Umoja wa Ulaya waipa Tanzania Msaada wa Billion 97.

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610



Ndugu zangu Watanzania,

Umoja wa ulaya umeipatia Tanzania Msaada wa Billion 97,Ambazo zitatumika katika maeneo matano ,ambapo miongoni mwa maeneo hayo ni pamoja na uboreshaji wa maendeleo endelevu katika Miji kama vile Kwanza,Tanga na Pemba.

Lakini pesa hizo zitatumika pia katika kuwawezesha wanawake na ushiriki wa wanawake hususani katika masuala ya uongozi.

Huu ni Muendelezo wa kuonyesha Imani kubwa ambayo Nchi ,jumuiya,Taasisi na mashirika mbalimbali yamekuwa nayo kwa nchi yetu tangia kuingia madarakani kwa Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan.

Sasa tunaendelea kupokea na kupata ushirikiano kutoka kila pembe ya Dunia.

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
 
Nazo zitaliwa na Viongozi wataongeza idadi ya mabasi ya mikoani
 
Wazungu wapo real sana Cha ajabu tumeng'ang'ania wachina. Asante mama kwa kutuheshimisha.
 
Aliyetoa haathiriki kwa sababu anajua kwann anatoa
 
Hizo Mwigulu ataongezea kwenye mtaji wake wa mabasi ya Easter
 
Baada ya huo msaada kuna raia watafukuzwa eneo flani ambalo halijafahamika mpaka sasa 🤣 ila liko karibu na hifadhi
 

Zitaishia kwenye mashangingi
Hivi kwanini hatushituki miaka nenda miaka rudi tunasaidiwa na hatusogei?
 
Dadeek
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…