Umihimu Wa Kitambulisho Cha NIDA ni nini?

Umihimu Wa Kitambulisho Cha NIDA ni nini?

ndio shida ya kuishi kwenye shithole country,wenzetu motto anapozaliwa tu kabla mama hajaruhusiwa kurudi nyumbani,motto anasajiliwa na kupewa birth certificates yenye ID number ambayo ni kama jina lake maana atakufa nayo,na number hiyo imo ndani ya central systems ya nchi nzima,kuanzia kwenye mabenki,polisi,maduka ya kukopesha etc etc

Well acha nikurekebishe hapo kidogo kwa uzuri tu. The contry is not shithole. The country is a jewel ni zahabu in its own. Systems ziko in place but the people ambao wanatikwa kushughulikia hizo vitu ndioambao hawafai. Tusi laumu nchi yetu, tuwalaumu hao wanafanyia kazi. Naomba tusianze kutukanana humu. Tujadiliane tu kwa uzuriipi ni zurina lipi ni baya na tu toe maoni juu ya kwanini tunafikiri kuwa lipi ni baya na lipi nii zuri...
 
Kitambulisho cha taifa ni nyaraka muhimu inayokuthibitisha na kukutangaza kama raia wa nchi husika kwa mamlaka zote zilizoko katika eneo la Tanzania. Msingi wa kutolewa kitambulisho cha Taifa ni cheti chako cha kuzaliwa ambacho, kwa hakika ni tangazo linaloelezea kuwa tarehe na mwezi katika mwaka fulani ulizaliwa mahali fulani katika jamhuri hii kwa kuwataja wazazi wako wote wawili.

Pasi ya kusafiria ni nyaraka inayotolewa na serikali kwa kukutambulisha wewe kama raia wa nchi hii pale tu unapohitaji kufanya safari nje ya mipaka ya nchi yetu, pale ambapo hakuna utaratibu wa kikanda uliowekwa kama mbadala. Ili upate pasi ya kusafiria ni lazima uthibitishe kuwa wewe ni raia wa nchi hii kwa kutoa cheti cha kuzaliwa. Hapa ndipo mamlaka ya uhamiaji inapoingia kazini.

Kwamba mamlaka ya uhamiaji imepewa mamlaka ya kuchunguza uhalali wa cheti cha kuzaliwa kwa kuchunguza asili ya wazazi wako kwa kuangalia wazazi wako, babu/bibi zako na hata ukoo wako hadi vizazi vitatu ili kujiridhisha kama unastahili kutambulika kama raia na kwa kuwa unasafiri kutambulishwa huko ugenini kama raia wa Tanzania.

Kwa waliotutangulia usajiri wa mtoto hufanyika mara tu anapozaliwa kuanzia namba ya mtoto kati ya watoto waliozaliwa kwa siku hiyo, wodi aliyozaliwa au kama ni nyumbani, namba ya mkunga aliyemhudumia katika mtaa, hospitali tajwa na mkoa husika. Taarifa zote huingizwa kwenye kanzidata ya taifa ili mamlaka zingine zitakapozihitaji ziweze kurejewa. kwa kawaida huwa hawatoi cheti cha kuzaliwa zaidi ya kopi tu ya taarifa zako. Mtoto anapofikisha miaka 18 anatambulika kama mtu mzima na hivyo ni lazima apewa kitambulisho cha Taifa lake mbali na vitambulisho vingine vya shule, kazi au vilabu mbali mbali.

Kwa Tanzania mamlaka za juu zilikuwa hazitunzi vizuri taarifa za vizazi na vifo kama inavyotakiwa, taarifa za kuzaliwa zilikuwa zinafahamika vyema kwa wazazi wenyewe na wakati mwingine kwenye nyumba za ibada na mashuleni.Kwa sasa serikali inataka kutunza taarifa hizi katika sehemu moja ili iwe rahisi kutumika pale zinapohitajika.

Mkanganyiko unaojitokeza sasa hivi kwenye utoaji wa vitambulisho vya taifa, unatokana na ukweli kwamba tunafanya mambo ukubwani huku serikali ikitegemea taarifa sahihi kutoka wetu kwa kuwa haikuwahi kuzikusanya na kuzitunza vizuri tangu ilipozaliwa Tanzania. Mfumo uliotayarishwa kupokea taarifa hizi unahitaji kuunganishwa na mifumo mingine ili taarifa zote zinazohitajika zipatikane kutoka sehemu moja..Watendaji kwa kiasi kikubwa ni watu wazima ambao mambo haya ya kufanya kazi kimtandao ni kitu kigeni kwao hata kwa vijana wetu wa leo pia.
 
BONGO BHANA MI HUWA NAJIULIZA HUWEZ KUPATA PASSPORT MPKA KITAMBULICHA NIDA JE HAKUNA OPTION NYINGINE ILI KUWEZA KUONDOA USUMBUFU UKIENDA NIDA KITAMBULISHO KUPATA TABU KILA KITU TABU KWANN KUSIWE SYSTEM MAALUM AMBAYO UHAMIAJI ITAKUA INA RAHISISHA KAZI KIWEPESI TU KULIKO KUMUHANGAISHA MTU BAFO TUNA SAFARI NDEFU SANA KM TZ HVI TUTAFIKIA UCHUMI WA VIWABDA KM KUMPATIA I.D TU AU PASSPORT RAIA HALALI WA TANZANIA NI MBINDE KM UNAFANYA BIASHARA YA MADAWA YA KULEVYA?...
 
Kitambulisho cha taifa ni nyaraka muhimu inayokuthibitisha na kukutangaza kama raia wa nchi husika kwa mamlaka zote zilizoko katika eneo la Tanzania. Msingi wa kutolewa kitambulisho cha Taifa ni cheti chako cha kuzaliwa ambacho, kwa hakika ni tangazo linaloelezea kuwa tarehe na mwezi katika mwaka fulani ulizaliwa mahali fulani katika jamhuri hii kwa kuwataja wazazi wako wote wawili.

Pasi ya kusafiria ni nyaraka inayotolewa na serikali kwa kukutambulisha wewe kama raia wa nchi hii pale tu unapohitaji kufanya safari nje ya mipaka ya nchi yetu, pale ambapo hakuna utaratibu wa kikanda uliowekwa kama mbadala. Ili upate pasi ya kusafiria ni lazima uthibitishe kuwa wewe ni raia wa nchi hii kwa kutoa cheti cha kuzaliwa. Hapa ndipo mamlaka ya uhamiaji inapoingia kazini.

Kwamba mamlaka ya uhamiaji imepewa mamlaka ya kuchunguza uhalali wa cheti cha kuzaliwa kwa kuchunguza asili ya wazazi wako kwa kuangalia wazazi wako, babu/bibi zako na hata ukoo wako hadi vizazi vitatu ili kujiridhisha kama unastahili kutambulika kama raia na kwa kuwa unasafiri kutambulishwa huko ugenini kama raia wa Tanzania.

Kwa waliotutangulia usajiri wa mtoto hufanyika mara tu anapozaliwa kuanzia namba ya mtoto kati ya watoto waliozaliwa kwa siku hiyo, wodi aliyozaliwa au kama ni nyumbani, namba ya mkunga aliyemhudumia katika mtaa, hospitali tajwa na mkoa husika. Taarifa zote huingizwa kwenye kanzidata ya taifa ili mamlaka zingine zitakapozihitaji ziweze kurejewa. kwa kawaida huwa hawatoi cheti cha kuzaliwa zaidi ya kopi tu ya taarifa zako. Mtoto anapofikisha miaka 18 anatambulika kama mtu mzima na hivyo ni lazima apewa kitambulisho cha Taifa lake mbali na vitambulisho vingine vya shule, kazi au vilabu mbali mbali.

Kwa Tanzania mamlaka za juu zilikuwa hazitunzi vizuri taarifa za vizazi na vifo kama inavyotakiwa, taarifa za kuzaliwa zilikuwa zinafahamika vyema kwa wazazi wenyewe na wakati mwingine kwenye nyumba za ibada na mashuleni.Kwa sasa serikali inataka kutunza taarifa hizi katika sehemu moja ili iwe rahisi kutumika pale zinapohitajika.

Mkanganyiko unaojitokeza sasa hivi kwenye utoaji wa vitambulisho vya taifa, unatokana na ukweli kwamba tunafanya mambo ukubwani huku serikali ikitegemea taarifa sahihi kutoka wetu kwa kuwa haikuwahi kuzikusanya na kuzitunza vizuri tangu ilipozaliwa Tanzania. Mfumo uliotayarishwa kupokea taarifa hizi unahitaji kuunganishwa na mifumo mingine ili taarifa zote zinazohitajika zipatikane kutoka sehemu moja..Watendaji kwa kiasi kikubwa ni watu wazima ambao mambo haya ya kufanya kazi kimtandao ni kitu kigeni kwao hata kwa vijana wetu wa leo pia.

Mweshimia umeongea vizuri sana na jambo la maana pia. Lakini msimamo wangu uko pale pale.

Mimi navo sema ni hivi

NIDA NI SAWA NA VIFUTAVYO
-Uraia wangu
-Cheti changu chakuzaliwa
-Vyeti vya wazazi wangu na babu na bibi zangu.

Nisameheni kama mnaona sielewi.
 
Mweshimia umeongea vizuri sana na jambo la maana pia. Lakini msimamo wangu uko pale pale.

Mimi navo sema ni hivi

NIDA NI SAWA NA VIFUTAVYO
-Uraia wangu
-Cheti changu chakuzaliwa
-Vyeti vya wazazi wangu na babu na bibi zangu.

Nisameheni kama mnaona sielewi.
Mkuu ni kwamba kitambulisho cha NIDA ndio hasa kinachotambulisha uraia na utaifa wako na ndio cheti muhimu kuwa nacho, Hivyo vingine hutolewa kwa madhumuni tofauti vikitumia kitambulisho cha taifa ambacho msingi wake ni cheti cha kuzaliwa. Kama nilivyoandika hapo mwanzo, taifa letu linafanya mambo haya ukubwani, yalipaswa kufanyika kabla.

Mwelekeo ni kuwa tukipata wote vitambulisho vya Taifa, vizazi na vifo vikasajiriwa na kuingizwa kwenye mfumo, kisha mifumo ya RITA, NIDA, Uhamiaji, TRA, anuani za makazi vikaweza kusomana, basi hakutakuwa na sababu ya kuambiwa ulete cheti cha kuzaliwa au nyaraka nyingine isipokuwa hicho cha NIDA tu.

Lakini mkuu kumbuka nchi ilikuwa inaenda kienyeji sana kiasi kwamba ukiwa ma mafuta kwenye mkono vyuma vyote vilikuwa vinalainika na kukuwezesha kupata hata kile usichostahili.
 
Mi swali langu limenyooka sana. Umihimu wa kuwa na kitambulisho cha NIDA ni nini?

Maana tukienda kutengenezesha Passport mpya tunahitajika ku wasilisha vyeti vya kuzaliwa na vinginevyo.

Mimi kwa akili yangu nilikuwa nafikiria kuwa tukishapata Kitambulisho cha NIDA basi tena kutakuwa hakuna usumbufu waku ulizana kuhusu vyeti vya hadi baba ake babu.

Hebu jamani nyie ambao mna elewa sheria tunaomba ufafanuzi kidogo humu.
Mkuu,
Umeishasema kwa akili yako; sasa unataka nani abadili hiyo mawazo yako?
Bali ukiona kitambulisho cha NIDA hakina maana!
 
Kuna Taasisi moja nilijaza taarifa flani. Waliniuliza kitambulisho cha Taifa au cha kuzaliwa..nikagundua kuwa kitambulisho cha NIDA kinatumika mbadala wa cheti cha kuzaliwa.
Yap,ukifanya online booking kwa upande wa ndege,ukienda airpot na kutoa kitambulisho cha NIDA,umemaliza kila kitu.
 
Mweshimia umeongea vizuri sana na jambo la maana pia. Lakini msimamo wangu uko pale pale.

Mimi navo sema ni hivi

NIDA NI SAWA NA VIFUTAVYO
-Uraia wangu
-Cheti changu chakuzaliwa
-Vyeti vya wazazi wangu na babu na bibi zangu.

Nisameheni kama mnaona sielewi.
Mkuu,
Wale wanaoona huko sawa si waachane na NIDA?
Tunajaribu kwenda kwenye Digital wengine hawataki.
Utawaambia nini sasa?
 
Back
Top Bottom