Ummy Mwalimu acha kuwahadaa Watanzania wewe sio mwadilifu

Ummy Mwalimu acha kuwahadaa Watanzania wewe sio mwadilifu

Afrikasana

JF-Expert Member
Joined
Oct 27, 2021
Posts
320
Reaction score
288
Jana kupitia vyombo vya habari waziri wa TAMISEMI Ummy Mwalimu amewataka wakurugenzi kufanya alichokiita msawazo wa watumishi katika halmashauri zao akilenga zaidi kwa walimu.

Amedai kwamba katika halmashauri nyingine sio kwamba walimu hawatoshi bali tatizo ni watumishi kulundikwa sehemu moja kwa wingi na kwingine ndani ya halmashauri hiyohiyo hakuna nguvukazi ya kutosha.

Ninamwambia Ummy aache kuwahadaa watanzania akiwafanya ni mazuzu yasiyoona. Mfano mzuri nikatika halmashauri yake ya Tanga jiji ambapo ndani ya ofisi ya Afisa elimu sekondari kuna kiini macho. Wapo maafisa elimu taaluma watatu na jamaa mmoja ambaye alikuja na afisa elimu sekondari kutoka huko aliko kua.

Mtu huyo aliyekuja na afisa elimu hajulikani kama anacheo gani kwenye hiyo ofisi. Je wale waliojazana pale sio walimu? Je wanafanya kazi gani pale zaidi ya majungu pale ofisini?

Kwataarifa yako Ummy nikwamba huyo jamaa aliyehama na huyo afisa elimu ndio anatumwa na afisa elimu huyo kwenda kuchukua bahasha za chochote kitu kwa wakuu wa shule. Pamoja na afisa elimu taaluma mmoja pale ambae naye anatumwa kukusanya posho kutoka kwa wakuu wa shule.

Pamoja na kuwapo kwa maafisa elimu taaluma wawili haitoshi Ummy kamuweka rafiki na kada mwenzake akawe afisa elimu taaluma ndani ya ofisi hiyo hivyo kuna maafisa elimu taaluma watatu kwenye ofisi moja. Je huo msawazo kwanini usianzie maofisini? Ummy ameamua kulipa fadhila kupitia ofisi ya umma hata kama hakuna uhitaji. Je wewe Ummy huo ndio msawazo au mvurugo?

Ummy unaiharibu Tanga kwakulea marafiki zako huku ukitaka watanzania watende haki.Nakuuliza je wewe kama haki huiwezi utawashurutisha vipi wenzako watende haki?

Kaondoe yule rafiki yako kwenye ofisi ya afisa elimu sekondari ambaye alikua mkuu wa shule ya sekondari Toledo kisha ndio utangaze msawazo.

Ukiongea uongo utakumbushwa. Ummy badilika ofisi ya umma sio kijiwe cha kubwabwaja pasipo kumaanisha. Tenda kwa usahihi ndio uwaongoze wengine kutenda kwa usahihi
 
Tena m babaishaji sana huyo anapenda kubwabwaja huku anachekacheka
Ummy anajua halmashauri yake imetawaliwa na rushwa ya ngono, wizi, ubadhirifu na kulindana.

Kwenye elimu ukabila na ukada ndio tiketi ya cheo

Waumini wa ngono mwenzao Daudi ameondolewa wao wanatamba eti ndio waliomuweka Ummy sasa niwakati wa kula nae mema ya nchi.

Ummy ameharibu halmashauri tena atulie asibwabwaje na kucheka cheka
 
Kama.taarifa hii ni kweli ajitafakari kama anatosha.

Halafu nani aliyesema waongeaji ndio watendaji..wengi ni vilaza.

#MaendeleoHayanaChama
 
Kama.taarifa hii ni kweli ajitafakari kama anatosha.

Halafu nani aliyesema waongeaji ndio watendaji..wengi ni vilaza.

#MaendeleoHayanaChama
Taarifa niyakweli.

Ofisi ya afisa elimu inanuka rushwa na ubadhirifu.

Ofisi inawatu wamelundikana haijulikani afisa elimu taaluma hasa ni nani sasa haitoshi Ummy au TAMISEMI wanapeleka afisa elimu taaluma mwingine.

Ninarudia tena kusema kuna jamaa anaitwa Mgombera yupo kwenye ofisi ya afisa elimu naalikuja nae kutoka Muheza.

Je kazi ya Mgombera ni nini na anakaa na afisa elimu kama nani pale ofisini?

Je Muheza haina upungufu wa walimu hadi huyo bwana amfuate afisa elimu Tanga jiji?

Je Tanga haina shida ya walimu tena mpaka wakalundikwe kwenye ofisi ya afisa elimu?

Ummy wacha fix,Tanga jiji pameoza wizara imekushinda
 
Ummy anajua halmashauri yake imetawaliwa na rushwa ya ngono,wizi,ubadhirifu na kulindana.

Kwenye elimu ukabila na ukada ndio tiketi ya cheo
Waumini wa ngono mwenzao Daudi ameondolewa wao wanatamba eti ndio waliomuweka Ummy sasa niwakati wa kula nae mema ya nchi.
Ummy ameharibu halmashauri tena atulie asibwabwaje na kucheka cheka
Kweli Ummy amejichanganya kwa kumpa jamaa yake uafisaelimu taaluma Tanga jiji.
Huyo Dada ameonekana mlipaji fadhila mzuritu
 
Huyu hana lolote

Ndio maana siku zote amekuwa mbunge wa viti maalum
Mshukuru JPM.
Tanga hatuna utamaduni wa kumchagua mwanamke kuwa kiongozi.
Yeye Dini siunajua sasa sema chochote.
Na hutorudi tena
 
Sas hapo kakosea nini? Waziri katoa Muongozo wa kisera mwenye wajibu wa kuhakikisha linafanyiwa Kazi ni Katibu Mkuu.

Pili hayo malalamiko yako peleka kwa DED ukishindwa yupo RAS.
Kosa lake nikuhubiri msawazo wa watumishi wakati yeye ndio mvurugaji na kinara wa kupigia chapuo jamaa na makada wenzake.
Ofisi yenye afisa elimu taaluma wawili kisha anampeleka mtu wa tatu pale?

Kuna rafiki wa afisa elimu sekondari aliyekuja nae kutoka Muheza na hana cheo Ummy anajua.Nadhani utaelewa sasa
 
Huyu hana lolote

Ndio maana siku zote amekuwa mbunge wa viti maalum
Mshukuru JPM.
Tanga hatuna utamaduni wa kumchagua mwanamke kuwa kiongozi.
Yeye Dini siunajua sasa sema chochote.
Na hutorudi tena
Mh. Rais ajue kwamba Ummy ni miongoni mwa mawaziri wanaoifikiria zaidi 2025 na inawezekana anasuka safu yake Tanga jiji
 
Kila waziri anahaha baada ya kupata fununu kuhusu FAGIO, mwenye uhakika na nafasi yake mpka sasa ni waziri wa afya tu... wengine wote matumbo joto
 
Kila waziri anahaha baada ya kupata fununu kuhusu FAGIO, mwenye uhakika na nafasi yake mpka sasa ni waziri wa afya tu... wengine wote matumbo joto
Ana mambo ya kitoto sana huyo Dada. Eti kazi yake kumposti mh. Rais huko Instagram. Hiyotu nidharau tosha. Mtu mzima tena waziri kazi kushinda kwenye media ukimpost mkuu wa nchi. Ummy aibu yako na utapigwa chini kwasifa na tabia zako
 
Back
Top Bottom