Ummy Mwalimu ayakubali maoni kinzani maduka ya dawa

Ummy Mwalimu ayakubali maoni kinzani maduka ya dawa

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001
Screenshot_20220125-173614_Chrome.jpg


Anaandika katika kurasa yake Twita

Tumepokea maoni na ushauri kuhusu Kanuni za mwaka 2020 zinazosimamia usajili wa majengo ya dawa (ikiwemo maduka binafsi karibu na Hospitali/Vituo vya huduma za Afya vya Serikali.

Ni mjadala mzuri. Tumefurahi kujua kuwa watanzania wengi tunakubali kuwa lipo tatizo kubwa ktk mfumo.mfumo mzima wa ugavi, usambazaji na usimamizi wa dawa. Sisi @wizara_afyatz tutasimamia maslahi ya watanzania kwa kuhakikisha kuwa wanapata dawa ambazo ni salama, zenye ubora na kwa gharama nafuu. Hivyo tutakuchukua hatua kadri tutakavyoona inafaa ili kufikia lengo hili ikiwemo

Kwanza, tutaisimamia vyema
@MsdTanzania kutimiza wajibu wake ktk kununua, kuhifadhi na kusambaza dawa nchini.

Pili, tutaboresha mifumo ya udhibiti na usimamizi wa dawa na bidhaa nyingine za Afya katika Hospitali na Vituo ya kutoa huduma za Afya vinavyomilikiwa na Serikali.

Tatu, Tutasimamia kikamilifu matumizi ya Mwongozo wa Taifa wa Matibabu (National Standard Treatment Guideline) wa mwaka 2021; cheti cha dawa sambamba na miongozo mingine ili kuwapunguzia wananchi adha ya kutafuta dawa wanazoandikiwa ambazo zipo nje ya Miongozo ya Matibabu.

Dawa ni Sayansi, Dawa ni Uhai, Dawa ni Biashara na Dawa ni Siasa. Asanteni wote kwa maoni. Tumeyapokea na tutayafanyia kazi.
 
Kwa hiyo kwa kauli hii anatengea agizo la kutaka maduka ya dawa ya binafsi yakae umbali wa mita 500 kutoka ilipo hospitali?
 
Kwa hiyo kwa kauli hii anatengea agizo la kutaka maduka ya dawa ya binafsi yakae umbali wa mita 500 kutoka ilipo hospitali?
Suala la kusimamia MSD itoe madawa za kutosha kulingana na taratibu za Ugavi ni muhimu kabisa. Kwasababu kwanza dawa zipatikanazo MSD Bei ni rahisi kushinda zinazouzwa na watu binafsi.

Kwahiyo hata Kama maduka ya watu binafsi yatafunguliwa ndani ya Hospitali, kwa vyovyote wagonjwa wataendelea kununua zile za MSD kwasababu Bei Ni rahisi. Mkiimarisha Ugavi wa dawa Mimi sioni haja ya kuondoa maduka ya watu binafsi wanaouza dawa nje ya Hospitali.

Tuwaache waendelee na shughuli zao maana Kuna wakati Hospitali zetu hukosa dawa kwahiyo linapotokea Hilo wagonjwa wawe na mahari karibu pa kununua dawa.

Wakati huo huo tuimarishe udhibiti wa dawa kusiwepo na udokozi au wizi wa dawa kupitia watumishi wa Hospitali hizo. Hao ndo wanatakiwa watungiwe Sheria Kali endapo watakamatwa wakiiba dawa.
 
Maduka ya dawa ya serikali(MSD) huwa na "Dawa muhimu..ESSENTIAL MEDICINES"... urasimu huchangia kupatikana kwa changamoto nyingi. Maduka ya dawa ya watu binafsi huwa na Dawa muhimu pamoja na dawa maalum"SPECIAL MEDICINE"hakuna urasimu hapa.
 
MSD wakiweza kusambaza dawa za kutosha kwa hospitali zetu hayo maduka ya madawa karibu na zilipo hospitali yatakufa yenyewe natural death, waziri asihangaike nayo kwa sasa, aiangalie MSD zaidi.
 
Yaani wenyewe washindwe kusimamia dawa zao waanze kuja kutusumbua huku mtaani. Dawa kazima ziuzwe maeneo ya hospitali maana ndipo penye uhitaji. Huwezi kumchapa mtoto wa jirani kwa wewe kushindwa kumlea mwanao. Ile hoja ya mita 500 ilikua inaeleweka na mwendawazimu tu.
 
Kwa hiyo kwa kauli hii anatengea agizo la kutaka maduka ya dawa ya binafsi yakae umbali wa mita 500 kutoka ilipo hospitali?
Hili la mita 500 halina tija.

Hata hayo maduka yangekua kilomita kumi as long as madawa yanaibiwa hayawezi kuwepo hospitali.

Kwanini wewe Ummy usidhibiti wizi kwanza?

Sioni logic ya duka la dawa zilizoibiwa kuwa mbali na hospitali, Kama hosp hhakuna dawa atakayefuata madawa mbali Ni mgonjwa. Na mwizi yuaendelea kula kwa urefu wa kamba yake.
 
View attachment 2095277

Anaandika katika kurasa yake Twita

Tumepokea maoni na ushauri kuhusu Kanuni za mwaka 2020 zinazosimamia usajili wa majengo ya dawa (ikiwemo maduka binafsi karibu na Hospitali/Vituo vya huduma za Afya vya Serikali...
Huyu dada Ummy atambue kuwa kushindwa kazi kwa mfumo wa usambazaji wa Wizara yake hautikani na wauza madawa binafsi.
Aboreshe usambazaji dawa wizarani na kwa bei nafuu, madua ya biashara yatakufa yenyewe.

Uvivu wako biashara kwa wengine.
 
Ummy huwa anakurupuka Sana. Analeta mipasho kwenye kazi.

She is an attention seeker.
 
Back
Top Bottom