Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amesema Sheria inayomuondoa mstaafu wa sekta binafsi kwenye Bima ya Afya baada ya kustaafu itarekebishwa ili kumutendea sawa na watumishi wa sekta ya umma.
Waziri amesema hayo baada ya kuulizwa swali na Deodatus Balile, ambapo alisema kwa sasa watumishi wa sekta ya umma huendelea kuhudumiwa na bima ya afya hadi wanakufa wakati watu wa sekta binafsi huwa hawaendelei kuhudumiwa.