Ummy Mwalimu: Ruksa Madaktari kutumia hospitali za Serikali kama private clinic baada ya muda wa kazi

Kosa kubwa sana hili

Kutumia jengo na vifaa tiba vilivyotokana na kodi ya wananchi kama private clinic tena?

Madaktari watazembea ili ukifika muda wa private clinic wapige pesa
Mbona yasemekana Private Clinics kwenye hospital kama MNH, MOI, JKCI zipo toka zamani
 
Wewe mfanyakazi wa serikali huna vitega uchumi vingine, hufanyi kazi nje huna biashara, Wewe ni wazi ni wale wajamaa wamiaka ya 80 huko hakuna ruhusa kufanya kazi nje ya kazi yako hakuna kumiliki nyumba 2 nadhani ni mawazo yako. Sasa nitajie DR gani bingwa hana kazi yake nje ya kazi ya serikali? kama hana Clinic yake ana shirikiana na private Hosp kama hana basi anapita Hosp hata 4 kwa wiki na ana appointement yake. Nataka wewe uniambia ni nani hana kazi nje ya kazi yake?

wenzetu nje watu wanapiga kazi mbilimbili ndio wanafika wewe unataka kudumaza watu na fikra za kijamaa mambo yameshapitwa na wakati. Nadhani labda age yako inakusuma mawazo hayo kama kina Shivji.
 
Wewe wa miaka ya 70 wajomba zako kina Shivji mmekunywa maji ya ujamaa, mambo hayo hayana nafasi amka huu mwaka 2023. Eti shift wakitoka hawa wanaingia ma Dr wengine unadhani hao walinzi wa Group 4? taja hiyo Hosp ina shift 24 Hrs ma Dr wanabadilisha. Usilete ujinga hapa na kauli za kisiasa tumenunua na kodi zetu hivi wewe unajuwa wanaolipa kodi nchi hii? hawafaiki hata million na siajabu wewe mmoja wapo haujawi kulipa kodi zaidi ya vifine tu labda. Ukiona mtu anarukia hii mali ya watu ujue hana akili, hata ndege zimenunuliwa na pesa za kodi unapanda bure? Mwendokasi kodi unapanda bure? Umeme kodi unapewa bure? maji ni kodi unapewa bure? ujinga tu.
 
Kumbe ushasema kazi ya nje, sasa wewe kwenye hospitali ya umma unakutaka ufanyie kazi zako za nje ili iweje. Nani asiyejua kuhusu vijiwe dogo, vijiwe vipo vingi na part time zipo za kutosha kuanzia aga khan, Rabininsia, Hindumandal na kwingineko. Fanyia kazi zako za nje uko. Tatizo unafikiri unaongea mshabiki au lay men. Dogo mambo yote hayo unayo nayaongea nayajua. Na extra work kuearn money mbona hadi biashara zipo acha ushamba. Yaani acha strict policy ibaki hivyohivyo, acha kuweka siasa. Wewe sio wa kwanza kujua kuhusu vijiwe na part time dogo. Ila acha hospitali za umma zibaki za umma. Kafanye biashara kwingine. Its public hospital not private property.
 
Ndio babu nimekusikia ila mzee staafu acha mawazo ya kina Nyerere kutuletea sisi waziri kisha tamka sasa hutaki wewe hama nchi wala usitupigie kelele wenye pesa watachagua wanataka kupiga foleni na wewe au waje jioni watibiwe. Ila tuondolee mawazo ya kizamani hapa. Hata mjini iko lunch mpaka alfu sio lazima ukale 20k
 
Sasa unabisha kuhusu shift, au call allowances zinalipwa kwa yeyote yule. Sasa maisha yangu kulipa kodi unayataka ya nini😂😂😂,
Yaani wewe mimi kutokulipa kodi umejuaje😂😂😂, unanijua kweli boss. Unabisha kuhusu shift au call allowances mnavyozipaginia ni za uongo. Acha siasa chief! Yaani unataka nielezee kazi yangu humu ujue kama nalipa kodi, sahau. Ila acheni siasa, madili hospitali hatuyataki. Fanyeni kazi, maliza sepa katafute kijiwe upige pesa😂😂😂. Acha hospitali iendelee kujiendesha yenyewe, private matters, tafuta private location.
 
😂😂😂 umeshindwa hoja. Yaani mnakuwa hamna hoja kwaujumla, ni kurukaruka tu. Mnauzwa mpo tu, kwakuwa linakufaidisha wewe basi haina shida ilayakikudhuru mnaanza kupayuka. Nchi ya ajabu kweli. 😂😂😂 ndio wasomi wa leo, halafu hadi WHO guidelines kuna mtu kakuainishia kule juu ila umefumba macho. Unayumba kijana.
 
Mimi binafsi ummy nimemuelewa alimaanisha nn , ujumbe umufikie muhusika. Mawaziri wengine waige hii !!
 
Bahati mbaya na wewe hunijui nadhani ungenijuwa labda ungekuja na kunishika mguu kuomba msamaha, ndio raha ya huku JF.
 
Hapo tunauzwa basi nimeshakujuwa ndio wale wale wazee wakupinga kila kitu hapo umejiweka hadharani wewe ni nani. Tuache na CCM yetu tuna imani nao 😛
 
Ummy anachomaanisha watu wasiache kazi wakimbilie vijiweee so wataweka utaratibu wawe wanafanya vijiwe hapoo ule muda wa ziada ila bado inaacha maswali maana Madaktari huwa wawalipwa overtime labda anataka hizo overtime zionekane ni sawa na hela ambazo wangeenda kufanya clinic binafsi.. Kama tamisemi hospital nyingi watu wanapiga mzigoo hata overtime zinakuja kwa kuchelewa sana so ni LUGHA YA KISIASA kama ukitafsiri haraka haraka utaona ummy kazingua ilaa kawachota akilii vizuri sana madaktarii maana usitegemee daktari atafanya kazi nje ya muda wake alafu HELA AKUSANYE AWEKE MFUKONI weee...weee umesikia wapi mapato yanaingia serikalini mwisho wa siku wanamegewa kiasi kama ikipendezwa serikalii 😀 😀 😀 😀
 
Hapo tunauzwa basi nimeshakujuwa ndio wale wale wazee wakupinga kila kitu hapo umejiweka hadharani wewe ni nani. Tuache na CCM yetu tuna imani nao 😛
😂😂 chief fanya kazi, madili hayatakiwi na siasa waachie wengine. Ungenijua labda, hunijui bado dogo. Ajira kwenye afya sio utajiri ni wito ohoo. Pia hapo umeonyesha umekosa hoja, yaani wewe bado sana dogo.
 
Mlipenda zama za Kikwete,sasa zinalejea kwa kasi-ile nidhamu aliyokuwa ameanza kuijenga Magufuli katika utoaji wa huduma ya afya sasa inakwenda kutoweka
Ni huyo huyo Magufuli ndio katuletea huyu Mama - mara mbili!

Samia hakuwahi kunyosha kidole kutaka uongozi, kila nafasi ya kitaifa kateuliwa. Wito wa public service hana, rekodi ya nyuma hana, upeo hana, uzalendo hana.

Na siku anapewa u vice president anasema mwenyewe alilia, alikataa, akasema hawezi. Kalazimishwa.
 
😂😂 chief fanya kazi, madili hayatakiwi na siasa waachie wengine. Ungenijua labda, hunijui bado dogo. Ajira kwenye afya sio utajiri ni wito ohoo. Pia hapo umeonyesha umekosa hoja, yaani wewe bado sana dogo.
Wito, acha siasa bwana mtu kasoma miaka 7 unasema kazi ya afya wito. wito ni mgambo tu acheni fikra mbovu hizi imewaita walimu wito mpaka imekuwa kazi imekosa heshima sasa unawaita wafanyakazi wa afya wito. Nini maana ya wito, ajitolee au unataka kusema nini? hakuna kazi ya wito hizi ni proffesional ajira uwe Dr uwe Nurse hizi kazi zinaheshimika nchi zingine wewe unasema wito.
 
Kwani kuna profession isiyo heshimika, kutokuheshimu umeamua mwenyewe usizungumzie wengine dogo. Halafu Doctor of Medicine degree ni 5yrs kwa TZ hiyo 7 ni yako. Internship period sio sehemu ya kusoma M.D degree.
Pia kosa kubwa vijana wakiwa wadogo wanaaminishwa kuwa udaktari unakufanya kuwa tajiri. Yaani its very different, ungekuwa Botswana, S.Africa, Germany na USA uko ungesema hivyo. Ila daktari hatajiliki kwa udaktari hata kidogo, ukiona katajirika ujue kuna kitu cha ziada kingine. So kamwe usianze kupindisha guidelines na kumalpractice ili utajirike, utauwa wengi. Ukiambiwa daktari ni wito jifunze kutafakari, sawa😂😂😂. Udaktari waweza kupa standard life ila ukitaka ya ziada, pasha kichwa hicho.
 
Wewe bado sana kama bado uko na mawazo hayo unasafari ndefu sana mwisho utasema jeshi ni wito pia. Hakuna kazi ya wito labda uwe mwenyekiti wa nyumba kumi.
 
Vipi kwa sisi tulioko Wilayani ambako hakuna hospital za Private? Kwanini tupange foleni kimasikini?
Hakuna wilaya isiyokuwa na hospitali ya private!! Kama wewe ni tajiri bado unaweza ukaifuata hospitali iliyoko mkoa mwingine!! Kama matajiri huenda hadi India kutibiwa wewe unayedai tiba ya kitajiri si uifuate ilipo!! Huwezi kufanya starehe kwa kutumia mali ya mwingine!! Hospitali za umma ni za watanzania kupitia kodi zao, hatukubali mtu binafsi azifanyie biashara yake binafsi!! Huyu Ummy tutampeleka mahakamani ka,ma akikomaa na huu uamuzi wake usio na tija kwa Taifa!
 
sasa muda wa kazi ndo hawatafanya kazi kabisaa sasa ni rushwa kwa kwenda mbele,huyu waziri sasa bange kapiga
 
Huwezi kusema wanaolipa kodi hawafiki hata milioni au wewe unajua kodi moja tu ya mapato? Kodi aina ya VAT wanalipa watanzania wote wakiwemo watoto (wanaolipiwa na wazazi wao). Kila wakati mtanzania ananunua bidhaa au huduma na kupewa risiti ya EFD anakuwa amelipa kodi ya VAT.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…