Umewahi kutokewa na hali kama hii ulipokuwa umelala?

TIASSA

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2014
Posts
2,926
Reaction score
3,530
Unajihisi unataka kuamka na upo kwenye akili za kawaida kabisa lakini hauwezi kusogeza hata msuli mmoja wa mwili wako hata ukipiga kelele sauti haisikiki. Nina maswali kuhusiana na hili
(1) je hii ni hali ya kibailogia au ni mapepo na mashetani?
(2) je ikitokea ukashindwa kupambana kuamka utakufa?
(3) je ukiwa katika hali kama hiyo mtu akaja kukuamsha kwa kukutingisha nini kitatokea..
(4) je nini husababisha..
Hata mimi huwa inanitokea mara moja moja kwa mwaka hasahasa ninapo kuwa nimelala chali yaani nimelalia mgongo.

Nashukuru kama nitapata majibu
 
nilisikia sina uhakika nilisikia sina uhakika narudia nilisikia sina uhakika kua wakati umelala viungo vyote hua vinakufa ganzi kwa hiyo hali ile hutokea wakati hisia zisharudi katika hali yake ya kawaida isipikuwa viungo vinakua bado
 
Pole_nilikuwa napatwa na hali hiyo zaman sana. ni Jinamizi. ni mdudu mwenye mkono wenye vidole viwili hukukaba koo kwa vidole hivyo viwili


anaua kabisa. tena fasta

mimi nikinikipwa na hali hiyo nasoma aya tuh kursii yanaachia
 
Hata mm ishanitokea sana, wajuzi mkuje hapa mtupe ufahamu wa hili swala
 
Hua ina nitokea especially ninapokua nimelala sana
 
Nataman sana uilete jukwaa la intelijensia pale kuna wajuzi sana
 
Pole_nilikuwa napatwa na hali hiyo zaman sana. ni Jinamizi. ni mdudu mwenye mkono wenye vidole viwili hukukaba koo kwa vidole hivyo viwili


anajua kabisa. tena fasta

mimi nikinikipwa na hali hiyo nasoma aya tuh kursii yanaachia

ushawai kumuona mkuu?
 
Ishawahi kunitokea siyo mara moja.. ila kwa sasa haijanitokea tena...
 
Kama umewahi kulala kisha ukaota kuwa upo sehemu umekabwa au kuna hali imekaa kooni kwako kisha sauti haitoki basi tambua hilo ni pepo, au ni wachawi walikuwa wanakukaba.
Usiku mwema.
 

Binafs imeshanitokea sana,hakuna idadi
 
Pole_nilikuwa napatwa na hali hiyo zaman sana. ni Jinamizi. ni mdudu mwenye mkono wenye vidole viwili hukukaba koo kwa vidole hivyo viwili


anaua kabisa. tena fasta

mimi nikinikipwa na hali hiyo nasoma aya tuh kursii yanaachia

Hongera mdau,yaan ukiwa katika hali ile utaweza kusoma kweli,au ukishastuka ndo unasoma?
 
Kama umewahi kulala kisha ukaota kuwa upo sehemu umekabwa au kuna hali imekaa kooni kwako kisha sauti haitoki basi tambua hilo ni pepo, au ni wachawi walikuwa wanakukaba.
Usiku mwema.

Mdau anachokizungumzia si hicho
 
ishanitokea hiyo nlivopata chance ya kujitambua niliruka kidogo nikatwe na pangaboy(Feni la juu)
 
Mwili wa kila kiumbe umepewa SUBCONSCIOUS hii ni sehem ambayo inafanya kazi without your conscious awareness!inaratibu vitu vyote mfano inapotokea hatari kama tungetumia conscius mind tungeshakufaga wote sbb iko slow sana kwenye snap decisions.unapokuw umelala then ukaota ndoto ya kutisha kuna fluid ambayo inafanya mwili uparalze temporary ili usijidhuru wakati unatishika ndotoni ndo maana ya jinamizi sio kwamba umekabwa au umekosa oxgen km watu wanavyodhani.Subconscious inafanya kazi involunteery yaan huwez kuicontrol kama mapigo y moyo au digestion y chakula.
 
MI inanitokea kuwa nimelala nimejifunika shuka mpaka usoni, kwaiyo huwa nakosa hewa kila nikijaribu kujitoa shuka nashindwa mikoni yangu imekosa nguvu ya kutoa shuka nipate hewa
 
All of the above
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…