beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,880
- 6,368
Ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kukabiliana na dharura inasema zaidi ya watu milioni sita katika maeneo kame ya mashariki na kusini mwa Ethiopia watahitaji msaada wa kuyaokoa maisha yao mwaka huu.
Shirika hilo linasema zaidi ya watu milioni 6.4 katika maeneo yaliyoathirika wanakadiriwa kuhitaji msaada wa chakula mwaka huu na wakati ambapo serikali ya Ethiopia na washirika wake wa misaada ya kiutu wakiwa wanashirikiana kukabiliana na mgogoro huo, mahitaji ni makubwa mno kuliko misaada iliyoko.
Ukame unaifanya hali ya kiutu kuwa mbaya zaidi nchini Ethiopia ambako vita kati ya vikosi vya serikali na wapiganaji wa TPLF kaskazini mwa nchi hiyo vimewaacha mamilioni ya watu wakihitaji misaada.
Karibu watu milioni tatu katika maeneo ya Somali na Oromia Kusini wanakabiliwa na matatizo ya maji huku idadi nyengine ya watu isiyojulikana wakiwa wamelazimika kuyakimbia makaazi yao.
Shirika hilo linasema zaidi ya watu milioni 6.4 katika maeneo yaliyoathirika wanakadiriwa kuhitaji msaada wa chakula mwaka huu na wakati ambapo serikali ya Ethiopia na washirika wake wa misaada ya kiutu wakiwa wanashirikiana kukabiliana na mgogoro huo, mahitaji ni makubwa mno kuliko misaada iliyoko.
Ukame unaifanya hali ya kiutu kuwa mbaya zaidi nchini Ethiopia ambako vita kati ya vikosi vya serikali na wapiganaji wa TPLF kaskazini mwa nchi hiyo vimewaacha mamilioni ya watu wakihitaji misaada.
Karibu watu milioni tatu katika maeneo ya Somali na Oromia Kusini wanakabiliwa na matatizo ya maji huku idadi nyengine ya watu isiyojulikana wakiwa wamelazimika kuyakimbia makaazi yao.