri nautolea wapi!!!!

tukiwa darasani nakumbuka demu mmoja ambaye niko naye darasani alikuja akanambia nini sijui??vile namwona mshamba sio hadhi yangu maana namingo na wakubwa nikamjibu mbovu,darsa zima likacheka wakaanza kumzomea,nisijue ana kinyongo na mimi nikaja kumuuliza nini sijui'akaninyooshea kidole nikakiputa kwamba aache dharau mimi sio wa kunyooshewa kidole,aisee kilikuja kibao hicho[emoji28][emoji28],sikutegemea kwakweli.
kujaribu kujibu mashambulizi aaah wapi!!nilichelewa akanikamata mikono,nyanyua juu akanishusha kama gunia juu ya dawati,mademu huwezi pigana naye ukiwa karibu atakuaibisha.
halafu yeye ni kama aliishaanza kuvunja ungo alinizidi pound kiasi fulani.

nilichapika kweli shati vifungo vyote kuleee,nakuja kuamuliwa sina hamu.
saa nne mapumziko napewa pole tu na warembo wangu wa madarasa mengine maana nilikuwa sitamaniki[emoji23].
Una kipaji cha uandishi.

Nimecheka mpaka mbavu zimeniuma [emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
 
We unacheza na njemba kutoka bush.
Zinakuwa na nguvu simchezo zinakula vyakula mlima. ..

Mini kuna jomba moja limetoka bush
Nikalichukulia ndezi ndezi nikazipanga kwani nilitoboa kila nikipiga jomba nikama nalitekenya

lilikaniotea nilipigwa ngumi ya uso mpaka macho yakacheza cheza.nkasema mungu wa yosefu ni mungu wadaudi...
Nkaona usntanie nikala chocho..
[emoji23] huku kata rufaa
 
Kuna watu wana mfupa mmoja kwenye mkono huyo akikupiga ngumi lazima akushushe hata kama anamwili mdogo
 
Mimi Mtaani kwetu walikua wananiita bluu siri maana enzi hizo ndio zmetoka jojo za chata ya bluu siri nilikua fiti sana kwa mateke, sasa bwana ilitokea kuna dogo alikuja jirani mgeni nakumbuka zilikua zmebaki siku chache krismas

Mi niliwakuta wanacheza mpira nikaomba namba wakanininyima nikaingia kwa nguvu mbaya zaidi nilikua golini nikaudaka nikaukatalia kumbe mpira ni wayule dogo

dogo akaja kuniomba mpila nikagoma huku naondokanao nikaona anavimbisha kifua nikamsukuma nikaona anakunja shati baaaasiiii nlikua mkorofi balaa nikamfata yaani sjui nlirusheje teke

Teke ya kwanza ikashikiliwa nikaanza kuburutwa kama nyoka mwishie nkaanguka jamaa kaniweka chini nikajaribu kutumia mabavu kumgeuza nikapigwa ngumi maeneo ya sikio nilijua nakufa nililia kwa nguvu huku nikiomba wamtoe nmetosha

hapo hakukua na watu wakubwa waliokuepo wote madogo tu kilichonsaidia alipita baba mmoja akatuachanisha kwa fimbo lijamaa ndo kukimbia mimi npo hoi huyo moja kwa moja nyumbani.

tokea hapo sjagombana tena


exalioth
jf geita
Nimecheka sana.
 
Mimi sinaga nguvu ila na hasira kali sana.Nilichokuwa nakifanya ntakutemea mate usoni au ntakumwagia mchanga usoni then mbio nyingi sana nyumbani.
 
[emoji23][emoji23][emoji23] Daah nimekumbuka mbali sana Shule ya Msingi Yombo Dovya
 
Mimi Mtaani kwetu walikua wananiita bluu siri maana enzi hizo ndio zmetoka jojo za chata ya bluu siri nilikua fiti sana kwa mateke, sasa bwana ilitokea kuna dogo alikuja jirani mgeni nakumbuka zilikua zmebaki siku chache krismas

Mi niliwakuta wanacheza mpira nikaomba namba wakanininyima nikaingia kwa nguvu mbaya zaidi nilikua golini nikaudaka nikaukatalia kumbe mpira ni wayule dogo

dogo akaja kuniomba mpila nikagoma huku naondokanao nikaona anavimbisha kifua nikamsukuma nikaona anakunja shati baaaasiiii nlikua mkorofi balaa nikamfata yaani sjui nlirusheje teke

Teke ya kwanza ikashikiliwa nikaanza kuburutwa kama nyoka mwishie nkaanguka jamaa kaniweka chini nikajaribu kutumia mabavu kumgeuza nikapigwa ngumi maeneo ya sikio nilijua nakufa nililia kwa nguvu huku nikiomba wamtoe nmetosha

hapo hakukua na watu wakubwa waliokuepo wote madogo tu kilichonsaidia alipita baba mmoja akatuachanisha kwa fimbo lijamaa ndo kukimbia mimi npo hoi huyo moja kwa moja nyumbani.

tokea hapo sjagombana tena


exalioth
jf geita
Kumbe dogo kabisa sisi tumezaliwa ata jojo hazipo dunianj
 
Mimi sinaga nguvu ila na hasira kali sana.Nilichokuwa nakifanya ntakutemea mate usoni au ntakumwagia mchanga usoni then mbio nyingi sana nyumbani.
Kama mimi tu. Ilikuwa unaweza kunipiga sana ila ukiniachia lazima nirushe mawe na matusi juu. Ukifanikiwa kunikamata tena nakuomba msamaha, upenyo ukipatikana nduki na mitusi tena
Ila utoto raha sana.
 
  • Kicheko
Reactions: EEX
Nakumbuka nikivyokuwa form 1 mwaka 2004 kuna muhuni alikuwa form 3 alikuwa anapenda sana sifa hasa akiona madem

So kuna siku alinikuta nakula mihogo akaiputa na kuimwaga dah kiukweli sikuwa na nguvu na nilikuwa muoga lakin nilimtia kichwa yule muhuni mpaka kapandaisha mashetan mi mbio tangu siku hiyo nilikiwa maharufu kwa jina la mzee wa mashetan
 
Hello,

Kuna muda hasa utotoni na tukiwa vijana wadogo huwa ni kawaida mtu ajitetee kwa kupigana, Hata wanyama hupigana ili kutafuta haki ama kuonyesha dominance.

Sasa katika mapambano haya kuna muda unakuta huna tofauti na mtu alievamia mtumbwi wa vibwengo, unaishia kuchapika mbele ya hadhara, Loh aibu hiyo isikieni tu.

Binafsi nakumbuka katika siku niliyopoteza pambano ilikuwa nikiwa kidato cha tano (form 5), Pambano lilikuwa ni mimi mtoto wa town mwenye rekodi yangu nzuri tu tangu shule ya msingi na mtaani nishakalisha wengi, niliyakanyaga kwa jamaa flani katoka kijijini huko mikoani namuona mshamba mshamba.

Nilikuwa napenda kumtania tania ila kuna siku alimaindi sana tukiwa darasani, nikamwambia atulize mshono jogoo wa shamba hawiki mjini, darasani pale nusu tudundane lakini tukakubaliana tuyamalize baada ya vipindi, mida ya saa saba hivi baada ya kutoka kwenye vipindi tukaenda nyuma ya ukuta wa shule ndio ilikuwaga sehemu ya kuyamaliza matatizo kiume.

Nikawa naruka ruka ile kujiona kama tyson kumtambia huyo jamaa wa bush jinsi watoto wa mjini tunavyopasha kabla ya mfumuo, mtoto wa town nikatumia mbinu yangu ya surprise attack, ile hata hajajiandaa vizuri nikamrushia ngumi kama mbili hivi, hii mbinu nishaitumia kumaliza pambano mapema ila kwa huyu jamaa hali ikawa tofauti, kwake ni kama ngumi zangu zilimpapasa yani kama hazijamuingia hata, alinirushia ngumi nikakwepa nikaongeza ujazo kwenye ngumi yangu kudhania za kwanza sikuzijazia lakini jamaa ilikuwa ni kama napiga gunia la mchele daaah!

Yeye ngumi nyingi akirusha nakwepa ila chache zinazonikuta ni zinauma jamani, ni kama napigwa na mawe, maumivu haya yalinipa hasira nikawa namtupia upper cut lakini wapi, narusha za chembe lakini wapi, narusha teke lakini ni kama napiga gunia tu, aisee!

yeye ngumi yake akiirusha inauma jamani acheni tu.
Ilibidi nikimbie pambano lakini watu walikuwa wametuzunguka wananisukuma nirudi ulingoni, najaribu kuzikinga ngumi za jamaa lakini jamaa ngumi zake zinaumiza mpaka mikono nayotumia kujikinga, na nikimrushia jama ngumi ni kama napiga gunia la mchele, kiukweli nilikata tamaa, tena kuna muda alinisoma ile navyomrushia ngumi nae anarusha yake na ikinikuta ilikuwa inanipasua kweli kweli.

Bahati yangu viranja walikuja kutuachisha lakini nilikuwa nimetandikwa si mchezo.
Nakumbuka tu baada ya wiki tulikuwa marafiki sana na huyo jamaa lakini aibu niliyoipata ile siku siwezi kuja sahau.

Nikiwa Darasa Pili bana Kuna Binti alikuwa White Sanaa class, ana Dadaake Darasa la tano,Mwanaume nikaleta uhuni wa Kitaa Kwa Kuanza kumpiga Sound Classmate, Mtoto akawa hataki, nikawa na force, akanisemelezea Kwa Sistaake wa Darasa la tano.

Darasa la Pili na La Tano yapo Mkabala, ukiwa Darasani kwetu wa Darasa la tano unamuona,vivyo hivyo wa Darasa la tano, yule Sistaake akawa ananioneshea Kidole Kunionya na kuniambia nitaona tukitoka shule.

Basi Kwa Ujeuri na plus kupewa Bichwa na wanangu wa Kitaa Class kuwa Demu anakutisha vipi, baadae Mpe kichapo

Basi bana, baada ya Kengele ya Parade, na baada ya kuruhusiwa tu Dada Mtu akaniibukia Kwa Mbele, Niko na Wanangu kadhaa, tukacheka sana, Wanangu walivyo Mashabiki, wakaanza kunifungua vifungo vya shati na kunipa Bichwa, Dada katulia tuliiii, Mikono kaweka Kwa Nyuma, ananisikilizia tu Navyojazwa na Wanangu.

Kumbe Dada Kwa Nyuma kashika Mfagio wa Chelewa, e bana eeeh, ghafla akanijia, nilichapwa Jamani na Lile Fagio, Dakika tano usoni sitamaniki, nilikuja kuokolewa na Kaka Mkuu aliyekuwa anapita ile Njia.

Wanangu wale walivyokuwa Wasenge wote wakasepa wakati Kamanda wao nimeingia Matatani.

Yule Demu White classmate sijui yuko wapi.
Natamani nikutane nae Ukubwani, Kwa Lile tukio najua anaweza kunipa game Ukubwani huku akinicheka.

Since then Mimi Sijawahi Kupigana kabisa
 
Ukutane na mwamba kama huyu katoka bush umletee mbambambaa, ww rukaruka ukitulia tu anakuweka
20220921_205624.jpg
 
mbona wako sio mtumbwi wa vibwengo,wangu ni mtumbwi wa majini[emoji23][emoji23].
sipendi ugomvi mpaka umri huu kisa nilipigwa na mwanamke"mwanamke" nikiwa darasa la tatu tu.

shuleni nilikuwa mpenda sifa sana,halafu maarufu shule nzima nikiwa la kwanza tu.natongoza mpaka wadada wa darasa la saba wengine wanaambizana wanacheka nikipita,hwaelewi huo ujasiri nautolea wapi!!!!

tukiwa darasani nakumbuka demu mmoja ambaye niko naye darasani alikuja akanambia nini sijui??vile namwona mshamba sio hadhi yangu maana namingo na wakubwa nikamjibu mbovu,darsa zima likacheka wakaanza kumzomea,nisijue ana kinyongo na mimi nikaja kumuuliza nini sijui'akaninyooshea kidole nikakiputa kwamba aache dharau mimi sio wa kunyooshewa kidole,aisee kilikuja kibao hicho[emoji28][emoji28],sikutegemea kwakweli.
kujaribu kujibu mashambulizi aaah wapi!!nilichelewa akanikamata mikono,nyanyua juu akanishusha kama gunia juu ya dawati,mademu huwezi pigana naye ukiwa karibu atakuaibisha.
halafu yeye ni kama aliishaanza kuvunja ungo alinizidi pound kiasi fulani.

nilichapika kweli shati vifungo vyote kuleee,nakuja kuamuliwa sina hamu.
saa nne mapumziko napewa pole tu na warembo wangu wa madarasa mengine maana nilikuwa sitamaniki[emoji23].
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
 
Mimi tangia nikiwa mdogo mzazi aliniambia ukiona watu wanapigana kimbia ,ndo ikawa desturi yangu,wakianza tuuuh kupigana mimi nachukua marathon mpaka nyumbani.


Kwa kawaida shuleni nilikuwa mpole sana,sikuwa napenda ugomvi na mtu,nilikuwa mtu mkimya na mwenye maneno machache kuliko wanafunzi wote.
Nikiwa darasa la saba ,siku moja nikiwa darasani ,mara paaap nikaaanzisha ugomvi na binti wa watu ,nilikuwa najiamini kweli,kumbe nilipanda mtumbwi wa vimbwengo,nikaona ngoja na mimi nionyeshe ubabe kidogo wakati huo,kila mara naona watu wanapigana,aiseeeh kilinichonikuta nikasema sitaaanzisha ugomvi tena,mimi nilipigwa ngumi moja na mtoto wa kike uso ukavimba vibaya mno ,nililia mpaka ticha anakuja kunibembeleza ,akaona sio kesi akaninunulia na ubuyu,nikapokea na pole nyingi kwa wenzangu ,saivi nikiona kuna dalili ya ugomvi kutokea na slow down,ili niepukane na aibu.


Ile siku sitaisaaahau mabinti wa vijijini wana mikono migumu sana ,mimi ata skutumia nguvu ilipigwa moja nikawa naona [emoji93] [emoji93] [emoji93] [emoji93][emoji93][emoji93][emoji93][emoji93][emoji93][emoji93] tuuuh .
 
Mimi tangia nikiwa mdogo mzazi aliniambia ukiona watu wanapigana kimbia ,ndo ikawa desturi yangu,wakianza tuuuh kupigana mimi nachukua marathon mpaka nyumbani.


Kwa kawaida shuleni nilikuwa mpole sana,sikuwa napenda ugomvi na mtu,nilikuwa mtu mkimya na mwenye maneno machache kuliko wanafunzi wote.
Nikiwa darasa la saba ,siku moja nikiwa darasani ,mara paaap nikaaanzisha ugomvi na binti wa watu ,nilikuwa najiamini kweli,kumbe nilipanda mtumbwi wa vimbwengo,nikaona ngoja na mimi nionyeshe ubabe kidogo wakati huo,kila mara naona watu wanapigana,aiseeeh kilinichonikuta nikasema sitaaanzisha ugomvi tena,mimi nilipigwa ngumi moja na mtoto wa kike uso ukavimba vibaya mno ,nililia mpaka ticha anakuja kunibembeleza ,akaona sio kesi akaninunulia na ubuyu,nikapokea na pole nyingi kwa wenzangu ,saivi nikiona kuna dalili ya ugomvi kutokea na slow down,ili niepukane na aibu.


Ile siku sitaisaaahau mabinti wa vijijini wana mikono migumu sana ,mimi ata skutumia nguvu ilipigwa moja nikawa naona [emoji93] [emoji93] [emoji93] [emoji93][emoji93][emoji93][emoji93][emoji93][emoji93][emoji93] tuuuh .
[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom