Umezuka Ugonjwa wa Kusahau Kulipa Madeni!

Umezuka Ugonjwa wa Kusahau Kulipa Madeni!

Setfree

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2024
Posts
1,679
Reaction score
2,123
Mtu anakuja kwako analia, kilio cha msibani. Anapiga magoti umkopeshe pesa. Unamkopesha kwa moyo safi kabisa. Anaondoka kwa shangwe utafikiri bwana arusi kaoa. Muda mliopatana wa kulipa deni ukifika, ghafla anapatwa na "ugonjwa wa kusahau kulipa madeni."

Ugonjwa usiotibiwa hospitali, ambao dawa yake ni "kidonge" kimoja tu - kulipa deni.😂 Cha ajabu ni kwamba, anasahau madeni tu, lakini nyama choma hasahau kula. Hasahau kuhonga wanawake. Hasahau “kilauri”

Ukimkumbusha deni, anakutazama kama vile umemkosea adabu; anashika kifua utafikiri ana shambulio la moyo. Anaanza hotuba ya maisha magumu, yenye maudhui kuliko mihadhara ya chuo kikuu.

Wakopaji wengine wakimuona kwa mbali aliyewakopesha, wanabadilisha “ruti.” Wengine wanabadili namba zao za simu. Mkopaji anayejiona mjanja zaidi kuliko sungura, atakuambia yuko safarini, akishuka atakupigia! Utasubiri wee, simu hupigiwi mpaka jogoo anawika! Asubuhi ukimuuliza vipi kulikoni, anakujibu: "Ooh samahani nilisahau." Wanaojifanya wamezaliwa na “simu janja,” wao “wanakupiga tofali” kabisa.

Biblia inasema wazi: "Asiye haki hukopa wala halipi" (Zaburi 37:21). I dare to talk openly:🗣️ ukikopa benki, ukikopa kwenye taasisi za kifedha, ukikopa kwa mtu, usiwe miongoni mwa wasio haki – lipa deni. Vinginevyo moto mkali wa jehanamu unakuhusu.😆
 
Uzi mzuri. Tujitahidi kulipa madeni. Wale wafanyabiashara wenzangu mnaopewa mzigo kwa mali kauli tunzeni uaminifu. Kuna manufacturer wa nchini India huwa namsikitikia sana kwa kuwapa mzigo wa mali kauli wabongo ambao wengi wameingia mitini na mamilioni ya watu. Kuna mmoja ni maarufu sana kwenye biashara yake hapa nchini kakimbia na zaidi ya 100m za mhindi.
 
Sio ugonjwa kwa kusahau kulipa madeni bali ni uhalisia kwamba watanzania wengi wanaingia katika aina mpya ya uchumi bila maandalizi wala utaratibu maalum; uchumi huu nadhani unaitwa "credit economy"
Yaani tunaanza kuendesha maisha kwa madeni, sio muda mrefu mkisikia mtu kajenga nyumba mpaka kamaliza kwa hela zake binafsi bila mkopo wa bank basi kweli huyo hela anazo
Yaani unaweza ona mtu ni mfumbufu kukulipa deni lako kumbe wewe ni wa kumi kwenye mnyororo
 
Mtu anakuja kwako analia, kilio cha msibani. Anapiga magoti umkopeshe pesa. Unamkopesha kwa moyo safi kabisa. Anaondoka kwa shangwe utafikiri bwana arusi kaoa. Muda mliopatana wa kulipa deni ukifika, ghafla anapatwa na "ugonjwa wa kusahau kulipa madeni."

Ugonjwa usiotibiwa hospitali, ambao dawa yake ni "kidonge" kimoja tu - kulipa deni.😂 Cha ajabu ni kwamba, anasahau madeni tu, lakini nyama choma hasahau kula. Hasahau kuhonga wanawake. Hasahau “kilauri”

Ukimkumbusha deni, anakutazama kama vile umemkosea adabu; anashika kifua utafikiri ana shambulio la moyo. Anaanza hotuba ya maisha magumu, yenye maudhui kuliko mihadhara ya chuo kikuu.

Wakopaji wengine wakimuona kwa mbali aliyewakopesha, wanabadilisha “ruti.” Wengine wanabadili namba zao za simu. Mkopaji anayejiona mjanja zaidi kuliko sungura, atakuambia yuko safarini, akishuka atakupigia! Utasubiri wee, simu hupigiwi mpaka jogoo anawika! Asubuhi ukimuuliza vipi kulikoni, anakujibu: "Ooh samahani nilisahau." Wanaojifanya wamezaliwa na “simu janja,” wao “wanakupiga tofali” kabisa.

Biblia inasema wazi: "Asiye haki hukopa wala halipi" (Zaburi 37:21). I dare to talk openly: ukikopa benki, ukikopa kwenye taasisi za kifedha, ukikopa kwa mtu, usiwe miongoni mwa wasio haki – lipa deni. Vinginevyo moto mkali wa jehanamu unakuhusu.😆
Nani huyo aliyekula hela yako na hataki kulipa 😃
 
Sio ugonjwa kwa kusahau kulipa madeni bali ni uhalisia kwamba watanzania wengi
Charles Ponzi alikuwa Mzungu mwenye asili ya Italia aliyefanya ulaghai mkubwa wa kifedha Marekani mwanzoni mwa karne ya 20. Alikopa pesa kutoka kwa wawekezaji kwa ahadi ya kulipa faida kubwa, lakini badala ya kulipa faida hizo, alitumia pesa mpya za wakopaji wapya kulipa wakopaji wa awali – mfumo unaojulikana kama Ponzi Scheme. Mwishowe, aliposhindwa kuwalipa watu waliomkopesha, alidai hakuwa na pesa na kudai kwamba mambo yaliharibika kwa bahati mbaya. Wengi wa waliomkopesha walipoteza kila kitu, huku yeye akijifanya hakuwa na uwezo wa kulipa madeni.

Kisa hiki kinaonyesha kwamba hata Wazungu, matajiri au watu wa kawaida, wanaweza pia kuwa na "ugonjwa wa kusahau kulipa madeni"
 
Charles Ponzi alikuwa Mzungu mwenye asili ya Italia aliyefanya ulaghai mkubwa wa kifedha Marekani mwanzoni mwa karne ya 20. Alikopa pesa kutoka kwa wawekezaji kwa ahadi ya kulipa faida kubwa, lakini badala ya kulipa faida hizo, alitumia pesa mpya za wakopaji wapya kulipa wakopaji wa awali – mfumo unaojulikana kama Ponzi Scheme. Mwishowe, aliposhindwa kuwalipa watu waliomkopesha, alidai hakuwa na pesa na kudai kwamba mambo yaliharibika kwa bahati mbaya. Wengi wa waliomkopesha walipoteza kila kitu, huku yeye akijifanya hakuwa na uwezo wa kulipa madeni.

Kisa hiki kinaonyesha kwamba hata Wazungu, matajiri au watu wa kawaida, wanaweza pia kuwa na "ugonjwa wa kusahau kulipa madeni"
Huyo Ponzi alifanywaje? Hakuuponza Ponzi kweli?
 
Huyo Ponzi alifanywaje? Hakuuponza Ponzi kweli?
Charles Ponzi aliposhindwa kulipa madeni, mambo yalimuendea mrama kabisa! Huu ni muhtasari wa yaliyompata:
  1. Kashfa yake Ilibumburuka (1920) – Mfumo wake wa Ponzi ulikuwa umekusanya zaidi ya dola milioni 15 kutoka kwa maelfu ya wawekezaji. Hata hivyo, watu walianza kutilia shaka biashara yake, na vyombo vya habari vikaanza kuchunguza.
  2. Watu Walianza Kudai Pesa Zao – Watu walipoanza kutaka faida zao, Ponzi alishindwa kulipa kwa sababu hakuwa na biashara halali—alikuwa akitumia pesa mpya kulipa wakopaji wa awali.
  3. Alikamatwa na Kufungwa – Mwaka 1920, alishtakiwa kwa udanganyifu wa kifedha na kufungwa miaka mitano gerezani. Baadaye, alihukumiwa tena kwa makosa mengine na alitumikia kifungo cha miaka 14.
  4. Alihamishwa na Kufukuzwa Marekani – Baada ya kutoka gerezani, Marekani ilimfukuza (deportation) hadi Italia kwa sababu hakuwa raia wa Marekani.
  5. Alijaribu Kujipanga Upya Lakini Akashindwa – Baada ya kufika Italia, alihangaika kutafuta maisha. Alifanya kazi ya vibarua, hata akajaribu kufanya ulaghai mwingine nchini Brazil lakini hakufanikiwa.
  6. Aliishia Kuwa Maskini wa Kutupwa – Mwishowe, Ponzi alikufa akiwa masikini sana huko Brazil mnamo mwaka 1949. Aliachwa na kila mtu, aliishi maisha ya shida; alikosa hata nauli ya kurudi nyumbani.
Umejifunza Nini? Ukikopa au kufanya ulaghai, siku moja utabumburuka tu! Hakuna shortcut kwenye kulipa madeni! Na mwishowe ni🔥 milele
 
Back
Top Bottom